Dhambi ambazo huwezi tubu peke yako bila kushirikisha watumishi wa Mungu

Mkuu uko sahihi kabisa! Lakini hata hivyo Sadaka ya Ukombozi ni ile iliyopatikana pale Msalabani,yaani damu ya Yesu,si vinginevyo,
(Mathayo26:28)
Hakuna Sadaka nyingine inayoweza kumridhisha Mungu atusamehe zaidi ya hiyo iliyopatikana pale Msalabani,
(Waebrania10:6-10)
Chakuzingatia tu kwa kuwa Sadaka hiyo ilitolewa mara moja mara mtu anapaswa kutubu dhambi zake kwa KUMAANISHA KUZIACHA hata kama dhambi hiyo ni kubwa kiasi gani mf.Kuua,Kuzini,Kulawiti,kubaka,kunyanganya,nk atasamehewa tu,
(Isaya1:18) (Mithali28:13)
HATARI iliyopo ni pale mtu ambapo ametubu dhambi,harafu baada ya kujifunza Kweli ya Neno la Mungu kwa muda mrefu ikatokea AKAFANYA DHAMBI KWA KUKUSUDIA huku akijua ni dhambi mf.ni mtumishi wa Mungu,askofu,nk pale anamhuzunisha Roho Mtakatifu! Kusamehewa siyo rahisi hivi hivi,ni shughuli kweli kweli,(Waebrania10:26-29)
 
Mkuu uko sahihi kabisa! Lakini hata hivyo Sadaka ya Ukombozi ni ile iliyopatikana pale Msalabani,yaani damu ya Yesu,si vinginevyo,
(Mathayo26:28)
Hakuna Sadaka nyingine inayoweza kumridhisha Mungu atusamehe zaidi ya hiyo iliyopatikana pale Msalabani,
(Waebrania10:6-10)
Chakuzingatia tu kwa kuwa Sadaka hiyo ilitolewa mara moja mara mtu anapaswa kutubu dhambi zake kwa KUMAANISHA KUZIACHA hata kama dhambi hiyo ni kubwa kiasi gani mf.Kuua,Kuzini,Kulawiti,kubaka,kunyanganya,nk atasamehewa tu,
(Isaya1:18) (Mithali28:13)
HATARI iliyopo ni pale mtu ambapo ametubu dhambi,harafu baada ya kujifunza Kweli ya Neno la Mungu kwa muda mrefu ikatokea AKAFANYA DHAMBI KWA KUKUSUDIA huku akijua ni dhambi mf.ni mtumishi wa Mungu,askofu,nk pale anamhuzunisha Roho Mtakatifu! Kusamehewa siyo rahisi hivi hivi,ni shughuli kweli kweli,(Waebrania10:26-29)
Nilichogundua, wengi wanaenda church na Bado wanazini,

Na wanaamini, unaweza kuzini, Kisha ukatubu pekeako chumbani ukasamehewa,

Dhambi hiyo shetani anewekeza sana maana anajua ukitenda ,Utaratibu wa kumalizana nayo ni ngumu,

Umeoa au Kuolewa Kwa Mfano, ukaanguka katika UZINZI na mke wa Jirani au na kahaba,

Lazima utubu Kwa mkeo kama umezini na kahaba,

Kama umezini na mke wa mtu lazima itafutwe namna ya kumalizana na mume wa mke uliyezini naye, na hapo, mtumishi wa Mungu anahutajika Ili kusaidia mchakato kuisha Kwa Amani.

Wengi wanachukulia pia dhambi ya UZINZI, inapeleka wengi kuzimu na WA eokoka na hawajui chanzo.
 
mkuu
Katika kutafuta toba kwa Mungu hakuna masharti zaidi ya kumuamini Bwana Yesu Kristo kwamba alikufa kwa ajili ya dhambi zetu na kupitia toba ya kumaanisha kuacha dhambi tunasamehewa dhambi zetu.

Hayo ya kusema baadhi ya dhambi lazima Mtumishi wa Mungu ndo akutubishe ama akuongoze ni sawa na kuweka Lango jipya zaidi ya Yesu Kristo ili kumfikia Baba kwa minajili ya ondoleo la dhambi.

