Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
KATIBU mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Willbroad Slaa amesema anazo nyaraka maalumu za CCM zinazowaagiza wakuu wa wilaya kuwaita wafanyabiashara ili wakichangie chama hicho fedha wakati huu wa uchaguzi.
Dk Slaa alisema kwamba, nyaraka hizo pia zinawaagiza Watendaji wa Vijiji wakichangishie chama hicho.
Dk Slaa ambaye ni mbunge wa Jimbo la Karatu mkoani Arusha aliibua suala hilo bungeni jana katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Alisema katika wakaraka huo wa CCM, wafanyabiashara wanatakiwa kuchangia kuanzia Sh20,000 na watendaji wa wijiji wachangiekuanzia Sh10,000.
Katika swali lake kwa Waziri Mkuu, Dk Slaa alisema; Mheshimiwa Waziri Mkuu, hivi sasa wakuu wa wilaya wanatumia ofisi, vyombo vya umma na mali nyingine za serikali kuwaita ofisini wafanyabiashara bila ya hiari yao ili waichangie CCM na kila mtendaji wa kijiji aichangie CCM?
Pinda alijibu; Kiufupi, kama hawajalazimishwa wala kusurutishwa kuchangia fedha hizo hakuna tatizo, lakini kama watalazimishwa hilo ni tatizo.
Kufuatia majibu hayo, Dk Slaa alilazimika kusimama tena na kusema kuwa anazo nyaraka maalumu kutoka CCM zinazowaelekeza wakuu wa wilaya kuzunguka katika kata pamoja na vijiji vyote kutekeleza maagizo hayo.
Ninazo nyaraka maalumu za CCM zinazowaelekeza wakuu wa wilaya kuzunguka katika kata pamoja na vijiji vyote kuichangishia fedha pamoja na kuwataka watendaji wa Vijiji kufanya hivyo pia, alisema
Alisema nyaraka hizo zinawataka wakuu wa wilaya kuwataka wafanyabiashara kukichangia chama hicho kuanzia Sh20,000 na Mtendaji wa Kijiji achangishe kuanzia Sh10,000.
Dk Slaa ambaye ameonekana kuwa mwiba kwa CCM, aliitaja Wilaya ya Nzega kuwa ni moja ya wilaya iliyokwisha anza kutekeleza maagizo hayo.
Dk Slaa alilalamika kuwa kitendo cha wakuu wa wilaya kutumia vyombo vya serikali na ofisi zao ni aina nyingine ya ufisadi unaotumia fedha za umma.
Wakuu wa wilaya kutumia vyombo vya serikali pamoja na nyaraka zake ni aina nyingine ya ufisadi unaotumia fedha za umma, alisema Dk Slaa
Dk Slaa alisema kitendo cha watumishi wa umma kutumia ofisi na vyombo vya serikali kwa ajili ya chama ni kinyume na maadili ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Maadili ya Nec hayaruhusu mtumishi wa umma yoyote kutumia nyaraka za serikali katika masuala yanayohusu chama, alisema Dk Slaa. Chanzo: Mwananchi
Dk Slaa alisema kwamba, nyaraka hizo pia zinawaagiza Watendaji wa Vijiji wakichangishie chama hicho.
Dk Slaa ambaye ni mbunge wa Jimbo la Karatu mkoani Arusha aliibua suala hilo bungeni jana katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Alisema katika wakaraka huo wa CCM, wafanyabiashara wanatakiwa kuchangia kuanzia Sh20,000 na watendaji wa wijiji wachangiekuanzia Sh10,000.
Katika swali lake kwa Waziri Mkuu, Dk Slaa alisema; Mheshimiwa Waziri Mkuu, hivi sasa wakuu wa wilaya wanatumia ofisi, vyombo vya umma na mali nyingine za serikali kuwaita ofisini wafanyabiashara bila ya hiari yao ili waichangie CCM na kila mtendaji wa kijiji aichangie CCM?
Pinda alijibu; Kiufupi, kama hawajalazimishwa wala kusurutishwa kuchangia fedha hizo hakuna tatizo, lakini kama watalazimishwa hilo ni tatizo.
Kufuatia majibu hayo, Dk Slaa alilazimika kusimama tena na kusema kuwa anazo nyaraka maalumu kutoka CCM zinazowaelekeza wakuu wa wilaya kuzunguka katika kata pamoja na vijiji vyote kutekeleza maagizo hayo.
Ninazo nyaraka maalumu za CCM zinazowaelekeza wakuu wa wilaya kuzunguka katika kata pamoja na vijiji vyote kuichangishia fedha pamoja na kuwataka watendaji wa Vijiji kufanya hivyo pia, alisema
Alisema nyaraka hizo zinawataka wakuu wa wilaya kuwataka wafanyabiashara kukichangia chama hicho kuanzia Sh20,000 na Mtendaji wa Kijiji achangishe kuanzia Sh10,000.
Dk Slaa ambaye ameonekana kuwa mwiba kwa CCM, aliitaja Wilaya ya Nzega kuwa ni moja ya wilaya iliyokwisha anza kutekeleza maagizo hayo.
Dk Slaa alilalamika kuwa kitendo cha wakuu wa wilaya kutumia vyombo vya serikali na ofisi zao ni aina nyingine ya ufisadi unaotumia fedha za umma.
Wakuu wa wilaya kutumia vyombo vya serikali pamoja na nyaraka zake ni aina nyingine ya ufisadi unaotumia fedha za umma, alisema Dk Slaa
Dk Slaa alisema kitendo cha watumishi wa umma kutumia ofisi na vyombo vya serikali kwa ajili ya chama ni kinyume na maadili ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Maadili ya Nec hayaruhusu mtumishi wa umma yoyote kutumia nyaraka za serikali katika masuala yanayohusu chama, alisema Dk Slaa. Chanzo: Mwananchi