Dhamira yangu sasa ni kuondoka Dodoma wiki ijayo!

Ondoka tuu maana ulikuwa sehemu ya kikwazo kwa mchakato mzima wa kupatikana katiba, Huna hoja , huna nia na huna dhamira nA.uzalendo.
 
Mh. Lema wakati wa kampeni zako 2010 mimi ni miongoni mwa waliokuunga mkono sana haswa kutokana na slogan zako mf. " wao wana pesa sisi tuna Mungu tutashinda", pia ahadi yako ya kujenga stand mbili kubwa nje ya mji (moja njia ya kutokea usa kabla ya kufika mjini na nyingine njia ya kutokea kisongo-ahadi uliitoa kwenye mkutano pale sanawari kwenye kale ka eneo wanako park tax. Ni katika siku hiyo pia ulisema serikali ya ccm inashindwa akili na mmiliki wa naura springs hotel kwa kuweka mt. meru hospital mahali ambapo palipaswa kuwekwa kitega uchumi na kuahidi kuindoa pale na kujenga hospital ya kisasa mahali pengine ili pale pajengwe kitega uchumi) kupitia ahadi zako hizi wadau wa mji wa arusha tuliona fikra mpya zenye kuleta mabadiliko ya kiuchumi na kijamii kwa kuboresha na ku locate kwa usahii miundo mbinu muhimu. Nilikupigia kampeni kwa watu wa karibu kwangu na kuhakikisha wanakuwa mabalozi wa kueneza kampeni yako kwa kila mpiga kura. Bahati mbaya sana hakuna hata moja kati ya ahadi hizi uliyotekeleza au hata kuisemea kimkakati wa utekelezaji baada ya kupata nafasi ya ubunge. kwa hili una deni kwa waliokuchagua au kukuunga mkono kwa moja kati ya ahadi hizi au zote kwa pamoja.

Kwenye bunge la katiba pia hujaonyesha umahiri wa kusababisha niamini kwamba ccm imekuwa kikwazo kwa hoja yako yoyote. pili umekuwa na mahudhurio hafifu kwenye vikao vya bunge hili muhimu (haswa siku za mwanzoni na kama sikosei wewe ni miongoni mwa wajumbe ambao hawakuapishwa/ kuapa kwa wakati sahii hivyo kulazimisha kutumika kwa muda mwingine kuapa badala ya utekelezwaji wa shughuli za bunge. Kutokana na haya yote siungi mkono hatua yako na ninakushauri tulia bungeni toa hoja za msingi na kama zikikwamishwa kwa mizengwe wananchi tutaona na tutaunga mkono hatua yako ila kwa sasa ustahili kuchukua hatua hiyo.

Mkuu mbukoi nadhani unajua jinsi siasa hasa hapo Arusha zinavoendeshwa. Serikali yote ya ccm wanapambana na Lema na wanahakikisha mbunge hatulii akafanya kazi yake vizuri. Tumeshuhudia ukatili ulofanywa na polisi kama mauaji, mabomu na kuwekwa ndani mara kwa mara. Kama kweli wana Arusha mnataka maendeleo mngemshukuru Mungu kuwa na mtu kama Lema jimboni kwenu.
Kuhusu katiba viongozi wa chadema walikosea walipoenda mara ya pili kwa kikwete kwa ajili ya maongezi. Walitakiwa wabaki na msimamo wao waliouita "civil disobedience " na wafanye mikakati wanaojua wao.
Kikwete ni rais wa nchi hii lakin c mtu wa kuaminika kwa jambo lolote kwa sababu moja tu, hataki kumkwaza mtu yoyote. Ni mtu wa kufunika kombe mwanaharamu.....
Kutokana na maamuzi yaliyofanyika Jana na mwenendo wa bunge ulivo, CHADEMA na wapenda maendeleo hawana tena nafasi ya kupigania katiba wanayoitaka wananchi. Uamuzi wa Lema niwakuungwa mkono
 
Last edited by a moderator:
Ondoka tu lema wala hakuna shida.Wewe ondoka tu! usafiri si unao!?Watakaobaki wataendeleza shughuli hiyo muhimu kwa mustakabali wa taifa letu.

Kama ulienda dodoma ukitegemea kwamba CCM Itakuwa inakubeba kama mtoto badala ya kutumia hoja kushawishi, basi wewe ondoka tu kaka!? Nchi hii ni ya kidemokrasia ndugu yangu.
 
bora uondoke tu . hakuna kitu chochote ulichochangia cha maana.. bunge limekuzidi akili... lakini siamini....hivi kweli utaachia posho ya laki tatu hivi hivi tu.? labda sio lema ninaemjua mimi....!

hujitambui mbulura wewe,Nawashauri wazalendo wote wajiondoe kwenye hilo bunge la kipuuzi lililogeuzwa kikao cha magamba kupeana posho!
 
Mheshimiwa Lema,

Kwa nini usiende kuongea na wananchi wako kwanza kabla ya kuchukua uamuzi wako. Ukiweza wape nafasi ya kupiga kura ya SIRI ili waamue kama wangependa uendelee au la.
 
Ondoka tu lema wala hakuna shida.Wewe ondoka tu! usafiri si unao!?Watakaobaki wataendeleza shughuli hiyo muhimu kwa mustakabali wa taifa letu.

