Dr. Kyauke amkosoa Msajili wa vyama kuingilia mgogoro wa CUF

Kwani amemrudisha Lipumba ofisini na kumtangaza kama Mwenyekiti halaliwa CUF ni nani?
Hongera Dr.
Kila mtu ameona na kusikia

Msajili alipaswa kumkemea Prof. Lipumba kwa ubabe na vuruvu alizofanya na kuharibu mkutano wa CUF.Ameonekana wazi akisamama na kutetea uvunjifu wa amani na mtu aliyesababisha wakina mama kupigwa na kudhalilishwa huku mali za ukumbi zikiharibiwa na viti vikivunjwa na watu kupigwa hovyo.

Hata kama Prof. Lipumba alikua na haki basi angeenda mahakamani na sio kutumia vijana kujichukulia sjeria mikononi.
Msajili anaufundisha nini umma wa watamzania kuhusu umuhimu wa kuzitumia mahakama kudai haki badala ya kufanya vurugu na ubabe kama alivyofanya Lipumba na mabaunsa wake.

Msajili wa vyama hakusimama kama juji zaidi ya kuegemea upande mmoja bila kujua kuwa hata kiongozi wa nchi kwa mfano akiamua kujiuzulu mwenyewe halafu ghafla akachukua baadhi ya majenerali wa jeshi waliokua marafiki zake na kutangaza kuridi basi atakua ameiweka nchi hiyo kwenye hali ya vurugu kwani unapojiuzulu unawafanya wanachama wengine kuwa kwenye nafasi ya kujiandaa kisaikolojia kupata nafasi iliyoachwa wazi.

Lipumba alipaswa ajiweke pembeni ili baadae achukue form tena ya kugombea kama mwanachama mwingine na akikosa kura basi akae pembeni na sio kulazimisha kurudi kama vile mtu aliyekua amesafiri.

Katiba ilikaa kimya mana hakuna mtu aliyetegemea kuona kiongozi mwenye akili timamu akijiuzulu yeye mwenyewe kwa hiyari halafu anakuja tena kusema ametengua barua yake.
Suala la kutengua linajadiliwa na kukubaliwa au kukataliwa na sio lazima likubaliwe.
 
Msomi amkosoa Msajili wa Vyama

MHADHIRI Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Kitivo cha Sheria, Dk Onsmo Kyauke amekosoa kitendo cha Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi kuegemea upande katika mgogoro wa kisiasa ndani ya CUF, akidai ni udhalilishaji wa taaluma ya sheria nchini.

Dk Kyauke alisema hayo jana alipozungumza na JAMBO LEO Dar es Salaam, siku chache baada ya Ofisi ya Msajili kutoa barua kwa CUF kuruhusu kufungua akaunti kupitia kwa Mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba jambo alilosema ni kinyume na sheria na Katiba ya chama hicho.

Alisema kulingana na hali ya chama hicho, Msajili alipaswa kuwa mtu wa kati, kwani kufanya hivyo ni kuongeza mpasuko na kudhalilisha taaluma ya sheria nchini.

“Nadhani Msajili anapaswa kujiuzulu kwani kimsingi ameonesha udhaifu, ushahidi upo kwenye mgogoro wa CUF kwa kuandika barua ya ufunguzi wa akaunti kinyume na taratibu,” alisema.

Alisema kwa mujibu wa Katiba ya CUF, chombo chenye mamlaka ya kufungua akaunti ni Bodi ya Wadhamini ambapo benki husika inapaswa kupokea cheti cha usajili na si barua ya Msajili kama ilivyofanyika katika mchakato wa kufungua akaunti kupitia Lipumba.

Alisema katika mchakato huo baada ya benki kupokea maombi inapaswa kupeleka taarifa kwa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) ambao ndio unatoa taarifa kwa benki husika kuhusu wadhamini na nia ya kufungua akaunti.

Dk Kyauke pia alisema inasikitisha kuona Lipumba anafanya mikutano ya hadhara mikoani huku kukiwa na katazo la Jeshi la Polisi bila kuchukuliwa hatua.
Mimi nilishaacha kujitambulisha kama msomi kwenye inji hii.Eti jaji anafanya mambo ya ajabu kiasi hiki,nafikiri kuna haja ya tume ya mahakama kumvua ujaji huyu mtu maana naona ata watu ambao aliwahukumu wakati wa ujaji wake walionewa sana,sisemi kwamba ni mla rushwa ila nina mashaka nae.
 
