Dk. Slaa: Sigombei urais

Status
Not open for further replies.

Habarindiyohiyo

JF-Expert Member
Aug 11, 2008
263
13
Dk. Slaa: Sitagombea urais

na Deogratius Temba

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilibrod Slaa, amesema hana mpango wa kugombea urais katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2010.

Dk. Slaa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Karatu kwa mihula miwili mfululizo, alisema, jukumu alilonalo katika maisha yake ni kuwatumikia watu wa Karatu ambao wamemwamini na kumpa nafasi hiyo na si kugombea urais.

Akizungumza katika kituo cha Televisheni cha TBC1, katika kipindi cha Jambo Tanzania, Dk. Slaa alisema yeye ni mtumishi wa watu wa Karatu na hawezi kuwaacha kwenda kugombea urais.

“Wananchi wangu waondoe wasiwasi, na wala wasijenge hisia kuwa nitasimama kuwania urais, wala sina wazo hilo, wala sijawahi kuota kuwa rais wa nchi hii, na sitakubali kuwasaliti wananchi wangu kwa kuacha kuwatumikia kama mbunge,” alisema.

Akizungumzia kuhusu CHADEMA kusimamisha mgombe urais katika uchaguzi mkuu ujao, Dk. Slaa alisema lazima wamsimamishe mtu kwani chama hicho kinaaminiwa na kupendwa na wananchi.

“Ni lazima CHADEMA tutamsimamisha mtu katika nafasi ya urais na kuendelea kupigania haki ya Watanzania mpaka mwisho,” aliongeza Dk. Slaa.

Akizungumzia suala la kuungana kwa vyama vya upinzani katika uchaguzi mkuu ujao, Dk. Slaa alisema CHADEMA kitaungana na chama chochote chenye nia ya dhati ya kutaka kulikomboa taifa, na kilichojijengea sera yakinifu na imara zinazokubalika na wananchi.

“Kuungana tutaungana, ila tutaungana na watu ambao ni ‘serious’ (makini), wenye mipango, tutaelekezana tukiwa mezani kama ni nini tunataka kufanya, na kila mmoja aseme ana nini, lakini haya yatafanyika wakati muafaka ukifika,” alisema.

Aliongeza kuwa, lengo la vyama vya upinzani, hasa CHADEMA, si kuitoa CCM madarakani tu, ni kuungana, maana kuna kitu cha msingi kinatakiwa kufanyika kwa umoja ili maisha ya Watanzania yabadilike na kufanyiwa mabadiliko ya kweli katika maisha ya watu.
 
Dr. muda bado, 2010 ikifika usisite waweza gombea vilevile kama chama chako kikikupendekeza. Hutakuwa umewasalitii watu wa karatu kwani hapo ndipo utaweza kuwasaidia vizuri zaidi.
 
Dk. Slaa: Sitagombea urais

na Deogratius Temba

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilibrod Slaa, amesema hana mpango wa kugombea urais katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2010.

Dk. Slaa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Karatu kwa mihula miwili mfululizo, alisema, jukumu alilonalo katika maisha yake ni kuwatumikia watu wa Karatu ambao wamemwamini na kumpa nafasi hiyo na si kugombea urais.

Akizungumza katika kituo cha Televisheni cha TBC1, katika kipindi cha Jambo Tanzania, Dk. Slaa alisema yeye ni mtumishi wa watu wa Karatu na hawezi kuwaacha kwenda kugombea urais.

"Wananchi wangu waondoe wasiwasi, na wala wasijenge hisia kuwa nitasimama kuwania urais, wala sina wazo hilo, wala sijawahi kuota kuwa rais wa nchi hii, na sitakubali kuwasaliti wananchi wangu kwa kuacha kuwatumikia kama mbunge," alisema.

Akizungumzia kuhusu CHADEMA kusimamisha mgombe urais katika uchaguzi mkuu ujao, Dk. Slaa alisema lazima wamsimamishe mtu kwani chama hicho kinaaminiwa na kupendwa na wananchi.

"Ni lazima CHADEMA tutamsimamisha mtu katika nafasi ya urais na kuendelea kupigania haki ya Watanzania mpaka mwisho," aliongeza Dk. Slaa.

Akizungumzia suala la kuungana kwa vyama vya upinzani katika uchaguzi mkuu ujao, Dk. Slaa alisema CHADEMA kitaungana na chama chochote chenye nia ya dhati ya kutaka kulikomboa taifa, na kilichojijengea sera yakinifu na imara zinazokubalika na wananchi.

"Kuungana tutaungana, ila tutaungana na watu ambao ni ‘serious' (makini), wenye mipango, tutaelekezana tukiwa mezani kama ni nini tunataka kufanya, na kila mmoja aseme ana nini, lakini haya yatafanyika wakati muafaka ukifika," alisema.

