DPP Biswalo Mganga: Mbunge Lema kuchukuliwa hatua kwa kupotosha vifo vya watu 14 Manyoni, Hatuwezi kuwa na Taifa la watu wazushi na wazua taharuki

mwanamwana

JF-Expert Member
Aug 1, 2011
1,076
4,113
Akizungumza leo Machi 12, 2020, DPP Mganga amesema kuwa taarifa alizozitoa Lema zimeleta taharuki kwa Watanzania na kuwafanya wasiishi kwa amani na kwa jambo hilo lazima atalichukulia hatua na kwamba alichokisema Mbunge Lema ni kauli za kisiasa, kwani matukio hayo yote yalikwishachukuliwa hatua stahiki.


DPP amesema... 'Nukuu'

Na kama yeye aliona hawa wamechinjwa na anawajua waliowachinja kwa mujibu wa sheria yeye anawajibika kutoa taarifa Polisi, Lema naomba ajitokeze aje kuniambia ni lini alienda kutoa taarifa kwamba kuna watu wanachinjwa na hatua hazikuchukuliwa

Hata kama sifa za kisiasa basi tuwe na mipaka, kuna marehemu mwingine kifo chake kimesababishwa na ajali ya pikipiki lakini mheshimiwa Lema katika taarifa yake amesema amechinjwa. Mwingine alishambuliwa na fimbo, mateke na ngumi lakini anataja wamechinjwa huu ni uongo.

Kwa hili lazima nitachukua hatua hatuwezi kuendelea na upotoshaji na uvunjifu wa namna hii. Halafu watu wanatoka na kusema wanasiasa wa upinzani wanaonewa wakati wanafanya upuuzi wa namna hii, haiwezekani, tusijifiche kwenye siasa kwa ajili ya kuvuruga amani, "amesema Mganga.

Pia soma
> Lema: Nimepewa orodha ya viongozi wa CHADEMA waliouliwa Manyoni na Polisi kutofanya uchunguzi wowote

> Godbless Lema aitwa na Ofisi ya RCO Arusha, asafirishwa na Polisi usiku kwenda Singida

Lema amjibu DPP Mganga Biswalo, amtaka aache kutisha watu
 
.
IMG-20200312-WA0041.jpeg


Jr
 
Bahati mbaya kila kona ya nchi ni majanga kwa watu kupotea, kuumizwa, kutekwa nk

At least wangeonesha kutatua matatizo

Tumeona nguvu inayotumika kwa kutafuta waliomzulu mzee wetu comledi Philip Mangula. Nijambo jema sana na hili lifanyike kwa wote sio kwa ccm tu.
 
Dpp anachukua hatua hizo akizingatia Rangi itikadi na Ukabila maana ukiacha vifo alivyotaja Lema kuna vifo vingii tu vya watu kuchinjwa na polisi hawajashika mtu yeyote na dpd haongei chochote
 
DPP, hayo ni maelekezo kwa mahakama? Hivi mmeisha kamilisha uchunguzi, Au ndio moja ya hatua mnazochukuaga kuchelewesha kesi kabla ya kumbadilishia mashitaka?
 
Back
Top Bottom