mkweli wa mambo
JF-Expert Member
- Oct 28, 2013
- 329
- 178
yeeees..ni yuleyule tena mkali wa wakali, sukari ya warembo hasa masuperstar wetu wa kike,yule anayejiita raisi wa wasafi, yuleyule ambae ana make headline kila koona ya Tz na Africa kwa ujumla..Platinuuuuuum...ebhana jamaa anajua,sio kwamba tu namsifia la hasha..nimepata kusikiliza nyimbo yake mpya hii iliyovuja sijui inaitwa nini vileee sijui kitorondo..mwanzoni nilipoona title ya kitorondo nikadharau ndo madudu gani ayo tena jamaa anaimba,ila daah namsifu mchizi anajua kusoma nyakati,anajua ni aina gani ya muziki autoe utakaoendana na nyakati zilizopo, kama mtakumbuka kuna kipindi kwaito zilitamba sana,mchizi akatupia nyimbo zake za style iyo akakomba mashabiki kibaaao..saivi kwaito inaishia ivo mchizi kasoma nyakati tena akaibuka na mtindo huu sijui ni mnanda sijui mchiriku mi sielewi, ila all in all nyimbo taamu balaa, nyimbo inachezeka..tena kalenga haswaaaa kuleeee kwa watoto wa uswazi kule kwenye vigodoro ambavyo kila mtu anafahamu siku izi vigodoro ndo mpango mzima. Daaah,kwa style hii Diamond atakaa sana kwenye peak ya game hili..wasanii wengine mjifunze kutoka kwake,someni nyakati.