sir.JAPHET
JF-Expert Member
- May 18, 2012
- 699
- 133
Jumapili, Agosti 26, 2012 06:46
Na Abdalah Amir, Igunga
Dk. Wilbrod Slaa
*Asema uchaguzi ukirudiwa haitashinda
*Kasulumbai amtupia kombora Magufuli
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willbrod Slaa amesema uchaguzi mdogo wa Igunga mkoani Tabora ukifanyika sasa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kisitarajie kushinda.
Dk. Slaa alitoa kauli hiyo jana mjini Igunga alipohutubia mamia ya wananchi kwenye uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine.
"Nawaambia wana Igunga, nimekuja kuwashukuru kwa kazi nzuri mlioifanya wakati wa uchaguzi mdogo wa mwaka jana, mlituonyesha imani…nawaambia CCM hata uchaguzi huu ukirudiwa sasa hivi hawashindi," alisema.
Alisema kwa sababu hiyo, Chadema kiko tayari kuingia kwenye uchaguzi wa marudio wakati wowote kwa sababu kina uhakika wa kushinda.
"Hatuna wasiwasi na hili, nawaambia Chadema wako tayari kwa uchaguzi, uamuzi wa Mahakama Kuu Kanda ya Tabora kutengeua matokeo haya tumeupokea kwa mikono miwili kabisa,"alisema Dk. Slaa.
Dk Slaa, ambaye aliogozana na Mbunge wa Maswa Mashariki, Silvester Kasulumbai, alisema CCM wanapaswa kujilaumu wenyewe kwa kuwatumia mawaziri kutoa ahadi kwa wananchi wakati wakitambua kufanya hivyo ni kosa.
Alisema makosa hayo yanazidi kuwagharimu wananchi wa Igunga kutokana na gharama kubwa zinazotumika kurudia uchaguzi.
Alisema katika uchaguzi mdogo uliompatia ubunge mgombea wa CCM, Dk. Peter Kafumu zaidi ya Sh bilioni tatu zilitumika kiasi ambacho kingefanya kazi za kuinua maendeleo ya wananchi.
"Uchaguzi ukiitishwa leo hatuna wasiwasi, tuna uhakika wa kushinda mapema saa 4 asubuhi. CCM hawana ubavu wa kupambana na Chadema, wanachofanya ni kushinda kwa ghiliba na vitisho,
"…mathalani, kauli ya Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama (eti Chadema kilikodisha makomandoo kutoka Libya na Pakstan) haiwezi kuvumilika, anapaswa kuwaomba radhi wana Igunga kwa uongo huo" alisema Dk. Slaa.
Naye Kasulumbai alizungumzia kauli ya Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli kujenga daraja la Mbutu endapo mgombea wao atachaguliwa haivumiliki.
Alisema Magufuli kama waziri, anapaswa kuwaomba radhi wananchi wa Igunga kwa sababu ujenzi wa miundombinu ni kazi ya serikali iliyoko madarakani.
"Daraja hili lilicheleweshwa kujengwa na Serikali iliyo madarakani… kwa nini waje kuwaomba muwachague eti ndiyo wajenge…namtaka Magufuli awaombe msamaha.
"…miaka yote walilifumbia macho, leo hii baada ya kuona Chadema tumejizatiti na kuwaeleza ukweli wananchi…eti ndiyo wanazinduka ujenzi wa daraja, sisi wapinzani kazi yetu ni kupiga kelele".
Toa Maoni yako kwa habari hii
Na Abdalah Amir, Igunga
Dk. Wilbrod Slaa
*Asema uchaguzi ukirudiwa haitashinda
*Kasulumbai amtupia kombora Magufuli
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willbrod Slaa amesema uchaguzi mdogo wa Igunga mkoani Tabora ukifanyika sasa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kisitarajie kushinda.
Dk. Slaa alitoa kauli hiyo jana mjini Igunga alipohutubia mamia ya wananchi kwenye uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine.
"Nawaambia wana Igunga, nimekuja kuwashukuru kwa kazi nzuri mlioifanya wakati wa uchaguzi mdogo wa mwaka jana, mlituonyesha imani…nawaambia CCM hata uchaguzi huu ukirudiwa sasa hivi hawashindi," alisema.
Alisema kwa sababu hiyo, Chadema kiko tayari kuingia kwenye uchaguzi wa marudio wakati wowote kwa sababu kina uhakika wa kushinda.
"Hatuna wasiwasi na hili, nawaambia Chadema wako tayari kwa uchaguzi, uamuzi wa Mahakama Kuu Kanda ya Tabora kutengeua matokeo haya tumeupokea kwa mikono miwili kabisa,"alisema Dk. Slaa.
Dk Slaa, ambaye aliogozana na Mbunge wa Maswa Mashariki, Silvester Kasulumbai, alisema CCM wanapaswa kujilaumu wenyewe kwa kuwatumia mawaziri kutoa ahadi kwa wananchi wakati wakitambua kufanya hivyo ni kosa.
Alisema makosa hayo yanazidi kuwagharimu wananchi wa Igunga kutokana na gharama kubwa zinazotumika kurudia uchaguzi.
Alisema katika uchaguzi mdogo uliompatia ubunge mgombea wa CCM, Dk. Peter Kafumu zaidi ya Sh bilioni tatu zilitumika kiasi ambacho kingefanya kazi za kuinua maendeleo ya wananchi.
"Uchaguzi ukiitishwa leo hatuna wasiwasi, tuna uhakika wa kushinda mapema saa 4 asubuhi. CCM hawana ubavu wa kupambana na Chadema, wanachofanya ni kushinda kwa ghiliba na vitisho,
"…mathalani, kauli ya Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama (eti Chadema kilikodisha makomandoo kutoka Libya na Pakstan) haiwezi kuvumilika, anapaswa kuwaomba radhi wana Igunga kwa uongo huo" alisema Dk. Slaa.
Naye Kasulumbai alizungumzia kauli ya Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli kujenga daraja la Mbutu endapo mgombea wao atachaguliwa haivumiliki.
Alisema Magufuli kama waziri, anapaswa kuwaomba radhi wananchi wa Igunga kwa sababu ujenzi wa miundombinu ni kazi ya serikali iliyoko madarakani.
"Daraja hili lilicheleweshwa kujengwa na Serikali iliyo madarakani… kwa nini waje kuwaomba muwachague eti ndiyo wajenge…namtaka Magufuli awaombe msamaha.
"…miaka yote walilifumbia macho, leo hii baada ya kuona Chadema tumejizatiti na kuwaeleza ukweli wananchi…eti ndiyo wanazinduka ujenzi wa daraja, sisi wapinzani kazi yetu ni kupiga kelele".
Toa Maoni yako kwa habari hii