Yesu aliweka category mbili za dhambi,
  1. Dhambi zote atendazo mwanadamu dhidi ya mwanadamu -- Hizi zote zinasameheka kwa toba ya kumaanisha kuziacha
  2. Dhambi atendayo mwanadamu dhidi ya Mungu nayo ni Kumkufuru ROHO MTAKATIFU -- Hii HAISAMEHEKI hata ufanye toba ya kuongozwa na mitume na manabii. Pia hii mpaka uifanye unakuwa umefungua mageti mengi sana kumsogelea Mungu na kuzijua siri za Mbinguni na kuishi katika tumaini la Roho Mtakatifu. Hivyo ukimsaliti unakuwa fungu moja na ibilisi muasi ambaye tayari adhabu yake imewekwa tangu kale
Tunachohitaji kutoka kwa Watumishi yaani mitume na manabii ni muongozo namna ya kukisogelea Kiti cha Enzi cha Mungu Baba kwa unyenyekevu, kujikana, kujuta na kutubu kwa kumaanisha kuziacha dhambi.
Umenena vyema,

Kutubu inahitajika mwongozo wa watumishi,

Nikuulize,

Umeoa, ikitokea umezini na mke wa Jirani Yako,

Unaamini ukitubu sirini, na huyo mzinzi mwenzio akitubu sirini bila mkeo kujua, na bila mume wa uliyezini naye,

Unaamini Mungu atasamehe?
 
Tupe mfano wa category ya pili
Category ya pili ni mtu aliyepanda viwango vikubwa vya utumishi,

Mtu amefikia Hadi level ya uchungaji, au Nabii, amejazwa na kuongozwa na Roho mtakatifu, anaisikia sauti ya Mungu live,

Halafu mtu huyo aamue Kwa hiari yake kwenda Kwa Waganga atumie uchawi madhabahuni kujipatia kipato.

Kingine ni hivi,

Unakuta mtu anahubiri barabarani, wewe hujui na hujathibitisha kuwa Nia ni anahubiri INJILI ametumwa na Mungu au la, wewe inakwenda pembeni na kuanza kumsema live kuwa ni mwongo,

Au unamsema live na kumtukana Yeye na KAZI afanyazo, hapo unajiweka katika nafasi ya kumkufuru Roho mtakatifu.

Kwa ufupi, mtu aliyejazwa Roho mtakatifu, amepanda viwango Hadi kufikia kunena Kwa lugha, ana karama ya unabii na ana macho ya Rohoni,

Mtu huyo kuasi huasi Kwa kudhamiria Si kudanganywa na shetani maana Kwa viwango hivyo, mitego yote ya shetani Huwa unaiona hata kabla haijakufikia, na unakuwa unajua namna ya kuepuka.
 
Watumishi wa Mungu waadilifu wamebaki wachache siku hizi.
Wengi wanakwenda kimwili..hii inaondoa kuaminiwa na jamii.
Hili nalo hulioni?
Na Mtumishi naye akitenda dhambi,akatubie kwa nani?
Je,Biblia imeweka utaratibu gani katika Toba?
Kuasi Kwa watumishi, hakukupi fursa ya kutengeza Utaratibu wako,

Mwombe Roho mtakatifu akuonyeshe watumishi sahihi wankukusaidia. Wapo Bado wenye unyofu wa moyo.
 
Nilichogundua, wengi wanaenda church na Bado wanazini,

Na wanaamini, unaweza kuzini, Kisha ukatubu pekeako chumbani ukasamehewa,

Dhambi hiyo shetani anewekeza sana maana anajua ukitenda ,Utaratibu wa kumalizana nayo ni ngumu,

Umeoa au Kuolewa Kwa Mfano, ukaanguka katika UZINZI na mke wa Jirani au na kahaba,

Lazima utubu Kwa mkeo kama umezini na kahaba,

Kama umezini na mke wa mtu lazima itafutwe namna ya kumalizana na mume wa mke uliyezini naye, na hapo, mtumishi wa Mungu anahutajika Ili kusaidia mchakato kuisha Kwa Amani.

