Amakweli Yanga imechagua wahuni kuongoza, Yanga ya sasa imevamia na wahuni ambao wanaharibu jina zuri la klabu yetu, Jana nilijivinjari uwanja wa Mkwakwani Tanga, nilishuhudia timu yangu ya Yanga ikitoka sare na Azam FC.
Baada ya Mchezo kuisha Davis Mosha alienda upande ambao Azam FC walikuwa wamekaa, akamuuliza kijana mmoja ambaye sijamtambua jina lake, "Na wewe Azam FC siku Hizi?" yule kijana akajibu mimi napenda mpira siyo sifa na Azam FC ndiko kwenye mpira wa kweli. Jibu lile lilimuudhi Mosha na kama mtu aliyepagawa akaanza kushusha makonde na Matusi kwa yule kijana
Watu walioshuhudia tukio lile wakapigwa na Butwaa, iweje kiongozi wa Hadhi ya Mosha apigane hadharani? pia wakajiuliza, hivi Mosha ana akili sawasawa?
Jamaa mmoja pale uwanjani akasema, eti hata kule kupigwa kwa Ndimbo na Mtawale wakihusishwa na imani za kishirikina Mwanza kulishawishiwa na Mosha, Alikuwa ni mosha aliyewachochea mashabiki wa Yanga wawapige akina Ndimbo halafu Mosha akakimbilia kupiga simu vituo Vya Redio kutangaza lile tukio.
Kifupi Mosha ni Mchochezi, Mzushi, Mhuni, na Mwehu, haiwezekani klabu kubwa kama Yanga kuongozwa na Mtu mwenye Tabia za Mosha kwani ipo siku atasababisha maafa kwa kuwachochea Yanga kufanya Fujo viwanjani
MOSHA JIREKEBISHE
Baada ya Mchezo kuisha Davis Mosha alienda upande ambao Azam FC walikuwa wamekaa, akamuuliza kijana mmoja ambaye sijamtambua jina lake, "Na wewe Azam FC siku Hizi?" yule kijana akajibu mimi napenda mpira siyo sifa na Azam FC ndiko kwenye mpira wa kweli. Jibu lile lilimuudhi Mosha na kama mtu aliyepagawa akaanza kushusha makonde na Matusi kwa yule kijana
Watu walioshuhudia tukio lile wakapigwa na Butwaa, iweje kiongozi wa Hadhi ya Mosha apigane hadharani? pia wakajiuliza, hivi Mosha ana akili sawasawa?
Jamaa mmoja pale uwanjani akasema, eti hata kule kupigwa kwa Ndimbo na Mtawale wakihusishwa na imani za kishirikina Mwanza kulishawishiwa na Mosha, Alikuwa ni mosha aliyewachochea mashabiki wa Yanga wawapige akina Ndimbo halafu Mosha akakimbilia kupiga simu vituo Vya Redio kutangaza lile tukio.
Kifupi Mosha ni Mchochezi, Mzushi, Mhuni, na Mwehu, haiwezekani klabu kubwa kama Yanga kuongozwa na Mtu mwenye Tabia za Mosha kwani ipo siku atasababisha maafa kwa kuwachochea Yanga kufanya Fujo viwanjani
MOSHA JIREKEBISHE