Dr. Slaa afunika mkutano wa hamasa wa kujiandikisha BVR, Momba -Mbeya

Dec 11, 2010
3,321
6,328
Leo katibu mkuu wa CHADEMA Dr Willbroad Slaa amefanya mkutano mkubwa wa hadhara jimbo la Momba mkoani Mbeya.

Mkutano huo umetanguliwa na shughuli za mchana kutwa za kukagua zoezi la uandikishaji daftari la kudumu la wapiga kura kwa mfumo wa BVR kwenye maeneo mbalimbali ya jimbo hilo ambapo zoezi la uandikishaji linaendelea.

Hamasa ilikuwa kubwa na watu wengi waliojitokeza kwenye vituo mbalimbali na kujiandikisha hasa baada ratiba ya ziara hiyo kutangazwa kwenye vijiji na vitongoji mbalimbali wilayani hapo.

Kwenye mkutano mkubwa wa hadhara Dr Slaa aliwaambia wakazi wa Mbozi kuwa huu ni wakati muhimu sana kwao kwa kuhakikisha wanachuja kauli za wagombea mbalimbali watakao waomba ridhaa ili kuwachagua kushika nafasi mbalimbali.

Aliwatahadhirisha na kundi la wagombea walioanza kutangaza nia kwa kutoa kauli za hadaa wakati wamekuwa viongozi waandamizi wa serikali ambayo imeshindwa kuwaletea watanzania maisha bora kama ilivyo ahidi miaka 5 iliyopita.

Amewaambia huu sio wakati wa kusikia kauli za hadaa kuhusu matumaini bali niwakati wa Watanzania kupata kiongozi atakaye waletea watanzania uhakika wa kupata huduma mbalimbali za kijamii.

Amesema huu ni wakati wa vijana wa kitanzania kuwa na uhakika wa kusoma elimu ya juu wakiwa na uhakika wa mikopo na kuwa na uhakika wa kupata ajira mara baada ya kumaliza elimu kwenye vyuo mbalimbali. Amesema hii haipaswi kuwa safari ya matumaini kwa kina mama wanao kwenda kujifungua kwenye mahospitali bali ni wakati wa kina mama kwenda kwenye huduma za afya wakiwa na uhakika kuwa watapata dawa, vitanda na watarudi nyumbani salama mara baada ya kujifungua na kuendelea na maisha yao tofauti na ilivyo sasa ambapo ujauzito umekuwa kama jaribio la kifo kwa kina mama.

Alieleza utajiri wa raslimali ambazo Tanzania imebarikiwa lakini bado hazija wanufaisha watanzania kama ilivyopaswa kuwa. Amewahimiza wakazi wa Mbozi kuhakikisha wana tunza kadi zao za mpiga kura ili wafanye maamuzi sahihi kwenye uchaguzi mkuu ujao kwa kuachana na chama ambacho kimendelea kuwaacha watanzania wengi wakiishi kwenye lindi la umaskini wakiwa hawana hata uhakika wa kupata mlo au kujenga nyumba bora za kuishi.

Naomba kuwasilisha japo kwa kifupi kilicho jiri Momba.
 

Attachments

  • 1433091271530.jpg
    1433091271530.jpg
    126.2 KB · Views: 3,782
  • 1433091355370.jpg
    1433091355370.jpg
    66.4 KB · Views: 3,659
"ujauzito umekuwa kama jaribio la kifo kwa akina mama"

kazi ya CCM hiyo kuonyesha udhaifu na kushindwa kwa uongozi wao
 
watu wanatangaza nia ya kuwapeleka waTZ kwenye matumaini kama ni wagonjwa hivi, badala ya kuwa na uhakika wa kupata anachokitaka mTanzani. Baeleze Dr, baeleze hao wenye kuleta taifa kwenye matumaini badala ya uhakika.
 
Leo katibu mkuu wa CHADEMA Dr Willbroad Slaa amefanya mkutano mkubwa wa hadhara jimbo la Momba mkoani Mbeya.

Mkutano huo umetanguliwa na shughuli za mchana kutwa za kukagua zoezi la uandikishaji daftari la kudumu la wapiga kura kwa mfumo wa BVR kwenye maeneo mbalimbali ya jimbo hilo ambapo zoezi la uandikishaji linaendelea.

Hamasa ilikuwa kubwa na watu wengi waliojitokeza kwenye vituo mbalimbali na kujiandikisha hasa baada ratiba ya ziara hiyo kutangazwa kwenye vijiji na vitongoji mbalimbali wilayani hapo.

Kwenye mkutano mkubwa wa hadhara Dr Slaa aliwaambia wakazi wa Mbozi kuwa huu ni wakati muhimu sana kwao kwa kuhakikisha wanachuja kauli za wagombea mbalimbali watakao waomba ridhaa ili kuwachagua kushika nafasi mbalimbali.

Aliwatahadhirisha na kundi la wagombea walioanza kutangaza nia kwa kutoa kauli za hadaa wakati wamekuwa viongozi waandamizi wa serikali ambayo imeshindwa kuwaletea watanzania maisha bora kama ilivyo ahidi miaka 5 iliyopita.