Wengi wanachukulia pia dhambi ya UZINZI, inapeleka wengi kuzimu na WA eokoka na hawajui chanzo.
Wamagharibi/uarabuni waliharibu sn ubongo wamwafrika kwa dini hii kitu kupona itachukua muda sn and possible isiwepo kabisa
 
....Nikuulize,

Umeoa, ikitokea umezini na mke wa Jirani Yako,

Unaamini ukitubu sirini, na huyo mzinzi mwenzio akitubu sirini bila mkeo kujua, na bila mume wa uliyezini naye,

Unaamini Mungu atasamehe?
Baada ya toba unafanya kitu kinaitwa jambo la kijamii ambalo linaitwa Malipizi ya ndoa. Hili siyo toba bali marekebisho baada ya kutengeneza na Mungu kwanza.
 
Baada ya toba unafanya kitu kinaitwa jambo la kijamii ambalo linaitwa Malipizi ya ndoa. Hili siyo toba bali marekebisho baada ya kutengeneza na Mungu kwanza.
Fafanua,

Hilo jambo la Kijamii linaloitwa malipizi ya NDOA ni lipi?

Una HAKIKA, BIBLIA kama Katiba, haijatoa mwongozo juu ya nini kifanyike baada ya mtu kuzini au kufanya uasherati nje ya NDOA takatifu?
 
Fafanua,

Hilo jambo la Kijamii linaloitwa malipizi ya NDOA ni lipi?

Una HAKIKA, BIBLIA kama Katiba, haijatoa mwongozo juu ya nini kifanyike baada ya mtu kuzini au kufanya uasherati nje ya NDOA takatifu?
Toba pekee ni ile unayouelekeza moyo wako kwa Mungu kuomba rehema zake.

Hiko ulichokitolea mfano ni matengenezo na siyo toba. Na hufanyika baada ya toba
 
Toba pekee ni ile unayouelekeza moyo wako kwa Mungu kuomba rehema zake.

Hiko ulichokitolea mfano ni matengenezo na siyo toba. Na hufanyika baada ya toba
Una andiko linaloshabiiana na usemacho kuwa hii ni TOBA na hii ni matengenezo?

Huoni wote wanaopinga wanaopinga hata huo Utaratibu unaouita matengenezo, sababu Yao kuu ni kuwa hata watumishi wanatenda dhambi kama hizo?

Nilichoandika ni Kweli tupu,

Kubalini UKWELI muwe huru.
 
Toba pekee ni ile unayouelekeza moyo wako kwa Mungu kuomba rehema zake.

Hiko ulichokitolea mfano ni matengenezo na siyo toba. Na hufanyika baada ya toba
Soma

(Mathayo 5:25)

Imetoa Utaratibu wazi, kabla ya kwenda kuomba msamaha Kwa Mungu, malizana na uliyemkosea kwanza,

Hata sadaka madhabahuni hupasi Kutoa ikiwa una tatizo na mtu hujamalizana nae.

Wengi mnalaaniwa sababu unakuta umezini Kwa Mfano, hujamalizana msamaha na mkeo, na mume wa uliyezini naye, unatubu kimya kimya Kisha inapeleka sadaka madhabahuni, sadaka hiyo hugeuka na kulaani KAZI zako ndomana hamfanikiwi katika KAZI mfanyazo na hamjui sababu ni nini!!

Mbinguni Si rahisi kama m avyodhani.
 
Nilichogundua, wengi wanaenda church na Bado wanazini,

Na wanaamini, unaweza kuzini, Kisha ukatubu pekeako chumbani ukasamehewa,

Dhambi hiyo shetani anewekeza sana maana anajua ukitenda ,Utaratibu wa kumalizana nayo ni ngumu,

Umeoa au Kuolewa Kwa Mfano, ukaanguka katika UZINZI na mke wa Jirani au na kahaba,

Lazima utubu Kwa mkeo kama umezini na kahaba,

Kama umezini na mke wa mtu lazima itafutwe namna ya kumalizana na mume wa mke uliyezini naye, na hapo, mtumishi wa Mungu anahutajika Ili kusaidia mchakato kuisha Kwa Amani.

