A
Anonymous
Guest
Mimi ni dereva Bodaboda napatikana Kata ya Mbezi Msumi hapahapa Dar es Salaam, tulijichanga tukanunua eneo la ardhi katika Kijiji kinaitwa Zumba kipo Boko Mnemela, Kibaha Mkoani Pwani, yaliyotukuta ni makubwa.
Tulichofanya tulioneshwa eneo lenye ukubwa wa ekari 10, tukiwa Bodaboda 50 tukajichanga na kununua eneo hilo kwa bei ya Shilingi 10,000,000 (Shilingi milioni 10).
Kabla ya kununua pia tulienda hadi kwa watu wa Ardhi Kibaha, wakatuambia kuwa eneo hilo halina tatizo tunaweza kuendelea na mchakato wa manunuzi.
Tukalipa pia 10% ya Serikali ya Mtaa ambayo ni Shilingi Milioni 1, baada ya hapo tukaanza mchakato wa kusafisha kwa awamu, tulianza kutumia shilingi 700,000, baadaye 600,000 na gharama nyingine nyingi ambazo jumla zilifika Shilingi Milioni 5.
Lengo ilikuwa tugawane ‘Sweka Mita’ 800 kila mmoja lakini baadaye ndipo tukagundua kuwa eneo hilo ni mali ya Mwekezaji Mo Dewji ambaye ana ekari 8,000 pande hizo.
Aliyetuuzia anaitwa Faraji, baada ya kuanza kufuatilia tukamkamata yeye na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa anaitwa Saleh kwa kuwa alisimama kama dalali lakini kumbe yeye na wauzaji walituingiza chaka na lengo lao ni moja.
Tukawapeleka Kituo cha Polisi Mji Mdogo Kibaha, yule Mwenyekiti akadhaminiwa na Askari flani ambaye ana cheo kituoni hapo, anaitwa Samata.
Tukamfikisha Muuzaji (Faraji) katika Mahakama ya Mwanzo Kibaha, akaahidi kuwa atarejea fedha hizo na kusema kuwa yeye katika ile hela tuliyolipa alichukua Shilingi Milioni 3 tu nyingine zilichukuliwa na Mwenyekiti wa Mtaa.
Baada ya kutoka Mahakamani Faraji akakimbia na hatukujua alipo, Polisi aliyekuwa anasimamia kesi akatuambia sisi ndio tumtafute, tukaenda kwa Hakimu kueleza malalamiko yetu ndipo Hakimu akatoa maelekezo kwa Askari huyo kuhakikisha mtuhumiwa anapatikana.
Baadaye tukagundua Mwenyekiti Saleh na Mwenyekiti mwingine wa mitaa hiyo ya Boko anayefahamika kwa jina la Mika wote ni matapeli na wamekuwa wakifanya michezo hiyo ya kutapeli watu wengi.
Tulifikisha suala letu hati kwa Mkuu wa Wilaya, Nikki Wa Pili akaagiza mafiasa wake kwenda eneo la tukio.
Tulichokibaini baadaye tukiwa na maafisa hao wa Wilayani ni kuwa kule Boko eneo tulilouziwa kulikuwa na mawe ya alama ambayo yaliweka pale kinyume cha Sheria kwa kuwa yaliibiwa kutoka Halmashauri ya Mji wa Kibaha na kupelekwa Kibaha Vijijini, yamefikaje? Hilo sisi hatujui.
Inavyoonekana kuna watu wakubwa kwenye Mamlaka ya Ardhi, Serikali za Mtaa na Polisi wanajua michezo inayoendelea na hakuna hatua zinazochukuliwa.
Wanaona sisi watu wenye kipato cha chini hatuna sauti ndio maana wanaacha tunaendelea kuonewa na hatupati haki yetu.
Tunaomba Serikali Kuu iangalie haki yetu inayopotea, pia niwashauri wanaotaka kununua viwanja maeneo ya Boko Mnemela kuwa makini, upigaji upo njenje huku.
Tulichofanya tulioneshwa eneo lenye ukubwa wa ekari 10, tukiwa Bodaboda 50 tukajichanga na kununua eneo hilo kwa bei ya Shilingi 10,000,000 (Shilingi milioni 10).
Kabla ya kununua pia tulienda hadi kwa watu wa Ardhi Kibaha, wakatuambia kuwa eneo hilo halina tatizo tunaweza kuendelea na mchakato wa manunuzi.
Tukalipa pia 10% ya Serikali ya Mtaa ambayo ni Shilingi Milioni 1, baada ya hapo tukaanza mchakato wa kusafisha kwa awamu, tulianza kutumia shilingi 700,000, baadaye 600,000 na gharama nyingine nyingi ambazo jumla zilifika Shilingi Milioni 5.
Lengo ilikuwa tugawane ‘Sweka Mita’ 800 kila mmoja lakini baadaye ndipo tukagundua kuwa eneo hilo ni mali ya Mwekezaji Mo Dewji ambaye ana ekari 8,000 pande hizo.
Aliyetuuzia anaitwa Faraji, baada ya kuanza kufuatilia tukamkamata yeye na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa anaitwa Saleh kwa kuwa alisimama kama dalali lakini kumbe yeye na wauzaji walituingiza chaka na lengo lao ni moja.
Tukawapeleka Kituo cha Polisi Mji Mdogo Kibaha, yule Mwenyekiti akadhaminiwa na Askari flani ambaye ana cheo kituoni hapo, anaitwa Samata.
Tukamfikisha Muuzaji (Faraji) katika Mahakama ya Mwanzo Kibaha, akaahidi kuwa atarejea fedha hizo na kusema kuwa yeye katika ile hela tuliyolipa alichukua Shilingi Milioni 3 tu nyingine zilichukuliwa na Mwenyekiti wa Mtaa.
Baada ya kutoka Mahakamani Faraji akakimbia na hatukujua alipo, Polisi aliyekuwa anasimamia kesi akatuambia sisi ndio tumtafute, tukaenda kwa Hakimu kueleza malalamiko yetu ndipo Hakimu akatoa maelekezo kwa Askari huyo kuhakikisha mtuhumiwa anapatikana.
Baadaye tukagundua Mwenyekiti Saleh na Mwenyekiti mwingine wa mitaa hiyo ya Boko anayefahamika kwa jina la Mika wote ni matapeli na wamekuwa wakifanya michezo hiyo ya kutapeli watu wengi.
Tulifikisha suala letu hati kwa Mkuu wa Wilaya, Nikki Wa Pili akaagiza mafiasa wake kwenda eneo la tukio.
Tulichokibaini baadaye tukiwa na maafisa hao wa Wilayani ni kuwa kule Boko eneo tulilouziwa kulikuwa na mawe ya alama ambayo yaliweka pale kinyume cha Sheria kwa kuwa yaliibiwa kutoka Halmashauri ya Mji wa Kibaha na kupelekwa Kibaha Vijijini, yamefikaje? Hilo sisi hatujui.
Inavyoonekana kuna watu wakubwa kwenye Mamlaka ya Ardhi, Serikali za Mtaa na Polisi wanajua michezo inayoendelea na hakuna hatua zinazochukuliwa.
Wanaona sisi watu wenye kipato cha chini hatuna sauti ndio maana wanaacha tunaendelea kuonewa na hatupati haki yetu.
Tunaomba Serikali Kuu iangalie haki yetu inayopotea, pia niwashauri wanaotaka kununua viwanja maeneo ya Boko Mnemela kuwa makini, upigaji upo njenje huku.