Diamond Platinumz vs Ali Kiba, nani mkali?

kila kitu khusu diamond ni best..kuanzia uvaaji wake..upangiriaji wa shows zake..tungo zake n.k ni tofaut sana na alivyokuwa ali k(maana siku hiz ni kama hayupo ametoa wimbo wa my everything bila shaka ni wachache tu wanaoufahamu
)

sasa napata shaka kama wewe sio wema sepetu au jokate,bas wewe n diamond mwenyewe..
 
Hata kama sio shabiki wa diamond ila kuna kitu lazima uwe kinakuvutia kutoka kwake.Unaweza kujitahidi kumchukia labda kutokana na skendo zake za nje ya muziki wake ila ukirudi kwenye muziki wake nadhani anastahili kuwa pale alipo.
Kuanzia muonekane wake mpaka anavyoweza kuji-brand kimataifa na anavyojua kucheza na akili za mashabiki.

Wasanii wengi wa bongo flava wana tabia ya kurithika kwa mafanikio yao ila Diamond toka atoke na Kamwambie mwaka 2009 mpaka 2013 amezidi kwenda juu bila kuonyesha kusuasua wala kutetereka.
Angalia video ya number 1.Wimbo unaweza sema ni wa kawaida kabisa ukilinganisha na mbagala, kamwambie au nitarejea ila akili ya kwenda kufanya video cape town,south africa kumeifanya nyimbo iwe number 1 kama jina lake lilivyo.

Ushawahi kujiuliza Ali kiba yupo wapi pamoja na kuwa kila mtu anajua ni mkali kuliko diamond?Ali kiba toka atoe my everything mwisho wa mwaka jana amepotea hata video ajatoa.Tukaja kumuona kwenye kidela na Abdu kiba bila kurefusha maneno Ali anashindwa kuufanya mziki wake kama mashabiki wake wanavyotarajia labda pengine angekuwa anafukuzana na diamond ila matokeo yake vijana wake kama Rich mavoko na Dimpoz ndio wapo nyuma ya Diamond huku Ali akibaki msanii mkali ambae ameshindwa kuendelea kutuonyesha ukali wake sijui anawaza nini!

Ushawahi kujiuliza kama ule wimbo wa airtel hands across the world waliopiga wakina r.kelly,fall ipupa,2 face kama nafac ile angeipata diamond leo angekuwa wapi?
Diamond leo anatuletea remix ya number 1 f.t Davido kila mtu anaisubiri kwa hamu ila Ali alishindwa hata kutuletea remix ya Dushelele f.t Fally ipupa pamoja kukaa nae wiki nzima wakifanya wimbo pamoja.
Diamond ni mjanja anaejua biashara ya mziki ilivyo labda pengine ni management yake inayomsimamia.Diamond kaweza kuubadilia mziki wetu kwa kiasi chake leo ndio msanii anaelipwa pesa nyingi kwa show.

Nampenda ali kiba,naipenda sauti yake,anajua mziki kuliko Diamond ila Ali ameshindwa kubadilika na kukubali soko la mziki linataka nini.

Amka Ali huyu Diamond hakuwezi ila usipokuwa makini utajikuta nyuma ya rich,barnaba,dimpoz na ben pol maana mziki sio kuimba peke yake mziki ni biashara pia
 
Mtu hata awe maarufu vipi, kwangu kama haja imba hata wimbo mmoja wa kuzungumzia uozo wa serikali na chama lake kwa kutuharibia nchi na kunyonya wananchi, huyo kwangu ni bure tu. Akili haiwezi kuishia kuimba mapenzi tu lazima kuta kuwa na tatizo la elimu kwa mtu huyo.

Nawapa salute akina Prof. J, Mr. II, Kala Jeremiah, E. Sanga na wapenda nchi kama hao kuliko wapenda magodolo, uroda na misifa ya kijinga.
 
Mtu hata awe maarufu vipi, kwangu kama haja imba hata wimbo mmoja wa kuzungumzia uozo wa serikali na chama lake kwa kutuharibia nchi na kunyonya wananchi, huyo kwangu ni bure tu. Akili haiwezi kuishia kuimba mapenzi tu lazima kuta kuwa na tatizo la elimu kwa mtu huyo.

Nawapa salute akina Prof. J, Mr. II, Kala Jeremiah, E. Sanga na wapenda nchi kama hao kuliko wapenda magodolo, uroda na misifa ya kijinga.

mziki ni kama biashara kila mtu anafanya kutokana na uwezo na mtaji wake sasa kama ww unataka wote waimbe kitu kimoja utasubiri milele
 
Back
Top Bottom