Wengi wanachukulia pia dhambi ya UZINZI, inapeleka wengi kuzimu na WA eokoka na hawajui chanzo.
Fahamu hao wanakuwa hawajabadilishwa bado ni watoto wachanga kiroho,ndiyo
Mi misingi ya kutubia kazi zisizo na uh na uhai,Waebrania5:12-14)
Nilichogundua, wengi wanaenda church na Bado wanazini,

Na wanaamini, unaweza kuzini, Kisha ukatubu pekeako chumbani ukasamehewa,

Dhambi hiyo shetani anewekeza sana maana anajua ukitenda ,Utaratibu wa kumalizana nayo ni ngumu,

Umeoa au Kuolewa Kwa Mfano, ukaanguka katika UZINZI na mke wa Jirani au na kahaba,

Lazima utubu Kwa mkeo kama umezini na kahaba,

Kama umezini na mke wa mtu lazima itafutwe namna ya kumalizana na mume wa mke uliyezini naye, na hapo, mtumishi wa Mungu anahutajika Ili kusaidia mchakato kuisha Kwa Amani.

Wengi wanachukulia pia dhambi ya UZINZI, inapeleka wengi kuzimu na WA eokoka na hawajui chanzo.
Hii dhambi inaangusha sana watoto wengi wa Mungu! Mpaka baadhi ya Watumishi wa Mungu.
 
Fahamu hao wanakuwa hawajabadilishwa bado ni watoto wachanga kiroho,ndiyo
Mi misingi ya kutubia kazi zisizo na uh na uhai,Waebrania5:12-14)

Hii dhambi inaangusha sana watoto wengi wa Mungu! Mpaka baadhi ya Watumishi wa Mungu.
Mtumishi wa Mungu Kwa Mfano, azini na mke wa muumini,

Hivi atalimalizaje hili na kupata ujasiri wa kuendelea kusimama madhabahuni?

Njia ya Mbinguni ni nyembamba sana, halafu watu wananitukana kana kwamba niliyoandika nimetoa kichwani mwangu, wakati yote niliyoandika ni biblical.
 
Mtumishi wa Mungu Kwa Mfano, azini na mke wa muumini,

Hivi atalimalizaje hili na kupata ujasiri wa kuendelea kusimama madhabahuni?

Njia ya Mbinguni ni nyembamba sana, halafu watu wananitukana kana kwamba niliyoandika nimetoa kichwani mwangu, wakati yote niliyoandika ni biblical.
Hukumu yake haiishi! Kwa Mtumishi wa Mungu,huko ndiyo kumkufuru Roho Mtakatifu! Ni gharama kuitubu.
 
Mnajiiiiiiiipa presha .Nan kakwambia Mungu ana formalities za kibinadam zaid namna hii!!???

Ujue anayekuondolea hatia sio kutubu mbele za mtu. NI Holly spirit, period!!!! Hii kwenda mbele za watu imekaa kisailolojia tu ili ku bust iman yako ila hata sio lazima wala haina ukwel...
Sahihi. Ni mtazamo wa mtu tu.
 
Salaam shalom.

INTRODUCTON.

Imeandikwa, Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na haki, hata atuondolee dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote.( 1 Yoh 1:9).

Dhambi ni kutotii, kwenda kinyume na maelekezo ya Mungu. Na Roho mtakatifu yupo kutukumbusha dhambi zetu Ili tuzitibie Ili tuendelee kuwa WATAKATIFU.

DHAMBI AMBAZO KAMWE HATIA YAKE HAITAKUONDOKA HADI USHIRIKISHE WATUMISHI WA MUNGU ILI UOMBEWE UKIAMBATISHA NA SADAKA YA UKOMBOZI NI ZIFUATAZO:


1. ZINAA NA UASHERATI.

UASHERATI ni kufanya Tendo la zinaa na mtu nje ya NDOA asiye mkeo au mumeo.

UZINZI ni kufanya tendo la uchafu, zinaa kabla ya Kuoa au Kuolewa.

Ukizini na mke wa mtu au mume wa Mtu, au ukiota unazini ndotoni na mtu au watu usiowafahamu, usijidanganye kuwa ukitubu sirini utasamehewa, HATIA itaendelea kuwepo Hadi uwatafute watumishi wa Mungu wa Kweli Ukiwa na sadaka ya Ukombozi. Watumishi Wana BUSARA ya kusuluhisha dhambi hiyo pande zote mbili Ili ufunguliwe.

