Dk Slaa: Mvumilieni Rais Magufuli. Natafakari kurudi nchini siku yoyote

Dr Slaa Ajitathimni Kurud Nchini.......Adai Upinzani Usipojipanga Unaweza Kufutika 2020 source MPEKUZI HURU
 
aende zake huko ,,,,hajakomaa kisiasa pamoja na kuwa na phd anakosa political torelance.....yani kukosa nafasi ya kugombea urais basi upinzani anaona haufai,!!Ni mnafiki na mfano wa utitiri wa wasomi wachumia tumbo tulionao Tanzania!!!
 
Dr ukweli ni mchungu, ila we real need u back hata uwe msemaji tu, hata JPM akikosea mripue tu.

Huko ulikotokaga Dr mwenzio kawapiga nusu kaputi hakuna hamasa kabisa
 
Hayo ni maoni ya Dr.Slaa kama yalivyoripotiwa katika gazeti la Mtanzania.

Pia kwa mujibu wa gazeti hilo,Dr.slaa sasa anafikiria kurejea nyumbani. Akizungumza na Mtanzania akiwa nchini Canada jana, Dk. Slaa alisema amemaliza masomo yake na baada ya kufanya tafakari atarejea nchini wakati wowote ''Ni kweli nimemaliza masomo yangu. Bado napima mazingira yaliyonifanya niondoke na familia yangu. Baada ya hapo tutaangalia uwezekano wa kurejea.

Alisema pamoja na kuachana na siasa za vyama atakuwa tayari kupiga kelele pale anapoona masilahi ya taifa yanaumia ''Hadi sasa sijapiga kelele kwa kuwa sijaona masilahi ya taifa yakiangamizwa , hatua mbalimbali zinazochukuliwa ni kweli zinawaumiza wasiohusika.

Ndio maana nilitumia katika makala mojawapo mtego wa panya huwakamata wanaohusika na wasiohusika. Hivyo makosa madogo mimi hayanisumbui kwa kuwa hakuna binadamu kamilifu.'' Alisema

Rais Magufuli
Akizungumzia utendaji wa Rais M agufuli alisema watu waelewe hakuna nchi hata moja ambapo kiongozi atakubalika kwa watu wote kwa asilimia 100.

Alisema wapo watu ambao masilahi yao yataguswa kwa namna moja au nyingine hivyo lazima watapiga kelele.

Kutokana na hilo amaesma Magufuli katika kundi ambalo halihitaji fedha ameyatekeleza yote kwa asilimia 99.9, ikiwa ninpamoja na uwajibikaji serikalini, kuchukua hatua dhidi ya rushwa, wizi wa mali za umma, uwindaji haramu na kudhibiti dawa za kulevya.

''Hatua zimechukuliwa zinapaswa kuwa endelevu . Kwa bahati mbaya mchwa wengine waliopenya mpaka ndani ya Ikulu na serikali na huwezi kufagia serikali nzima kwa siku moja.

Kwa jinsi ambavyo Rais hayumbiwala hayumbishwi , nina hakika atafika malengo ya kurudisha taifa kwenye misingi ya tunu za taifa ya uwazi, ukweli,uadilifu kuheshimiana na na kuthaminiana na hasa kujali utu''

Hii ndio ambayo JPM anaiita kipindi cha mpito. Tutafika tu, tunatakiwa kuwa wavumilivu na wenye uzalendo wa kweli, ana nia njema ya kufikisha taifa mahali pazuri.

Hii inahitaji kuweka pembeni masilahi yetu binafsi kama mtu mmoja mmoja, viongozi wa serikali hata wa kisiasa''

Kuhusu Upinzani

Kuhusu mwenendo huo endapo utasaidia upinzani kuingia Ikulu 2020, Dk. Slaa alisema wakija na ajenda mbadala na makini yenye kuwalenga wananchi moja kwa moja itawasaidia.