Kama ulienda dodoma ukitegemea kwamba CCM Itakuwa inakubeba kama mtoto badala ya kutumia hoja kushawishi, basi wewe ondoka tu kaka!? Nchi hii ni ya kidemokrasia ndugu yangu.

wewe ni mpuuzi tu gamba gumu! hivi kuna demokrasia hapo dodoma??? njaa itakuua!
 
Wadau: Point of Consideration an concetration!;

Kama Lema anaondoka; aondoke kweli, isije ikawa ni sawa na suala lile la kumpa Rais Kikwete siku tatu!? tukadhani ni siku tatu za duniani kumbe mbinguni.Tuzingatie sana mambo haya! Sio watu kufanyafanya mizaha kwenye mambo ya kitaifa kutafuta sifa tu!.
 
bora uondoke tu . hakuna kitu chochote ulichochangia cha maana.. bunge limekuzidi akili... lakini siamini....hivi kweli utaachia posho ya laki tatu hivi hivi tu.? labda sio lema ninaemjua mimi....!

Hahaha abakorakamo frustration zitakumaliza
 
Last edited by a moderator:
Kwa mpinzani yeyote wa ukweli.Ni wakati sasa kuondoka bungeni ili kuwaondolea CCM uhalali wanaouhitaji.
 
Katika wajumbe wote waliokuwapo pale mjengoni ni Lema pekee alielewa kioja cha upigaji kura wa jana.
Kimsingi kamati iliwasilisha mapendekezo ya namna ya upigaji kura...na kabla wajumbe hawajaridhia namna hiyo ya upigaji kura tukajionea inaanza kutumika!sielewi kilichokuwa kinapigiwa kura ni kipi ilihali kimantiki wajumbe walikubali probably through maridhiano.Ni heri ingetumika kura ya kuhoji kwa ujumla au kura ya siri au kura ya wazi....yaani ni ujuha kalulu wa aina yake...ONLY LEMA NDIYE ALIYELIONA HILO!

I support you,rudi nyumbani kwani kuna mengi ya kufanya kuliko unafiki,vioja na uharibifu wa fedha unaoendelea hapo dodoma

Alipoitwa jina sikumwona akijibu kwa kipaza sauti ,ckumwona akienda mbele kupiga kura na wala sikuona akipelekewa karatasi apige kura, nadhani hakupiga kura(I stand to be corrected)
 
Hakuna mwananchi mwenye akili timamu anayemuhitaji Lema kwenye Bunge la Katiba.

Haya ndiyo matatizo ya wanasiasa uchwara ya kuamini kile anachokitaka ni lazima kifanyike hivyo hivyo kuklitokea mawazo tofauti anasema demokrasia imebakwa. Hivi hapa anayebaka demokrasia ni yupi ni huyu asyetaka wazo tofauti na la kwake na likitokea anabeba mabegi anakimbia au ni yule aliye tayari kusimamia kwa hoja wazo lake? Mimi nafikiri Lema sio mwanasiasa ameingia kwa bahati mbaya tu aache siasa akasimamie mashamba yake hukooo.
 
Huyu kama ni mume wangu nnampa talaka hukohuko aliko. Aibu kubwa sana mwanamme anaejiita mpambanaji kukata tamaa. Khaa! Mwanamme mzima hata haoni haya kuongea namna hiyo? chadema poleni sana na watu wa Arusha, huyo ndiye "mpambanaji" mliyemchaguwa!

Bora angejiita mpambaji.

Sasa naamini zile picha zilikuwa ni za kweli.

Kuna mambo mengine ambayo kwa mtu mwenye FIKRA HURU, siyo mkumbo lazima ajiulize mara mbili! Kura ya WAZI????!!!! Tutaendelea kupigwa gap na wanajumuia wenzetu hivihivi. Kwa ufupi Tanzania bla bla na mambo ya kupindisha pindisha mambo ni mengi. Kilichobaki ni mnyororo tu na kufuata MIKUMBO baada ya uamuzi ule wa jana. Hoja ikikubalika na mmoja basi wale wooote wataunga, mmoja akipinga wooote watapinga. Hakuna hata mmoja atajifikirisha. Dada FF, leo trh 29.03.2014, PLEASE MARK MY WORDS! Ni kufuatak mikumbo tu. Inafifisha mambo mengi, tutaendelea kudumaa na Tanzania yetu hadi INFINITY. Japo wengi wape lakini jambo lililoungwa mkono siyo NAMNA BORA ya kufikia maamuzi!
 
Lema nakubaliana na wewe kwenye hili suala, amini amini nawaambieni hapo Dodoma ni kupoteza muda na fedha za umma, hakuna katiba hapo,
Lema usiogope kwa kuwa hujawahi kuogopa, najua hata humu kuna maccm wanabeza, yamkini kuna wapenda mabadiliko watakushangaa, au hata viongozi wa ukawa na wachama, watakushauri tofauti,
Hakika usipotekeleza uamuzi wako utaingia kwenye kundi la wasaliti wa wananchi wanyonge, narudia tena, ktk mazingira hayo hakuna katiba mpya ya watanzania bali ni katiba ya maccm,
 
Back
Top Bottom