Kuzini na mke wa mtu, faini ya juu ni kulipa Mahari aliyotoa muoaji Ili akusamehe, kushirikisha mtumishi ni kutumia BUSARA ya Mungu Ili muibiwa mke aridhie kukusamehe kutomlipa, au akupunguzie faini.

(Mithali 6:20-35,) UZINZI hufunga NAFSI, Amri ya Mungu usizini (Kumbukumbu la torati 5:1-21)

2. USHOGA.

Ikiwa uliwahi kuwa shoga, ukaamua kuacha, kamwe usitubu sirini na kuishiwa hapo, USHOGA huambatana na mapepo na kufungwa NAFSI, mfungwa kamwe hawezi jifunguanpingu mwenyewe, unawahutaji watumishi wa Kweli Ili UOMBEWE na kuwekwa huru, sadaka ni LAZIMA Ili itolewe huko. ( Mwanzo 38:9-10) Mungu alimwua Onani Kwa kumwaga shahawa nje ya uke makusudi Ili asizae na mke aliyepewa.

3. USAGAJI.

Mwanamke pia aliyewa kufanya dhambi hiyo, huwezi kufunguliwa na Utumwa na HATIA hiyo pekeako Kwa kutubu sirini, nenda Kwa watumishi wa Kweli, Ukiwa na sadaka ya Ukombozi. mwanzo 38:9-10, Onani aliuwawa Kwa dhambi hiyo, ( kumbukumbu la torati 5:1-21) Amri za Mungu Usiue.

4. PUNYETO/ KUJICHUA.

Ikiwa uliwahi kujichua, ukaamua kuacha, unahitaji kwenda Kwa mtumishi wa Mungu wa Kweli Ukiwa na sadaka ya Ukombozi Ili ufunguliwe, Mpiga PUNYETO ni mfungwa, ni mke au mume wa Roho chafu katika Ulimwengu wa Roho, hivyo kufunguliwa ni LAZIMA utoe sadaka, uvunje NDOA chafu hiyo ya kiroho na hati ya NDOA chafu ya kiroho iondolewe, usipofanya hivyo, unajidanganya. Mbinguni huingii ng'o!! (Mwanzo 38:1-25) Mungu alimwua Onani Kwa kumwaga shahawa nje ya uke Ili asizae na mke wa marehemu kaka yake.
Neno Hilo hapo juu ni ROHO. Amen.

5.MWANAMKE KUOA MWANAMKE/MWANAUME KUOA MWANAUME MWENZIE.

Kutubu dhambi hii sirini bila watumishi wa Mungu ni kujidanganya. Chukua sadaka, nenda Kwa mtumishi, Sema Kweli Ili UOMBEWE na kufunguliwa, NDOA haramu ivunjwe na ufungwa wako kiroho uondolewe. ( Mwanzo 38:9-10, (Mithali 6:20-35)Amen.

6. ORAL SEX.

Ikiwa uliwahi kushiriki oral sex, kunyonya au kuramba Kwa mdomo sehemu za Siri za mwanamke au Mwanaume na ukatambua ni DHAMBI, ukaacha, Bado u kifungoni.

Chukua sadaka, mwone mtumishi wa Kweli wa Mungu ufunguliwe na Mungu.

(1 Wakorintho 6:9-11), (Ufunuo wa Yohana 21:8) (Mzo 38:9-10) Mungu alimwua Onani Kwa kutenda Tendo la NDOA kinyume.

7. ABORTION./ UTOAJI MIMBA/ KUFUNGA UZAZI/ KUTUMIA VIDONGE VYA KUPANGA UZAZI.

Kimbia haraka Kwa mtumishi wa Mungu wa Kweli ,beba sadaka kulingana na uwezo wako, UOMBEWE ufunguliwe.

(Kumbukumbu la torati 5:1-21) Usiue ni Amri ya Mungu.

Ukipuuza Utakataliwa GETI la Mbinguni.

