Does it matter?

PetCash

JF-Expert Member
Mar 20, 2012
1,997
1,999
So, niko hospital na huyu Jamaa ambaye naweza kusema ni rafiki muhimu sana kwangu. Tunaendana kwenye baadhi ya mambo ila ana hii tabia ambayo si nzuri kwa kweli na nimesha jaribu kumuonya(at least kila mtu wa karibu kafanya hivyo) ila ndo vile dunia yake chaguo lake. Kwa hiyo nika'turn blind eye to his habit'. Tabia ya kutoka na huyu mdada wa kazini kwetu huku nyumbani ana mke. Cha kushangaza mkewe alishanibana sana nimpe hint kama mumewe ana smol haus, nikamjibu-majibu ya mahusiano yenu anayo mumeo u should ask him(kwa hiyo secretly nilihisi kama mkewe anajua ila hamjui mhusika).

Sasa bwana gafla wakaja mkewe na huyo mdada wa job wameleta chakula kwa jamaa kwa mida tofauti ila mkewe ndo alimkuta bi shosti eneo la tukio. Nikawa nimemkinga jamaa kwa sababu ni mgonjwa (alisukumwa kidogo tu na gari akaangukia mkono, so kuna some sort of a fracture) ili kimbembe kikianza wasije umalizia huo mkono. Basi wadada wenyewe hawapigani wala kusemeshana ni mifyonzo na kuangaliana with a kill wish mwanzo mwisho.

Honestly I was suprised kwamba mke ameshajua(au alikuwa anajua) and dont care enough to show!
Basi ikabidi nimshindikize wife wake hadi home baada ya sisi wote kukickiwa out of hospital ili hao wadada wasijepigana huko njiani na hiyo ni baada ya mke
kwa 'bahati mbaya' kumwaga chakula alicholeta yule dada . Ndani ya gari huyu mke wa jamaa anamponda huyo smol haus.
small haus gani mhudumu wa chai, nyuma pasi (if u know what she means), sura mbaya kisha hajui kuvaa, mchafu!

So profile ya mwizi wako wa mahusiano inajalisha kwenye decision za nini ufanye baada ya kugundua?
 
mara nyingi mwanamke akigundua mwizi wake ni nani jambo la kwanza uwa ni kujikompea na uyo mwizi kwa muonekano wa nje, na mara nyingi wezi wanakuwaga wabovu kuliko wenye mali halali, hii sijui kwa nini ila ndo kautafiti kangu kadogo nilikodiskava
 
huyo mwizi mpumbavu, unaiba halafu unajionyesha ili iweje? Ukila na kipofu usimshike mkono
 
Ndio maana tunasema ikitaka kula nguruwe basi japo chagua alienona.Ukiwa na nyumba ndogo sheria moja wapo ni kwamba mkeo asijue,kwani akijua either aseme kitu au anyamaze wanawake wengi huwa wanalipiza kisasi.Tell your freind to be careful ataingiza hiyo ndoa kwenye migogoro.
 
Ila mara nyingi wanaume wanapowasaliti wake zao hukimbilia wanawake mashangingi,au utakuta mwanamke mbovu mpk ukimwangalia mkewe unasikitika coz mkewe ni mrembo na mchakarikaji..
 
mapenzi hayana kanuni wakuu.... Waweza kuta kitu kibaya lakini very cared kuliko mama mwenye nyumba...
 
Pet Cash mie naamini habari za cheating kwa wanaume na wanawake hupokelewa tofauti...

Kwa mwanaume itaanza Mshangao, Hasira, Kinyaa na sometimes kutoamini kuwa mke wake kamcheat na kutoka nje. Wanaume wengi wesha jua wake za jamaa kibao wanacheat na kutoka nje ya ndoa ILA hakuna ambae anataka aamini kuwa mke wake anaweza fanya hivo sababu kila mmoja anataka aamini mke wake ni spesho (ni wachache ambao wanaweza dhani kuwa mkewe anaweza cheat, labda ziwe zile ndoa za kudimba na walikwapuana vichochoroni na kwenye bar).

Kwa mwanamke akisika mume wake kacheat (beleive me you ni wachache sana hushangaa to the extent ambayo wanaume hushangaa). In most cases wanawake wengi itaanza roho kuuma (hakuna mfano), then inafuata hasira ambayo imeambatana na curiousity; Hii uzaa maswali kama yukoje (hasa is she beautiful or young)? ana nini cha ajabu? Then ukishamjua mara nyingi hu determine hata ambavo unaweza ku react...

Back to the Topic;

Wanawake tunaumia sana ukisikia mumeo katoka nje... Ila yote tisa, inauma zaidi ukisikia kuwa huyo mwanamke ni nyumba ndogo. Na in most cases maamuzi yetu hutegemea nafasi yetu katija maisha yetu, familia yetu na huyo mume wako. Huyo mwanamke kama kweli kajua kuwa huyo mwanamke ndie nyumba ndogo na kawa mpole ana haya yafuatayo:-


  • Aidha ndio wale ambao ni tegemezi, bila huyo mume ni hajui pa kuanzia ama kuishia.
  • Aidha ndio wale ambao kwa kweli hajitambui, anaona kama uthamani wake unakuwa defined in the lines ya kuwa a huyo mume.
  • Au maybe ndio kupenda... Anapenda hadi hajali nini mume wake anamfanyia.

Upande wa mume

Hana busara kabisa... Naona ndio mana hapo juu Kaizer kamkumbusha The Boss atoe mwongozo. Kweli kabisa on a serious note PetCash mpe hio nakala huyo rafiki yako baada ya kuipata kwa Boss... Hana busara. Yeye kama mume anaumwa alijua dhahiri mke wake alikuwa anakuja hio asubuhi, huyo mke mdogo haikupaswa aje muda huo... otherwise kama alikuwa anakuja na kuondoka hapo hapo. Mbaya zaidi (labda kama sijaelewa) kakutwa na mke wa jamaa alafu bado yeye ndio kabaki.
 
