Crashwise
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 22,227
- 8,735
Licha ya kuzuiliwa na polisi CCM kufanya mkutano na mapokezi, mbunge wa Arusha mjini kufanya mkutano jioni hii kwenye uwanja wa Baruti.
Kwa sasa magari ya yanapita mitaani yakitangaza juu ya mkutano huo....
===============
Mkutano kwa sasa unaendelea japo umetangazwa kwa saa moja na sasa katibu wa Chadema mkoa wa DODOMA anaongea
Kwa sasa magari ya yanapita mitaani yakitangaza juu ya mkutano huo....
RPC akiwa ametoa taarifa kwa CHADEMA kuhusu zuio la mkutano ambao ulikuwa uhutubiwe na Lema kwa sababu zifuatazo:
1. Polisi hawatoshi kwa sababu ya bunge(itifaki)
2. Eneo ni dogo watu watakuwa wengi sana (BARUTI-pale chako ni chako)
Mara baada ya taarifa hiyo mheshimiwa Lema amekuja ofisi za CHADEMA Mkoa na kuwaambia makamanda watangaze mkutano utakuwepo kwa sababu zifuatazo:
1. Wakikubali kuahirisha mkutano, maana yake nikuwa CHADEMA haitafanya mikutano DODOMA maana kwa mwaka bunge linakaa zaidi ya mara moja
2. RPC hana mamlaka ya kuzuia mkutano (mwenye mamlaka ni OCD)
3. Kuhusu idadi ya watu, ana uhakika gani watu watakuwa wengi? (kwani RPC ndo atawaleta?)
Baada ya maelezo hayo gari la CHADEMA limeingia mtaani kutangaza mkutano. Lema anasema wakikamata gari tuyalifuata polis.
Nina Picha, Audio na video za kamanda Lema akiwasili na kutoa tamko hilo akiwa Ofisi za CHADEMA.
Naelekea kwenye mkutano nitakuwa nawapa updates.
NOTE: DODOMA watahimili mikiki ya Polisi? Lets wait and see.
===============
Mkutano kwa sasa unaendelea japo umetangazwa kwa saa moja na sasa katibu wa Chadema mkoa wa DODOMA anaongea