Dk. Slaa ambaye pia alipata kugombea urais kupitia Chadema mwaka 2010, alisema endapo wataendelea kurukia kauli za Rais, basi upinzani utafutika kabla ya 2020.

“Kama nilivyorejea mara kadhaa, upinzani makini utaingia Ikulu kwa ajenda mbadala. Ajenda makini yenye kuwalenga wananchi moja kwa moja katika kuwatoa kwenye kero zao mbalimbali.

“Hadi sasa ninachoona ni ‘kurukia’ kauli za JPM, lakini kauli si ajenda na hatupeani maksi kwa kuzungumzia usahihi wa lugha. Wako wanaotazama usahihi wa lugha na mahali pa kutazama usahihi huo. Kimsingi hayo ni masuala ya darasani au kwenye uandishi wa vitabu.

“Aidha kumtuhumu JPM kukiuka Katiba na sheria nayo haina tija. Wote wanaomtuhumu wanajua kuwa wakiambiwa waonyeshe kifungu mahususi alichokiuka yeye mwenyewe katika utendaji wake hawana majibu ya kuridhisha.

“Hivyo mimi sijaona mwenendo wa JPM unaosaidia kuingiza upinzani Ikulu. Isitoshe kama hawatakuja na ajenda makini na mkakati ulioandaliwa unaowatoa wananchi hapa walipo kwenda kwenye raha, upinzani unaweza kufutika kabla ya 2020,”alisema Dk. Slaa.


Chanzo:Mtanzania

Akirudi ahamie hiko chama.
Mzee wewe ulikimbia nchini,ukaenda kula raha kwa wazungu maneno-maneno kuhusu nchi yetu? We baki na raha zako huko canada na sisi tubaki nchini kwetu tutajuana wenyewe humu humu.Kaa kimya.
 
Endelea kuvumilia wewe; sisi tuache na yetu isitoshe shida zetu hazikuhusu kumbe una njia mbadala ya kukaa ulaya mwenzetu
 
Slaa1-300x173.jpg

Dr Slaa


Kuhusu Upinzani

Kuhusu mwenendo huo endapo utasaidia upinzani kuingia Ikulu 2020, Dk. Slaa alisema wakija na ajenda mbadala na makini yenye kuwalenga wananchi moja kwa moja itawasaidia.

Dk. Slaa ambaye pia alipata kugombea urais kupitia Chadema mwaka 2010, alisema endapo wataendelea kurukia kauli za Rais, basi upinzani utafutika kabla ya 2020.

“Kama nilivyorejea mara kadhaa, upinzani makini utaingia Ikulu kwa ajenda mbadala. Ajenda makini yenye kuwalenga wananchi moja kwa moja katika kuwatoa kwenye kero zao mbalimbali.

“Hadi sasa ninachoona ni ‘kurukia’ kauli za JPM, lakini kauli si ajenda na hatupeani maksi kwa kuzungumzia usahihi wa lugha. Wako wanaotazama usahihi wa lugha na mahali pa kutazama usahihi huo. Kimsingi hayo ni masuala ya darasani au kwenye uandishi wa vitabu.

“Aidha kumtuhumu JPM kukiuka Katiba na sheria nayo haina tija. Wote wanaomtuhumu wanajua kuwa wakiambiwa waonyeshe kifungu mahususi alichokiuka yeye mwenyewe katika utendaji wake hawana majibu ya kuridhisha.

“Hivyo mimi sijaona mwenendo wa JPM unaosaidia kuingiza upinzani Ikulu. Isitoshe kama hawatakuja na ajenda makini na mkakati ulioandaliwa unaowatoa wananchi hapa walipo kwenda kwenye raha, upinzani unaweza kufutika kabla ya 2020,”alisema Dk. Slaa.