Aliongeza kuwa, lengo la vyama vya upinzani, hasa CHADEMA, si kuitoa CCM madarakani tu, ni kuungana, maana kuna kitu cha msingi kinatakiwa kufanyika kwa umoja ili maisha ya Watanzania yabadilike na kufanyiwa mabadiliko ya kweli katika maisha ya watu.

Kuwa rais atakuwa amewasaliti vipi wananchi wake? Na je, huyo mtu wanayemsimamisha hana 'wananchi wake', au wa kule kwetu wakisalitiwa powa tu?!
Na nilidhani watu wa jimboni kwake ni watanzania vilevile kwa hiyo angeweza kuwasaidia vizuri!

Mwenye ujuzi zaidi anifahamishe tafadhali.
 
Kuwa rais atakuwa amewasaliti vipi wananchi wake? Na je, huyo mtu wanayemsimamisha hana 'wananchi wake', au wa kule kwetu wakisalitiwa powa tu?!
Na nilidhani watu wa jimboni kwake ni watanzania vilevile kwa hiyo angeweza kuwasaidia vizuri!

Mwenye ujuzi zaidi anifahamishe tafadhali.

hii ni tactical withdrawal, baada ya kupima na kuona wakati muuafaka bado labda bada ya hiyo 2010
 
Very smart position. For my opinion Dr. Slaa is good on what he does now, let him not leave his MP position. I respect his stand for knowing what he can do best and stick to it.
 
dk. Slaa: Sitagombea urais

na deogratius temba

katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo (chadema), dk. Wilibrod slaa, amesema hana mpango wa kugombea urais katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2010.

Dk. Slaa ambaye pia ni mbunge wa jimbo la karatu kwa [b]mihula miwili mfululizo[/b], alisema, jukumu alilonalo katika maisha yake ni kuwatumikia watu wa karatu ambao wamemwamini na kumpa nafasi hiyo na si kugombea urais.

Akizungumza katika kituo cha televisheni cha tbc1, katika kipindi cha jambo tanzania, dk. Slaa alisema yeye ni mtumishi wa watu wa karatu na hawezi kuwaacha kwenda kugombea urais.

“wananchi wangu waondoe wasiwasi, na wala wasijenge hisia kuwa nitasimama kuwania urais, wala sina wazo hilo, wala sijawahi kuota kuwa rais wa nchi hii, na sitakubali kuwasaliti wananchi wangu kwa kuacha kuwatumikia kama mbunge,” alisema.

Akizungumzia kuhusu chadema kusimamisha mgombe urais katika uchaguzi mkuu ujao, dk. Slaa alisema lazima wamsimamishe mtu kwani chama hicho kinaaminiwa na kupendwa na wananchi.

“ni lazima chadema tutamsimamisha mtu katika nafasi ya urais na kuendelea kupigania haki ya watanzania mpaka mwisho,” aliongeza dk. Slaa.

Akizungumzia suala la kuungana kwa vyama vya upinzani katika uchaguzi mkuu ujao, dk. Slaa alisema chadema kitaungana na chama chochote chenye nia ya dhati ya kutaka kulikomboa taifa, na kilichojijengea sera yakinifu na imara zinazokubalika na wananchi.

“kuungana tutaungana, ila tutaungana na watu ambao ni ‘serious’ (makini), wenye mipango, tutaelekezana tukiwa mezani kama ni nini tunataka kufanya, na kila mmoja aseme ana nini, lakini haya yatafanyika wakati muafaka ukifika,” alisema.

Aliongeza kuwa, lengo la vyama vya upinzani, hasa chadema, si kuitoa ccm madarakani tu, ni kuungana, maana kuna kitu cha msingi kinatakiwa kufanyika kwa umoja ili maisha ya watanzania yabadilike na kufanyiwa mabadiliko ya kweli katika maisha ya watu.

mihula mitatu mfululizo
 
Very smart position. For my opinion Dr. Slaa is good on what he does now, let him not leave his MP position. I respect his stand for knowing what he can do best and stick to it.


I second that!

Hii inaweka uhakika zaidi kuimarika kwa chama. Hii ni sawa na kuwa na Queen (chess) wawili kwenye mchezo wa chess, badala ya mmoja.
 
Mimi nafikiri Dr. slaa amesahau kuwa hata akiwa rais bado atawatumikia watu wake wa karatu kwa sababu nao wapo ndani ya TZ!!.
 
Mimi nafikiri Dr. slaa amesahau kuwa hata akiwa rais bado atawatumikia watu wake wa karatu kwa sababu nao wapo ndani ya TZ!!.

Ameshapima na kuona kuwa ni vigumu yeye kushinda urais sasa hivi. Akigombea akakosa, itakuwa amekosa nafasi ya 'kuwatumikia' watuw a karatu hata kwa nafasi hiyo ambayo aligombea
 
Safi sana Dr.Slaa hata Mrema naye angekuwaga na mawazo kama haya basi upinzani ungekuwa una nguvu sana bungeni tukiunganisha nguvu za Slaa+Mbatia+Cheyo n.k
 
Dr Slaa ni practical na realist. Mtu wa vitendo na mambo ya ukweli. Kuna watu wanagombea urais ili tuu nao wawepo wa boost CV zao kwamba ni 'presidential hopeful' hata kama wanaujua ukweli kuwa they don't stand a chance.

