NGULI
JF-Expert Member
- Mar 31, 2008
- 4,803
- 637
Dhana nzima ya kubemenda mtoto
Kuna hili suala linaloitwa 'kubemenda' mtoto. Watu wanadai kuwa sperms huwa zinaleta madhara kwenye maziwa ya mama na kumdhoofisha mtoto kiafya na wengine wanasema ukimshika mtoto baada ya sex pia ina madhara. kiukweli suala la Kubemenda ni imani potofu (myth) na hakuna uhusiano wa sperms na maziwa ya mama katika kudhoofisha afya ya mtoto; iwe kwa kushirikiana tendo la ndoa au kumshika mtoto baada ya sex.
Je, nini maana ya kubemenda mtoto?
Kwanza hii imani potofu inaeleza kwamba kubemenda mtoto ni pale wanandoa wanapojihusisha na tendo la ndoa baada ya mtoto Kuzaliwa (pale mke anapokuwa tayari kiafya kwa tendo la ndoa baada ya kujifungua) kwa maana kwamba sperms huharibu maziwa ambayo mtoto ananyonya, si kweli hakuna uhusiano wowote kati ya maziwa ya mama na sperms katika kuathiri afya ya mtoto.
Pili kubemenda mtoto ni kitendo cha wanandoa kujihusisha na tendo la ndoa na mke kushika mimba miezi mwili tu au mitatu tu baada ya kujifungua na kupelekea kuzaa mtoto mwingine baada ya mwaka na matokeo yake mtoto aliyetangulia Kuzaliwa huwa dhaifu kiafya (huchelewa kutembea) na huitwa ni mtoto ambaye amebemendwa, kitu ambacho ni imani potofu kwani kuna wanandoa wengi tu wamezaa watoto waliopishana mwaka na wote wana afya njema kabisa.
Tatu kubemenda ni kitendo cha mwanandoa mmoja kutoka nje ya ndoa (sex) na akirudi ndani huendelea na tendo la ndoa na matokeo yake mtoto wa ndani ya ndoa huwa dhaifu, pia ni imani potofu hakuna kitu kama hicho. Jambo la msingi ni kufuata ushauri wa kitaalamu ambao ni wiki sita baada ya kujifungua. Je, kuna ukweli wowote kuhusiana na hii imani potofu Iwe wanandoa kujihusisha na tendo la ndoa baada ya mtoto Kuzaliwa au kuzaa mwingine baada ya mwaka au hata kutoka nje hakuna uhusiano na mtoto aliyezaliwa kama suala la usafi na lishe bora litazingatiwa kwa mtoto anayehusika.
Je, kulikoni mababu zetu wakaweka imani kama hiyo kwa wanandoa?
Kama zilivyo imani zingine potofu kama vile mwanamke mjamzito kutokula mayai mababu zetu walikuwa na somo ndani yake, inawezekana walitaka kuhakikisha wanandoa wanashiriki vizuri katika kulea mtoto kwa pamoja bila kupendekeza tabia za uchafu na kujirusha nje na ndani ya ndoa bila utaratibu. Pia labda mababu zetu walihofia kitendo cha mwanamke kutoa maziwa (chuluzika) wakati wa tendo la ndoa hasa anapofika kileleni (tangu akifungue hadi miezi 8 hivi) na wakawa wanahofia kinaweza kuathiri kiwango cha chakula cha mtoto hivyo ili kuzuia ni kutunga imani (potofu) kwamba mtoto ataathirika kwa mke na mume kushiriki tendo la ndoa.
Je, ili mtoto asionekane amebemendwa wanandoa wanahitaji kufanya kitu gani?
Ni vizuri kufahamu kwamba hakuna uhusiano wa sperms kuharibu maziwa ya mama wakati wa kumnyonyesha mtoto hivyo wanandoa kushiriki tendo la ndoa halina uhusiano wowote na mtoto kuwa na afya mbaya kiasi cha kuchelewa kutembea. Mtoto anahitaji watoto chakula bora chenye viini-lishe vyote vinavyohitajika ili kukua vizuri pia mama anahitaji kujiweka mazingira safi (kuwa msafi) wakati ananyonyesha, ahakikishe anasafisha chuchu zake na mikono yake au kuzingatia usafi kimwili kabla ya kumnyonyesha mtoto iwe baada ya sex au muda wowote.
Je, kulikoni mababu zetu wakaweka imani kama hiyo kwa wanandoa?