Chanzo: Mtanzania
Ana mawazo mgando sana Dr Slaa. Hii ni dunia mpya, wewe unadhani Sera za kwenye makaratasi hata ziwe nzuri namna gani bila kuondoa njaa na matatizo kwa wananchi watakukubali?
Ccm haitakiwi sasa hivi kwa vile kuna njaa na mateso basi, na Magu anapiga fix tuu
 
Hizo hoteli nyingi zilijengwa kwaa kifisadi, na zilikuwa zikitegemea pesa za wananchi walalahoi, seminars za uongo na ambazo zimepangwa kifisadi fisadi, kila siku utaona Dar peke yake semira 40 hadi 60 , kitu ambacho kingefanyika katika kumbi za mikutano za wizarani. Seminar ya siku moja inafanywa kwa siku 5.

Seminar ya wafanyikazi wa mbeya inafanyika Dar ama Arusha.

Hii ndio ilikuwa inawalipa wenye hoteli, bei za vyumba vilipanda kwa sababu hiyo, chumba Dar 150000 kwa siku tena hotel ya kawaida tuu. Arusha 80, 000 hali myu wa kawaida analipa 30,000 KWA CHUMBA . Hao watu walikuwa wakupuwaji wa pesa za umma.

Umeongea kwa mantiki na kwa ustaarabu sana. POINT noted!
 
Kilikuwa ni kipindi kigumu sana. ...wakati katibu wetu Dr. Slaa anatuacha. ..hatukujua kama tungefika hapa. ..ukiangalia mzee Lipumba naye alikuwa amejiachia. ...kwa sasa siasa zimebadilika sana. ..Daktari ni lazima ajue zama zimebadilika sana...
 
Hilo ni buludoza, Slaa anajua aset na liability. Mkimtaka arudi ondoeni liabiliti muone mziki wake.
Akiingia Ccm, toba!
 
rudi huku tumvumilie wote, na hayo mengine uyasemee huku huku.
hatutaki umbea kutoka canada.
unataka kutuaminisha kuwa ungekuwa bado ni katibu mkuu chadema huku tz ungekuwa unamsifia Magufuli kwa kukataza mikutano ya hadhara na watu kushitakiwa ovyo kwa "uchochezi" hewa?
huo ni upinzani uchwara.
unajikombakomba ili iweje? by the way uliomba ruhusa kwa mchumba kuongea haya?
utatafuta nchi ya tatu ya kuishi ohoooo!!
 
Hilo ni buludoza, Slaa anajua aset na liability. Mkimtaka arudi ondoeni liabiliti muone mziki wake.
Akiingia Ccm, toba!
Hiyo ni historia, siasa zile za Slaa sasa hivi hakuna wa kumsikiliza na haziwezj kuleta badiliko lolote
 
Mzee wewe ulikimbia nchini,ukaenda kula raha kwa wazungu maneno-maneno kuhusu nchi yetu? We baki na raha zako huko canada na sisi tubaki nchini kwetu tutajuana wenyewe humu humu.Kaa kimya.
..wala hakuna cha raha huko aliko wala nini...aliyekudanganya anakula raha nani?.....huko ng'ambo aliko wala hapati mapato kama alivyokuwa anapata TZ chini ya chedema....huko waliko na mchumba wake sana sana wanafanya kazi nje ya taaluma zao....kama kuna ufadhili na utakua unaishia sasa...na kama ni kazi wanafanya basi ujue ni za kitwana tu....mfano kuosha vyooo ama vyombo kwenye mahoteli ya wazungu....usidhani wanapokaa nje ya nchi wana raha sana....usisahau pia kuwa hata hali ya hewa sio friendly huko waliko.....sasa inaonekana ufadhili wao huko umeisha...na sasa wanatafta kiki za kurudia bongo...ni rahisi sana kuwasoma watu wanafiki na waongo....kama huyu babu...
 
Akirudi na akitaka kurudisha heshima yake aache kumtumia yule "mchumba" kama mshauri wake.
Hakika nawaambia, aliyemharibia Slaa maisha yake ya kisiasa ni "mchumba"
Mkuu kubali Dr Slaa amekuchakaza. Gusia hoja zake na siyo personality.
 
Back
Top Bottom