NyaniMzee
JF-Expert Member
- Nov 24, 2010
- 396
- 727
Kama wewe ni mkristo na una mke mkorofi na umechoka naye ila ukifikiria kumwacha unashindwa kwa vile divorce hairuhusiwi katika christian marriage, jaribu kufanya hivi:
Mwambie kuwa umefikiria na kuamua kubadili dini, usipoteze muda waone wahusika usilimishwe. Hatakataa wewe kubadili dini kwa vile ni haki yako. Utakapokuwa converted baada ya muda mwambie dini yako inaruhusu kuoa mke wa pili na una uwezo wa kuwatunza wote.
Bila kupoteza muda tafuta umpendaye na funga ndoa, huyo mkorofi atakuwa bi mkubwa na bi mdogo ni huyo mpya. Kama Bi mkubwa atastahimili huo ukewenza ukorofi utakuwa umeisha.
Lakini uwezekano ni kuwa atafungasha na kutokokomea ajuako yeye, utabaki na Bi mdogo ambaye with time we mwambie umetafakari na kuona huna budi kurejea ktkt dini yako ya awali.
Chukua hatua haraka na rudi kundini hapo utakuwa umeondokana na kelele, technical divorce.
Mnasemaje hapo wanaJF?
Mwambie kuwa umefikiria na kuamua kubadili dini, usipoteze muda waone wahusika usilimishwe. Hatakataa wewe kubadili dini kwa vile ni haki yako. Utakapokuwa converted baada ya muda mwambie dini yako inaruhusu kuoa mke wa pili na una uwezo wa kuwatunza wote.
Bila kupoteza muda tafuta umpendaye na funga ndoa, huyo mkorofi atakuwa bi mkubwa na bi mdogo ni huyo mpya. Kama Bi mkubwa atastahimili huo ukewenza ukorofi utakuwa umeisha.
Lakini uwezekano ni kuwa atafungasha na kutokokomea ajuako yeye, utabaki na Bi mdogo ambaye with time we mwambie umetafakari na kuona huna budi kurejea ktkt dini yako ya awali.
Chukua hatua haraka na rudi kundini hapo utakuwa umeondokana na kelele, technical divorce.
Mnasemaje hapo wanaJF?