Hata Freeman aliposimama, hili alilijua bali alisimama tuu kuuza sura na kumthibitishia Baba Mkwe (Mtei) kuwa yuko serious kufuata nyayo zake as politician.

Niliwahi kusema mahali, Chadema bado hawana presidential material. So do CUF hata NCCR. The one and only ambaye vyama vyote vya upinzani vikimuunga mkono ni John Cheyo anaweza kumpa wakati mgumu JK japo hawezi kumshinda ila labda zikitembezwa kampeni chafu za udini, ukanda na ukabila, Kikwete Chali hiyo 2010. Tatizo wapinzani bado hawajakomaa kushika safu ya uongozi wa nchi.

Cha muhimu, ni wapinzani wamwachie boya Lipumba ang'ang'ane na fupa, wakati Cheyo, Mbowe, Mbatia, Mrema, na damu changa kina Myika, Lisu na wengine wakishika majimbo na kuitumia 2010-2015 ni muda wa kujipanga wachukue nchi 2015.
 
The one and only ambaye vyama vyote vya upinzani vikimuunga mkono ni John Cheyo anaweza kumpa wakati mgumu JK japo hawezi kumshinda...

Mkuu Pasco, ni nini kinakufanya uamini kwua Cheyo ni presidential material ambaye anaweza kumpa shida Kikwete?
 
Sasa aukimbie vipi while its beyond his reach..!! Hizi headlines nyingine zakipuuz tuu..
 
Slaa hawezi kuikosa posho na marupurupu yanayopatikana kwenye ubunge ,jamani si aseme kweli tu ,kuwa penye ubunge ndio penye kula isyokuwa na shida ,kusema kuwa ana watu wake wa karatu hapo anakipa mtihani Chama chake na kuzidi kuonekana ni cha kikabila au kimajimbo ,ni bora angelisema kama atapendekezwa atafikiria au kwa kifupi aseme bado hajawa tayari au yumo katika matayarisho ambayo anaona hayajatimia katika kuifuatilia ngazi ya Uraisi ,kujikomba kwa watu wa Karatu ni kujitenga na WaTanzania wengine ,kama mbunge awe tayari vilevile kuongoza WaTanzania kama akipendekezwa kuwa Raisi awache woga wa kukosa posho.
 
Slaa hawezi kuikosa posho na marupurupu yanayopatikana kwenye ubunge ,jamani si aseme kweli tu ,kuwa penye ubunge ndio penye kula isyokuwa na shida ,kusema kuwa ana watu wake wa karatu hapo anakipa mtihani Chama chake na kuzidi kuonekana ni cha kikabila au kimajimbo ,ni bora angelisema kama atapendekezwa atafikiria au kwa kifupi aseme bado hajawa tayari au yumo katika matayarisho ambayo anaona hayajatimia katika kuifuatilia ngazi ya Uraisi ,kujikomba kwa watu wa Karatu ni kujitenga na WaTanzania wengine ,kama mbunge awe tayari vilevile kuongoza WaTanzania kama akipendekezwa kuwa Raisi awache woga wa kukosa posho.

Akili zako kama Maalim na Jussa mwenye kusema kwamba Dr Slaa na CHADEMA ni mafisadi!. Kwani Urais na Ubunge upi una posho kubwa?

CHADEMA inakuaje ya kikabila kwa Slaa kuwapenda wananchi wake wa Karatu?

Kwani akiwa Mbunge anatumikia watu wa Karatu pekee yake? Kama ingekuwa ni Karatu si angetoa orodha ya mafisadi wa Karatu!

Hivi ulisikiliza mahojiano yake yote na TBC au unarukia tu kutokana na hiyo mistari michache iliyoandikwa kwenye habari

Asha
 
Akili zako kama Maalim na Jussa mwenye kusema kwamba Dr Slaa na CHADEMA ni mafisadi!. Kwani Urais na Ubunge upi una posho kubwa?

CHADEMA inakuaje ya kikabila kwa Slaa kuwapenda wananchi wake wa Karatu?

Kwani akiwa Mbunge anatumikia watu wa Karatu pekee yake? Kama ingekuwa ni Karatu si angetoa orodha ya mafisadi wa Karatu!

Hivi ulisikiliza mahojiano yake yote na TBC au unarukia tu kutokana na hiyo mistari michache iliyoandikwa kwenye habari

Asha

Tatizo ni mapenzi yako na CHADEMA, unalipuka kweli kweli!

Posho ya bungeni haifuatiliwi kama ukiwa rais. Wabunge wanapenda posho na kujineemesha familia zao kupitia migongo ya wananchi "eti wanawapenda na kuwatumikia wananchi wao" - nawe unakubali.
Au na wewe una 'wananchi wako' huko kwenye kitongoji gani sijui?
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom