Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Na Tumaini Makene
SAKATA la kashfa ya kampuni tata ya Dowans ambayo inatakiwa kulipwa sh. bilioni 94 jana lilitikisa katika mdahalo wa wasomi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ambako lilielezwa kuwa ni 'sehemu ndogo ya familia kubwa ya ufisadi' unaoendelea nchini ambayo kama haitachukuliwa hatua stahili, itahatarisha amani na utulivu nchini.
Ilielezwa kuwa kashfa hiyo ni dalili ya tatizo kubwa katika sekta mbalimbali ikihusisha mikataba ya kilaghai, huku ikiathiri maendeleo ya nchi kisiasa na kiuchumi, kiasi ambacho viongozi wameshindwa kutumikia umma wa Watanzania, badala yake wanatumikia maslahi binafsi.
Kashfa zingine zilizotajwa kukuhusishwa katika hicho kinachoitwa 'familia ya ufisadi' zilikuwa ni pamoja na ununuzi wa rada, mikataba ya IPTL, ubinafsishaji wa mali za umma, matatizo ya ardhi ambapo wawekezaji wamekuwa na sauti kubwa kuliko wananchi wa maeneo husika, ukitajawa mgogoro wa wakulima na wawekezaji huko Babati.
Hayo yalisemwa jana katika mdahalo juu ya sakata la Dowans, ulioitishwa na Chama cha Wanataaluma UDSM (UDASA), ambapo pia ilitolewa njia mbadala ya kutatua matatizo kama ya Dowans kwa kutaifisha mali za wahusika.
Akiwasilisha maada yake juu ya sakata la Dowans katika mlengo wa Sayansi ya Siasa, Bw. Bashiru Ally ambaye pia ni mhadhiri wa idara hiyo UDSM, alisema kuwa kashfa hiyo ni sehemu ya familia kubwa ya ufisadi inayoendelea kuitafuna nchi katika nyanja ya uchumi na siasa, kiasi cha kupandisha hasira za makundi mbalimbali ya watu katika jamii.
Kwa upande wake, Dkt. Adolf Mkenda aliwasilisha mada yake kwa mlengo wa uchumi, alisema kuwa soko huria haliwezi kuwa sababu ya kulaumiwa pale kashfa kama hizo zinazonuka makosa ya jinai kama rushwa, zinapotokea, bali hiyo ni dalili ya watumishi wa umma wakishirikiana na wale wa sekta binafsi kujinufaisha wao.
Akiwasilisha mada yake kwa mlengo wa kisheria, kwa kutoa historia ya Dowans, kuanzia Richmond, mpaka hukumu ya kesi ya ICC, Bw. Jesse James kutoka Shule Kuu ya Sheria Chuo Kikuu Dar es Salaam, alisema kuwa mkataba ulioifikisha nchi katika sakata la Dowans hauna tofauti na ile iliyokuwa ikisainiwa na machifu wajinga, wakati wa enzi za kuingia ukoloni (Chifu Mangungo wa Msovero).
Kwa upande wake, mwanasheria na mwanaharakati Bw. Tundu Lissu alisema kuwa wanasheria waliowakilisha upande wa serikali wakati wa uendeshaji kesi, hawakuzungumza dalili za uwepo wa rushwa katika sakata zima la Dowans, kuanzia katika Kampuni ya Richimond, suala ambalo lingeweza kusababisha ICC isisikilize kesi hiyo, kwa mujibu wa mikataba ya kimataifa.
Wakati huo huo Majira limepata habari ya kuwepo kwa maandalizi ya maandamano ya amani ya wanafunzi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam ambapo moja ya hoja zitakuwa ni kudai ongezeko la fedha za kujikimu kutoka sh. 5,000 ya sasa mpaka sh. 10,000.
Habari kutoka vyanzo mbalimbali zilisema kuwa hoja nyingine ambayo imewasukuma kuandaa maandamano hayo ni kupinga tamko la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) la kutaka kuvunjwa kwa Uongozi wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kwa madai kuwa umeshindwa kuwahudumia wanafunzi inavyotakiwa.
Alisema kuwa tatizo la mikopo na migomo ya wanafunzi vyuo vikuu ni mfumo wa uanzishwaji wa bodi yenyewe unaotokana na serikali kushindwa kusimamia na kuiwezesha vya kutosha pamoja na uzembe wa uongozi wa baadhi ya vyuo na Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), hasa katika kuwasilisha taarifa za wanafunzi mapema.