Kama zilivyo imani zingine potofu kama vile mwanamke mjamzito kutokula mayai mababu zetu walikuwa na somo ndani yake, inawezekana walitaka kuhakikisha wanandoa wanashiriki vizuri katika kulea mtoto kwa pamoja bila kupendekeza tabia za uchafu na kujirusha nje na ndani ya ndoa bila utaratibu. Pia labda mababu zetu walihofia kitendo cha mwanamke kutoa maziwa (chuluzika) wakati wa tendo la ndoa hasa anapofika kileleni (tangu akifungue hadi miezi 8 hivi) na wakawa wanahofia kinaweza kuathiri kiwango cha chakula cha mtoto hivyo ili kuzuia ni kutunga imani (potofu) kwamba mtoto ataathirika kwa mke na mume kushiriki tendo la ndoa.
Je, ili mtoto asionekane amebemendwa wanandoa wanahitaji kufanya kitu gani?
Ni vizuri kufahamu kwamba hakuna uhusiano wa sperms kuharibu maziwa ya mama wakati wa kumnyonyesha mtoto hivyo wanandoa kushiriki tendo la ndoa halina uhusiano wowote na mtoto kuwa na afya mbaya kiasi cha kuchelewa kutembea. Mtoto anahitaji watoto chakula bora chenye viini-lishe vyote vinavyohitajika ili kukua vizuri pia mama anahitaji kujiweka mazingira safi (kuwa msafi) wakati ananyonyesha, ahakikishe anasafisha chuchu zake na mikono yake au kuzingatia usafi kimwili kabla ya kumnyonyesha mtoto iwe baada ya sex au muda wowote. Huwezi kusikia takataka za neno kubemenda katika nchi zilizoendelea kama Canada, Sweden, Australia, Ujerumani nk why? Ni traditions (Myth).
Chanzo: sayi manyanda
FAHAMU MAMBO YA MSINGI KUHUSIANA NA MTOTO MCHANGA.1. Ni muda gani tangia kuzaliwa anaweza kutoka nje?Hakuna muda maalum ambao mtoto anaweza toka nje, anaweza hata kutoka siku ya pili tu baada ya kuzaliwa. Cha muhimu ni kwamba, uwezo wa mtoto kutunza joto ni mdogo (hasa watoto njiti), hivyo ukimtoa nje hakikisha umemvika nguo na kumfunika ili asipoteze joto kabisa.
2. Ni muda gani tangia kuzaliwa anaweza kuanza kula chakula kingine zaidi ya maziwa ya mama?
Mtoto anaweza kula chakula kingine mbali na maziwa ya mama baada ya miezi 6. Maziwa ya mama yana kila kitu mtoto anachohitaji katika miezi sita ya kwanza bila kuongeza chakula chochote. Baada ya miezi sita mtoto aendelee kunyonya mpaka miaka mi2 au zaidi huku akila vyakula mbalimbali vinavyoshauriwa kufuatana na umri wake.
3. Aogeshwe mara ngapi kwa siku?
Kuoga ni njia mojawapo ya kupoteza joto la mtoto. Ile siku ya kwanza kuzaliwa inashauriwa hasiogeshwe. Kisha waweza kuendelea kumuosha mtoto (epuka maji mengi) kadri inavyohitajika. Ni vyema kumfuta kwa kitambaa kilicholoweshwa maji ya vugu vugu unapombadili mtoto akijisaidia kuliko kumuogesha kila mara.
4. Nini kitamtokea mtoto kama nitaanza kufanya mapenzi na mamake baada ya siku arobaini tangia kuzaliwa na kama sita tumia condom?
Kwa kawaida mwanamke baada ya kujifungua inachukua muda kidogo kurudi kwenye mzunguko wake wa mwezi, hii hucheleweshwa zaidi na kunyonyesha..ndio maana kunyonyesha inachukuliwa kama njia mojawapo ya kupunguza uwezekano wa mimba ya mapema. Ukifanya mapenzi na mama mtoto baada ya siku arobaini ataweza kupata mimba. Akipata mimba mfumo wake wa 'hormoni' hutabadilika na maziwa yatapungua hadi kuisha kabisa, kitu ambacho kinaweza kuathiri afya ya mtoto (ndio wanaita kubemenda, sio kweli manii/mbegu ndio zitamuathiri mtoto kupitia maziwa). Sio mbaya kuanza kufanya mapenzi baada ya arobaini, lakini mtumie 'kondomu' ili kuepusha mimba ya haraka ambayo zaidi ya kuweza kuleta athari kwa mtoto, inamuathiri na mama pia.
5. Na mambo mengine ambayo sijayaorodhesha ila yanaweza kunifaa juu ya mtoto mchanga.
Mambo mengine: mpende sana mwanao na mama yake, spend nao time ya kutosha, hii inamsaidia mama kutulia kiakili na kihisia na kutoa maziwa ya kutosha kwa mtoto, shiriki kumhudumia mtoto (kuchange dippers, nepi, etec), cheza na mtoto ujenge bond, and enjoy fatherhood!
Chanzo: Jayson Jr Facebook.