Last edited by a moderator:
So, niko hospital na huyu Jamaa ambaye naweza kusema ni rafiki muhimu sana kwangu. Tunaendana kwenye baadhi ya mambo ila ana hii tabia ambayo si nzuri kwa kweli na nimesha jaribu kumuonya(at least kila mtu wa karibu kafanya hivyo) ila ndo vile dunia yake chaguo lake. Kwa hiyo nika'turn blind eye to his habit'. Tabia ya kutoka na huyu mdada wa kazini kwetu huku nyumbani ana mke. Cha kushangaza mkewe alishanibana sana nimpe hint kama mumewe ana smol haus, nikamjibu-majibu ya mahusiano yenu anayo mumeo u should ask him(kwa hiyo secretly nilihisi kama mkewe anajua ila hamjui mhusika).

Sasa bwana gafla wakaja mkewe na huyo mdada wa job wameleta chakula kwa jamaa kwa mida tofauti ila mkewe ndo alimkuta bi shosti eneo la tukio. Nikawa nimemkinga jamaa kwa sababu ni mgonjwa (alisukumwa kidogo tu na gari akaangukia mkono, so kuna some sort of a fracture) ili kimbembe kikianza wasije umalizia huo mkono. Basi wadada wenyewe hawapigani wala kusemeshana ni mifyonzo na kuangaliana with a kill wish mwanzo mwisho.

Honestly I was suprised kwamba mke ameshajua(au alikuwa anajua) and dont care enough to show!
Basi ikabidi nimshindikize wife wake hadi home baada ya sisi wote kukickiwa out of hospital ili hao wadada wasijepigana huko njiani na hiyo ni baada ya mke
kwa 'bahati mbaya' kumwaga chakula alicholeta yule dada . Ndani ya gari huyu mke wa jamaa anamponda huyo smol haus.
small haus gani mhudumu wa chai, nyuma pasi (if u know what she means), sura mbaya kisha hajui kuvaa, mchafu!

So profile ya mwizi wako wa mahusiano inajalisha kwenye decision za nini ufanye baada ya kugundua?

sana aisee!mno!yani kupita maelezo!
 
mara nyingi mwanamke akigundua mwizi wake ni nani jambo la kwanza uwa ni kujikompea na uyo mwizi kwa muonekano wa nje, na mara nyingi wezi wanakuwaga wabovu kuliko wenye mali halali, hii sijui kwa nini ila ndo kautafiti kangu kadogo nilikodiskava
Hapo kwenye blue Mkuu uko sahihi kabisa lkn kwa mwonekano wa nje,kwa yale mengine wezi wanakuwaga wazuri by far compared na wenye mali.
 
Ila mara nyingi wanaume wanapowasaliti wake zao hukimbilia wanawake mashangingi,au utakuta mwanamke mbovu mpk ukimwangalia mkewe unasikitika coz mkewe ni mrembo na mchakarikaji..


hapa nyie mnazungumzia uzuri wa nje ndo mana mnasema mara nyingi mke ni mzuri kuliko vimada...ila mnasahau kua kimada anaweza kua anajua mambo ya ndani ya nyumba kuliko mke mwenyewe na hapo ndio wanapoliwagwa...sasa wewe fikiria kama mke anaibiwa na housegirl wake wa nyumbani ndio itakua hao wanawake wa maofsini?
 
mara nyingi mwanamke akigundua mwizi wake ni nani jambo la kwanza uwa ni kujikompea na uyo mwizi kwa muonekano wa nje, na mara nyingi wezi wanakuwaga wabovu kuliko wenye mali halali, hii sijui kwa nini ila ndo kautafiti kangu kadogo nilikodiskava

Kuna wezi wengine ukiwaona duh! kama wewe ni msuluhishi unashikwa na kigugumizi
 
It should'nt matter.
The only thing that should matter ni kuwa amecheat!

Na mwanamke mzuri zaidi yako au mbaya zaidi yako haibadilishi maana kuwa mwanaume sio mwaminifu.

Sawa suppose amecheat na mwanamke mzuri zaidi yako, kwa maoni yangu inaweza kukufanya ujifeel inferior kiasi na labda ukaanza kuiga uvaaji wake, make ups zake au hata upuuzi wake (case mbaya kutoa tigo)

Haya akicheat na 'mbaya' zaidi yako; ndio kama hivyo unaanza kumsagia na huenda bado ukajiuliza alikuwa anafuata nini huko na bla bla zingine.

Kwangu mimi haijalishi labda awe amebaka mnyama and l will be concerned na afya yake ya kichwani au roho gani iliyo muingia!
 
It should'nt matter.
The only thing that should matter ni kuwa amecheat!

Na mwanamke mzuri zaidi yako au mbaya zaidi yako haibadilishi maana kuwa mwanaume sio mwaminifu.

Sawa suppose amecheat na mwanamke mzuri zaidi yako, kwa maoni yangu inaweza kukufanya ujifeel inferior kiasi na labda ukaanza kuiga uvaaji wake, make ups zake au hata upuuzi wake (case mbaya kutoa tigo)

Haya akicheat na 'mbaya' zaidi yako; ndio kama hivyo unaanza kumsagia na huenda bado ukajiuliza alikuwa anafuata nini huko na bla bla zingine.

Kwangu mimi haijalishi labda awe amebaka mnyama and l will be concerned na afya yake ya kichwani au roho gani iliyo muingia!

Hahahahaha!

Kwani mtu akibaka mnyama nae kacheat?

Eti mwizi wako ni mnyama!
 
Back
Top Bottom