Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Leo gazeti la Majira lleo imeandika kwa kumnukuu Jaji Mark Bomani akisema kwamba Dowans wasipolipwa kuna hatari mali za nchi hii zilizo nje ya nchi kuweza kukamatwa.
Aidha katika mdahalo mmoja wa TV hivi karibuni kuna mchangiaji mmoja alitamka hayo hayo. Jee Wana-JF hii ya kukamatwa mali za nchi yetu zilizo nje lawezekana kwa suala hili la kudaiwa na Dowans? -- kwani nafahamu serikali yetu inadaiwa na wengi tu, wa ndani humu na wa nje. Kwa nini hili la Dowans ndiyo liibue hofu kubwa na ya kipekee ya kukamatwa mali?
Nawasilisha.