Hii nchi ataa ukitaka ujinyamazie unashindwa kwa madudu yanayo chipuka .nikama mtu anakujambia mdomoni .itafika maali wasomi watadharauliwa kabisa .heri yake Dr Kyauke kwa kutetea taaluma angalau
 
Mh Yangu Macho
 

Attachments

  • 1476357403700.jpg
    1476357403700.jpg
    95.6 KB · Views: 31
NNi aibu kuwa na wasomi kwa aina ya mtungi na propesa. Wamejivua nguo hadharani na watanzania wameshaelewa ni nini kinaendelea. Propesa anatumika na watawala kufifisha nguvu imara ya wapinzani. Ukishanza kula nyama ya watu bais huwezi kuacha ndio kitu kinachoendelea kwa propesa na kwa msaada wa mtugi na kwa baraka ya mamlaka za juu.
 
hongera dr kyauke kwa kutetea taaluma na elimu ya tanzania,maana imekua shida kwa nchi zingine kuamini wasomi wa tanzania kwa sasa.ndio maana tumebaki kulilia tu kwenye soko la ajira kimataifa sababu ya wasomi aina akina mtungi ,lipumba na wenzie.inatia shaka kama kweli huyu mtungi anastahili kuitwa jaji maana jaji ni mtu anaeshimika na kuaminika sana katika jamii yoyote ile.kwanini wasimnyang'anye ujaji abaki na nafasi ya msajili ili kulinda hadhi ya majaji wetu?
Ndugu mimi nadhani majaji waunde chombo kitakacho fuatilia weledi,na maadili ya wale wote walio beba title ya ujaji mpaka wanakufa, katika kipindi cha maisha yao wakifanya kitu chochote nje ya maadili ya kijaji basi wavuliwe ujaji. Kuhusu uprofesor hatuwezi kuongelea sababu hiyo ni international pia wengi baadae wanaburunda kwa kutoa matokeo feki ya kitafiti yaliyo gharimu fedha kibao, ni jukumu la chuo kilicho mpa hiyo title.
 
Wana mpango wa kugawana pesa mutungi na propesa pumba na ndio maana yupo upande wa pumba mutungi ni mwizi tu hana taaluma ya sheria vyeti vyake ni vyakufoji
 
Huwa nawaza hivi mtu kam huyu hana mke anaeweza kumshauri kuwa anayofanya ni insanity!?Huyu mke wake haoni aibu kwa haya anayofanya mume wake?Au hata watoto wake na ndugu zake hawamshauri kabisa????Nahisi na yeye atakuwa hashauriki...such a shame
 
Msajiri line za SIMU jaji Mitumba amesomea chuo gani na ujaji alipataje??Au mke wake anafanya kazi serikalini?
 
Kwani amemrudisha Lipumba ofisini na kumtangaza kama Mwenyekiti halaliwa CUF ni nani?
Hakumkemea.
Alipaswa amkemee kwa vitendo vyake.
Na pia kama jaji na mwanasheria aliyebobea alipaswa amshauri Prof. Lipumba aende mahakamani kudai haki yake aliyonyimwa kama ipo na sio kumsaidia na kumtetea kwa kuamua kutumia vijana na kujirudisha ofisini kwa nguvu.

Ndio maana kuna mahakama ambayo ipo kwa ajili ya kutoa haki na sio kila kitu kutumia nguvu na ushabiki usiofaa jujenga utawala wa sheria.

Haihitaji hata elimu darasa la tatu kujua kuwa Lipumba amekosea na pia Msajili amekosea kuegemea upande mmoja tena upande wa mtu mmoja na kutelekeza maelfu ya wanachama na mamia ya viongozi wa CUF walioamua kumkatalia Lipumba kurudi kienyeji kabisa kama vile ana hati miliki ya uenyekiti wa CUF!!
 
Tusikalilishwe hapa,msajili alishakana kuhusu kuhusu kufunguliwa kwa account mpya,harafu hilo la lipumba ni makosa yao wenyewe Cuf,walikuwa wapi kusaini barua ya kujiuzuru miezi yote hiyo hadi mtu anakuja kutengua maamuzi yake? Harafu eti wanamvua uanachana baada ya kutengua? Huku ni kutotumia akili kabisa.lipumba atashinda tu hii vita trust me
 
Back
Top Bottom