Amewaambia huu sio wakati wa kusikia kauli za hadaa kuhusu matumaini bali niwakati wa Watanzania kupata kiongozi atakaye waletea watanzania uhakika wa kupata huduma mbalimbali za kijamii.

Amesema huu ni wakati wa vijana wa kitanzania kuwa na uhakika wa kusoma elimu ya juu wakiwa na uhakika wa mikopo na kuwa na uhakika wa kupata ajira mara baada ya kumaliza elimu kwenye vyuo mbalimbali. Amesema hii haipaswi kuwa safari ya matumaini kwa kina mama wanao kwenda kujifungua kwenye mahospitali bali ni wakati wa kina mama kwenda kwenye huduma za afya wakiwa na uhakika kuwa watapata dawa, vitanda na watarudi nyumbani salama mara baada ya kujifungua na kuendelea na maisha yao tofauti na ilivyo sasa ambapo ujauzito umekuwa kama jaribio la kifo kwa kina mama.

Alieleza utajiri wa raslimali ambazo Tanzania imebarikiwa lakini bado hazija wanufaisha watanzania kama ilivyopaswa kuwa. Amewahimiza wakazi wa Mbozi kuhakikisha wana tunza kadi zao za mpiga kura ili wafanye maamuzi sahihi kwenye uchaguzi mkuu ujao kwa kuachana na chama ambacho kimendelea kuwaacha watanzania wengi wakiishi kwenye lindi la umaskini wakiwa hawana hata uhakika wa kupata mlo au kujenga nyumba bora za kuishi.

Naomba kuwasilisha japo kwa kifupi kilicho jiri Momba.

ni muda wakuja kutupa darasa na sisi watu wa mkoa wa tanga kwa nini watu wa mbeya unawapendelea hivyo kila siku huko ina maana sisi watu wa tanga mmeamua kututoa sadaka kwa ccm?
 
Hayo maneno ya Dr.yanatosha kumkabidhi nchi.Amegusia nyanja zote muhimu kwa Mtanzania wasasa,siyo hao watangaza nia ambayo wanaonekana kusutana.
 
Kwa jinsi hali inavyokwenda hii mikoa inakwenda kufanya vizuri... Kagera..simiyu...shinyanga...Mara....Mwanza....Geita...Manyara....Ruvuma....Rukwa...Morogoro...Mbeya,

Kamati kuu chadema ilifanya maamuzi mazuri kuigawa Tanzania kikanda... Ccm watarajie wasichokijua

Kwa sasa kanda zinashindana... Ni kanda ipi itapata madiwani wengi? Wabunge wengi? Mwisho kura za Rais

Siku za nyuma tuliaminishwa kwamba chadema iko kaskazini.... Lakini maajabu yanakuja 25/10/2015
 
watu wanatangaza nia ya kuwapeleka waTZ kwenye matumaini kama ni wagonjwa hivi, badala ya kuwa na uhakika wa kupata anachokitaka mTanzani. Baeleze Dr, baeleze hao wenye kuleta taifa kwenye matumaini badala ya uhakika.

Kuna mtu aliwahi kuniaambia kwamba ukisikia mtu anaishi kwa matumaini ujue yuko kwenye dozi ya HIV natatizika isijekuwa hata sisi tuliyeanza safari ya matumaini tuko kwnye dozi bila kujijua.
 
Safari ya matumaini ni hadaa za mchana na hafiki popote.Chadema ni safari ya mabadiliko ya uhakika
 
Kwa jinsi hali inavyokwenda hii mikoa inakwenda kufanya vizuri... Kagera..simiyu...shinyanga...Mara....Mwanza....Geita...Manyara....Ruvuma....Rukwa...Morogoro...Mbeya,

Kamati kuu chadema ilifanya maamuzi mazuri kuigawa Tanzania kikanda... Ccm watarajie wasichokijua

Kwa sasa kanda zinashindana... Ni kanda ipi itapata madiwani wengi? Wabunge wengi? Mwisho kura za Rais

Siku za nyuma tuliaminishwa kwamba chadema iko kaskazini.... Lakini maajabu yanakuja 25/10/2015

Umenena kweli mkuu.

Mfumo wa kanda umekibeba sana chama na kupunguza mzigo wa uendeshaji kutoka makao makuu.

Ccm kama kawaida yao walifanya sana propaganda kuhusiana na mfumo huu kwa madai kwamba utawagawa watanzania.

Walivyo kuwa wanafiki kimyakimya wakaanzisha mfumo wa kanda 12 tofauti na zile 10 za Chadema. Wao walikuwa wamelenga kuhakikisha katiba yao ya kihuni itapita.

Tatizo huanza kubeza na kufanya propaganda ndio wanakuja kuiga.
 
Kuna mtu aliwahi kuniaambia kwamba ukisikia mtu anaishi kwa matumaini ujue yuko kwenye dozi ya HIV natatizika isijekuwa hata sisi tuliyeanza safari ya matumaini tuko kwnye dozi bila kujijua.
nimeipenda hii. ndivyo wanavyombiwa watu wenye ugonjwa hatari, wanapopata ushauri wa washauri au madaktari
 
Back
Top Bottom