SAKATA la kashfa ya kampuni tata ya Dowans ambayo inatakiwa kulipwa sh. bilioni 94 jana lilitikisa katika mdahalo wa wasomi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ambako lilielezwa kuwa ni 'sehemu ndogo ya familia kubwa ya ufisadi' unaoendelea nchini ambayo kama haitachukuliwa hatua stahili, itahatarisha amani na utulivu nchini.
Ilielezwa kuwa kashfa hiyo ni dalili ya tatizo kubwa katika sekta mbalimbali ikihusisha mikataba ya kilaghai, huku ikiathiri maendeleo ya nchi kisiasa na kiuchumi, kiasi ambacho viongozi wameshindwa kutumikia umma wa Watanzania, badala yake wanatumikia maslahi binafsi.
Kashfa zingine zilizotajwa kukuhusishwa katika hicho kinachoitwa 'familia ya ufisadi' zilikuwa ni pamoja na ununuzi wa rada, mikataba ya IPTL, ubinafsishaji wa mali za umma, matatizo ya ardhi ambapo wawekezaji wamekuwa na sauti kubwa kuliko wananchi wa maeneo husika, ukitajawa mgogoro wa wakulima na wawekezaji huko Babati.
Hayo yalisemwa jana katika mdahalo juu ya sakata la Dowans, ulioitishwa na Chama cha Wanataaluma UDSM (UDASA), ambapo pia ilitolewa njia mbadala ya kutatua matatizo kama ya Dowans kwa kutaifisha mali za wahusika.
Akiwasilisha maada yake juu ya sakata la Dowans katika mlengo wa Sayansi ya Siasa, Bw. Bashiru Ally ambaye pia ni mhadhiri wa idara hiyo UDSM, alisema kuwa kashfa hiyo ni sehemu ya familia kubwa ya ufisadi inayoendelea kuitafuna nchi katika nyanja ya uchumi na siasa, kiasi cha kupandisha hasira za makundi mbalimbali ya watu katika jamii.
Kwa upande wake, Dkt. Adolf Mkenda aliwasilisha mada yake kwa mlengo wa uchumi, alisema kuwa soko huria haliwezi kuwa sababu ya kulaumiwa pale kashfa kama hizo zinazonuka makosa ya jinai kama rushwa, zinapotokea, bali hiyo ni dalili ya watumishi wa umma wakishirikiana na wale wa sekta binafsi kujinufaisha wao.
Akiwasilisha mada yake kwa mlengo wa kisheria, kwa kutoa historia ya Dowans, kuanzia Richmond, mpaka hukumu ya kesi ya ICC, Bw. Jesse James kutoka Shule Kuu ya Sheria Chuo Kikuu Dar es Salaam, alisema kuwa mkataba ulioifikisha nchi katika sakata la Dowans hauna tofauti na ile iliyokuwa ikisainiwa na machifu wajinga, wakati wa enzi za kuingia ukoloni (Chifu Mangungo wa Msovero).
Kwa upande wake, mwanasheria na mwanaharakati Bw. Tundu Lissu alisema kuwa wanasheria waliowakilisha upande wa serikali wakati wa uendeshaji kesi, hawakuzungumza dalili za uwepo wa rushwa katika sakata zima la Dowans, kuanzia katika Kampuni ya Richimond, suala ambalo lingeweza kusababisha ICC isisikilize kesi hiyo, kwa mujibu wa mikataba ya kimataifa.
Wakati huo huo Majira limepata habari ya kuwepo kwa maandalizi ya maandamano ya amani ya wanafunzi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam ambapo moja ya hoja zitakuwa ni kudai ongezeko la fedha za kujikimu kutoka sh. 5,000 ya sasa mpaka sh. 10,000.
Habari kutoka vyanzo mbalimbali zilisema kuwa hoja nyingine ambayo imewasukuma kuandaa maandamano hayo ni kupinga tamko la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) la kutaka kuvunjwa kwa Uongozi wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kwa madai kuwa umeshindwa kuwahudumia wanafunzi inavyotakiwa.
Alisema kuwa tatizo la mikopo na migomo ya wanafunzi vyuo vikuu ni mfumo wa uanzishwaji wa bodi yenyewe unaotokana na serikali kushindwa kusimamia na kuiwezesha vya kutosha pamoja na uzembe wa uongozi wa baadhi ya vyuo na Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), hasa katika kuwasilisha taarifa za wanafunzi mapema.