ouagadougou
Member
- Sep 12, 2012
- 5
- 1
Kutokana na yaliyojiri juzi mji mdogo wa Tunduma, polisi walimshikilia Diwani Frank Mwakajoka wa Chadema tangu saa 3 asubuhi. Ajabu ni kwamba yaliyotokea juzi ni mgogoro wa kuchinja kati ya Wakristo na waislamu. Diwani aliyekuwa na kikao shule ya sekondari mpakani aliambiwa kuhusu yaliyokuwa yakiendelea, ifahamike kuwa shule ya sekondari ya mpakani iko nje kidogo ya mji. Diwani huyo wa CHADEMA aliamua kuacha kikao hicho kinachotokana na vurugu za wanafunzi zilizofanywa hivi karibuni akaelekea Polisi na akamwambia RPC uitishe mkutano wa wananchi ili wazungumze nao, RPC aligoma kwa sababu anazozijua. vilevile ifahamike siku moja kabla ya juzi Mkuu wa mkoa Abbas Kandoro alikaa na viongozi wa dini katika Hotel ya Ukinga Hill ili kupata hatma ya tatizo.
baada ya kukosekana kwa muafaka mkuu huyo wa mkoa aliamuru "KILA MTU ALE VYAKE". ushahidi wa CD upo.
Baada ya mkutano huo ilipofika asubuhi ya siku ya jumatano wakristo waliwahi asubuhi kuchinja na wakakuta kuna askari polisi na kuwa wameagizwa wawazuie kuchinja. hali hiyo ilipelekea wakristo kuzuia nyama ya waislamu kuuzwa na hapo vurugu zikaanza. ikumbukwe waislamu katika mji wa Tunduma ni asilimia 1%
Ajabu ni kwamba diwani alishikiliwa Polisi mtu asiyehusika na lolote katika mgogoro
Vile vile ifahamike kuwa askari polisi jana walipora wananchi fedha nyingi na simu za mkononi leo nimekutana na mama ambaye aliingiliwa nyumbani kwake na m aaskari hao na akaporwa shilingi milioni moja ambazo ni ada ya mtoto wake ambaye shule inafunguliwa siku chache zijazo baada ya likizo ya pasaka. alipowang'ang'ania walimrudishia laki saba na wakaondoka na laki 3 pia ushahidi upo. (kumbuka alifuatwa nyumbani usiku, mama asiyejua lolote na leo amemfuata Mbunge na akaonyesha karatasi aliyotoka nayo polisi na kusimulia kisa chote.
MY TAKE:
Kwa kuwa mji wa Tunduma na Jimbo la Momba yanaongozwa na CHADEMA. CCM kupitia makada wake hao inatakakuutumia mgogoro huu ambao ni wa kitaifa ili kuwapumbaza wananchi na kuionea CHADEMA.
Mwenyekiti wa CCM bwana JUMA MWANDUSU yuko tayari kutumia mbinu zozote chafu kama afanyavyo mwigulu Nchemba ili kuwapa moyo mabosi wake kuwa anafanya kazi kubwa ya kuirudisha CCM kwenye chati. Ukorofi huu hauvumiliki.
baada ya kukosekana kwa muafaka mkuu huyo wa mkoa aliamuru "KILA MTU ALE VYAKE". ushahidi wa CD upo.
Baada ya mkutano huo ilipofika asubuhi ya siku ya jumatano wakristo waliwahi asubuhi kuchinja na wakakuta kuna askari polisi na kuwa wameagizwa wawazuie kuchinja. hali hiyo ilipelekea wakristo kuzuia nyama ya waislamu kuuzwa na hapo vurugu zikaanza. ikumbukwe waislamu katika mji wa Tunduma ni asilimia 1%
Ajabu ni kwamba diwani alishikiliwa Polisi mtu asiyehusika na lolote katika mgogoro
Vile vile ifahamike kuwa askari polisi jana walipora wananchi fedha nyingi na simu za mkononi leo nimekutana na mama ambaye aliingiliwa nyumbani kwake na m aaskari hao na akaporwa shilingi milioni moja ambazo ni ada ya mtoto wake ambaye shule inafunguliwa siku chache zijazo baada ya likizo ya pasaka. alipowang'ang'ania walimrudishia laki saba na wakaondoka na laki 3 pia ushahidi upo. (kumbuka alifuatwa nyumbani usiku, mama asiyejua lolote na leo amemfuata Mbunge na akaonyesha karatasi aliyotoka nayo polisi na kusimulia kisa chote.
MY TAKE:
Kwa kuwa mji wa Tunduma na Jimbo la Momba yanaongozwa na CHADEMA. CCM kupitia makada wake hao inatakakuutumia mgogoro huu ambao ni wa kitaifa ili kuwapumbaza wananchi na kuionea CHADEMA.
Mwenyekiti wa CCM bwana JUMA MWANDUSU yuko tayari kutumia mbinu zozote chafu kama afanyavyo mwigulu Nchemba ili kuwapa moyo mabosi wake kuwa anafanya kazi kubwa ya kuirudisha CCM kwenye chati. Ukorofi huu hauvumiliki.