Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 573
- 2,553
Kwa mujibu wa Mazungumzo ya Msemaji Mkuu wa Serikali yanayoendelea Clubhouse Usiku huu, Julai 1, 2023, Gerson Msigwa akiwa na Msemaji Mwingine (Mwanasheria) anayefahamika kwa jina la Mohamed Salum wamesema IGA ni mkataba wa Kimataifa unaoitaka Serikali kuu pindi inapofanya majadiliano na nchi nyingine kusaini, na haimaanishi mkataba huo tayari umeanza kutekelezwa.
Aidha, baada ya maridhiano hayo, makubaliano hupaswa kupelekwa Bungeni ili upitishwe na wabunge kwa kuwa hulenga kubadilisha baadhi ya sheria za Nchi.
Ili mkataba huu uanze kufanya kazi ni lazima mabadilishano ya hati za Mkataba yafanyike. Hivyo, kwa sasa DP world hawajaanza kufanya kazi yoyote nchini na watu hawapaswi kudanganywa au kupotoshwa kuwa DP World tayari wameshaanza kufanya kazi wakati mabadilishano ya hati bado hayajafanyika.
Aidha, baada ya maridhiano hayo, makubaliano hupaswa kupelekwa Bungeni ili upitishwe na wabunge kwa kuwa hulenga kubadilisha baadhi ya sheria za Nchi.
Ili mkataba huu uanze kufanya kazi ni lazima mabadilishano ya hati za Mkataba yafanyike. Hivyo, kwa sasa DP world hawajaanza kufanya kazi yoyote nchini na watu hawapaswi kudanganywa au kupotoshwa kuwa DP World tayari wameshaanza kufanya kazi wakati mabadilishano ya hati bado hayajafanyika.