9. IKIWA ULIWAHI TUMIA DAWA ZA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME/ KIKE.

(Mwanzo 38-9-10) Mungu alimwua Onani Kwa kutenda kinyume na Utaratibu wa Tendo la NDOA na taratibu za UZAZI alizoweka Mungu.


Chukua sadaka, mwone mtumishi wa Kweli UOMBEWE na kufunguliwa.

10. MAUAJI.

Ikiwa uliwahi kuua bila kukusudia ,ukahukumiwa JELA ukatoka, ikiwa uliua Kwa Siri na hukubainika, ikiwa ulishiriki kuua, usijidanganye kuwa unaweza kutubu sirini, HATIA Ili ikuondoke uwe na Amani, Tafuta kiongozi wa Mungu wa Kweli mwenye BUSARA za Mungu, akuongoze Cha kufanya, utoe pia sadaka ya Ukombozi. ( Acts 9:3-6) Sauli alikuwa mwuaji, Yesu alimwelekeza aende Kwa mtumishi.

(Kumbukumbu la torati 5:1-21) Mungu ameamrisha " Usiue".

11. IBADA ZA SANAMU, KUSHIRIKI IBADA ZA WAFU NA KUTOA SADAKA KWA MIZIMU KIMILA NK NK.

Kushiriki Ibada za KIMILA na Kutoa sadaka Kwa Roho za kishetani za Mababu, ni DHAMBI pia, ni kufungwa ni Utumwa ambao huwezi kujifungua pekeako.

(Mithali 6:20-35) kifungo Cha NAFSI sababu Ibada ya sanamu ni UZINZI kiroho mbele za Mungu, ( UFUNUO 21:8, (1 korinthians 6:9-11) watendao uchawi na Ibada ya sanamu watatupwa Jehanum.

Ukiamua kuacha na kuokoka, hatua inayofuata ni kushirikisha watumishi kukusaidia kukutenga na madhabahu hizo.

Sadaka ni LAZIMA, sababu, Ulimwengu wa Nuru na Giza sadaka ni inevitable. Amen

HITIMISHO.

Dhambi nilizotaja hapo juu, ni baadhi tu ya dhambi ambazo huwezi tubu pekeako, zimetajwa sawasawa na Ruhusa ya Roho mtakatifu Kwa mtumishi wake sawasawa na ufunuo wake apendavyo.

NB: Si DHAMBI zote zinahitaji kuona mtumishi wa Kweli kukusaidia kufunguliwa pingu za dhambi, ni baadhi ya dhambi ambazo Zina vifungo na attachment na maagano ya kipepo na kishetani.

ANGALIZO: Sadaka tutoazo Si Kwa ajili ya kununua Muujiza, au kununua Msamaha wa Mungu, Yesu msalabani alikwisha maliza yote Kwa Damu yake msalabani. Sadaka tunatoa kama shukrani tu na kuonyesha Upendo Kwa Yale Mungu alikwisha tutendea.

Mungu awabariki.

Source: Nabii Justine Ibrahim, U-Tube., Promover Tv channel U-Tube.

Ikiwa hujampokea Yesu kuwa BWANA na Mwokozi wako, fuatisha Sala hii,

EE YESU, NINAKIRI KWAKO KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NINAOMBA UNISAMEHE, ULIFUTE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU,ULIANDIKE KATIKA KITABU CHA UZIMA, NINAOMBA UWEZO WA KUSHINDA DHAMBI, NIWEZESHE NIISHI MAISHA MATAKATIFU.

Ameen
Kuwasaidia wanaojihusisha na hayo mambo ili iwe rahisi kuwatongoza.... Ni hayo tu kwa Sasa. Mungu hahitaji dalali ili akuondolee dhambi !!
 
Kuwasaidia wanaojihusisha na hayo mambo ili iwe rahisi kuwatongoza.... Ni hayo tu kwa Sasa. Mungu hahitaji dalali ili akuondolee dhambi !!
Ukizini na mke wa mtu unaingia chumbani, unapiga magoti na kutubu Kwa Mungu, Badala ya kutubu Kwa uliyemwibia mke?

Yaani uibe mke wa Juma, Badala ya kutubu Kwa juma, unatubu Kwa Mungu?

WANADAMU mna mapuuza!!
 
Back
Top Bottom