Dawa madhara ya amoeba

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,318
33,125
MARADHI YA AMOEBA.jpg

WATU wengi wamekuwa wakisumbuliwa na ugonjwa wa Amoeba lakini hupuuzia pale dalili zinapoanza, ni ugonjwa mbaya ambao ukikaa sana tumboni husababisha madhara makubwa , kama kuhara damu kupindukia, kutapika, kusikia kizunguzungu, kukosa hamu ya kula na kupata homa kali.

Ugonjwa huu mara nyingi husababishwa na maji na vyakula jamii ya mbogamboga kama hutakuwa umesafisha vizuri.

Dalili za ugonjwa ni pamoja na tumbo kujaa na kukata kwa vipindi fulani, mtu akienda kujisaidia mara nyingi huishia kujikamua sana na akipata choo huwa hajisikii kumaliza.

Hizo ni baadhi ya dalili ila zipo nyingi lakini usitumie dawa mpaka utakapogundua kwa kupima kwani dawa nzuri inanywewa pale mtu anapogundua ana tatizo gani.


Tiba asilia ya Amoeba

Majani ya mpera


Tiba asilia inayotumika kumaliza kabisa tatizo hili ni pamoja na majani ya mpera, unayachukua na kuyakamua kwenye maji masafi ya kunywa ukiwa umeshayaosha vizuri kisha unakunywa nusu kikombe kwa siku mara tatu kwa siku tatu mfululizo.

Kitunguu swaumu

Chukua kitunguu swaumu punje tano menya kisha viweke ndani ya nusu lita ya maji safi na salama, changanya na maji ya limao moja chemsha mpaka maji yapungue, usisahau kuweka chumvi kidogo kwa ajili ya kupata ladha.

Ukishatengeneza kinywaji hicho unaweza kunywa kila siku glasi moja.
Ni tiba nzuri isiyo na madhara kwa mgonjwa.
 
Mimi ninayojua na nilituamia, ni asali robo, kitunguu swaumuu, kama 2 vikubwa, tangawizi 3 kubwa, mbegu za mpapai zilizokaushwa. Unatwangaa kitunguu, tangawizi, na mbegu za mpapai vinalainika. Unaweka kwenye asali, unaongezea maji la limao kama vijiko viwili vikubwa. Unaweka mahala penye giza kwa siku 3. Unaanza kunywa kijiko kidogo asubuhi na jioni. Kwa sababu vinakua vimeshikana inabidi utumie kijiko kukandamiza ili upate majimaji. Mi nina 17years now tangu niitumie na sijapata tatizo tena na amoeba
 
View attachment 538266
WATU wengi wamekuwa wakisumbuliwa na ugonjwa wa Amoeba lakini hupuuzia pale dalili zinapoanza, ni ugonjwa mbaya ambao ukikaa sana tumboni husababisha madhara makubwa , kama kuhara damu kupindukia, kutapika, kusikia kizunguzungu, kukosa hamu ya kula na kupata homa kali.

Ugonjwa huu mara nyingi husababishwa na maji na vyakula jamii ya mbogamboga kama hutakuwa umesafisha vizuri.

Dalili za ugonjwa ni pamoja na tumbo kujaa na kukata kwa vipindi fulani, mtu akienda kujisaidia mara nyingi huishia kujikamua sana na akipata choo huwa hajisikii kumaliza.

Hizo ni baadhi ya dalili ila zipo nyingi lakini usitumie dawa mpaka utakapogundua kwa kupima kwani dawa nzuri inanywewa pale mtu anapogundua ana tatizo gani.


Tiba asilia ya Amoeba

Majani ya mpera


Tiba asilia inayotumika kumaliza kabisa tatizo hili ni pamoja na majani ya mpera, unayachukua na kuyakamua kwenye maji masafi ya kunywa ukiwa umeshayaosha vizuri kisha unakunywa nusu kikombe kwa siku mara tatu kwa siku tatu mfululizo.

Kitunguu swaumu

Chukua kitunguu swaumu punje tano menya kisha viweke ndani ya nusu lita ya maji safi na salama, changanya na maji ya limao moja chemsha mpaka maji yapungue, usisahau kuweka chumvi kidogo kwa ajili ya kupata ladha.

Ukishatengeneza kinywaji hicho unaweza kunywa kila siku glasi moja.
Ni tiba nzuri isiyo na madhara kwa mgonjwa.
Asante. Naomba kuuliza je haya majani ya mpera kwa kuyakamua na mikono dawa inaweza kutoka vizuri au lazima yatwangwe kwenye kinu?

Dawa ni 2 ya vitunguu swaumu ,unaitumia kwa wakati mmoja na ike ya mpera au unatumia moja wapi?

Naomba jibu mkuu.asante
 
Back
Top Bottom