Dar Village Project in Dar es Salaam

be caferul of what you wish for au ndio unataka kuprovoke watu wamweke wazi huyu ZADOCK kisha uje kulalama kuwa ohhh mmekuwa personal..?

hiyo ya pesa za TIB mbona hujaligusa?
hii thread umeanzisha wewe mkuu sasa tupe na wengine fursa ya kuchangia mazuri na mabaya na wala usiweke vitisho maana haisaidii, au tukuachie wewe uchangie TU!
 
hii thread umeanzisha wewe mkuu sasa tupe na wengine fursa ya kuchangia mazuri na mabaya na wala usiweke vitisho maana haisaidii, au tukuachie wewe uchangie TU!
unaposema niwe careful katika what i wish for una maana gani? sina ninalo wish for mkuu, nimetumia uhuru wangu kuchangia kama wengine, na wala sitazuia watu kumweka wazi kwanza mimi nani mpaka nizuie.

tena nitashukuru sana kufahamu zaidi maana huenda ninachofahamu ni kidogo so please nifahamishe zaidi kuhusu TIB...
 
Nasikia jamaa hana pesa na mabenki yamemuona hakopesheki. Sasa hivi anaishi South Africa na hapo dar Village hakuna cha maana kinachoendelea.
 
Nyambele! Nakushukuru!!

Utadhani tuko pamoja. Huyo Zadock kafikia alikofikia!! Wanasema ulichokiacha pwani kakingojee ufukweni?Ukimwona kijana wa kichaga anakimbia Dar akaishi bondeni ambako usalama uko tete ujue kuna kasoro!! Let us wait and see!!
 
Kwani ukianza project kama hizi sio kwamba unakuwa una secure funding kwanza? Au ndo mambo ya kujenga ground floor then kupangisha watu ili umalizie floor zengine?
Na hakopesheki kivipi?
Kwani mabenki hawaoni kuwa ikikamilika hela zitaanza kuingia?
Something strange is going on here!
 
hata mimi hilo limenishtua, nakwenda movie pale karibu kila friday na sijawahi kuona umeme ukikatika...hata panya sijawahi kuona.Labda time ninazoenda mimi huwa panya wamelala, na jamaa wa Tanesco wanaokata umeme nao wanakuwa movie.

Swala la PANYA ni la kweli tena wakubwa kama paka.
Wapo tele pale kwani mlo wa kumwaga kuanzia bisi mpaka malala nje ya shoprite.
 
kwa jamaa zadock kuna jambo la kujifunza jamani,ukifanya biashara au maissue yako yote then ukakamata hela nyingi please usifuje!hakuna kitu hela nyingi ntatumia hii kwani itaisha,afterall naingiza kibao!sasa jamaa lifestyle yake imemwangusha,jeuri kuwa anazo,haambiliki hasikii la ushauri.kuingilia mradi ambao alijua kuwa utamaishia njiani!ok hata aingie ubia na wenye nazo,mh noop huo uwezo hana kuingia mikataba mikubwa! sory for him!!
 
GT
Kuhusu trafic umesema kweli
Nafikiri itakuwa shida kubwa once hicho kijiji kikianza kazi, manake hivi sasa tu barabara zote za H.Mwinyi na ile Old Bagamoyo (nafikiri bado inaitwa hivyo) kipindi nipo dar kulikuwa na trafic ya kutisha asubuhi na jioni, sasa jaribu kufikiria msongamano wa magari kipindi kijiji kikifunguliwa! Sijaona planning yao hao jamaa na jinsi watakavo lilitaua hili suala, labda wanazo solution tayari! Ila kwa ujumla mipango miji sisi ovyo!
 
kwa jamaa zadock kuna jambo la kujifunza jamani,ukifanya biashara au maissue yako yote then ukakamata hela nyingi please usifuje!hakuna kitu hela nyingi ntatumia hii kwani itaisha,afterall naingiza kibao!sasa jamaa lifestyle yake imemwangusha,jeuri kuwa anazo,haambiliki hasikii la ushauri.kuingilia mradi ambao alijua kuwa utamaishia njiani!ok hata aingie ubia na wenye nazo,mh noop huo uwezo hana kuingia mikataba mikubwa! sory for him!!

utajifunza nini nawakati ujui ukweli, una speculate tuu kilichotokea....
bank kibao zime stop lending na miradi kibao duniani ipo katikati imesimama, dar village is no difference
 
jumuia ya kiislam itakuja na jambo gani hapo ebuu tutoe tongotongo mkuu Solomon David
 
dar+village+2.jpg



Of course kila mtu anajua kuwa kulitokea uhuni wao kupata ile sehemu na nashangaaa kwa nini wasingepewa maeneo kama kule Pugu wakaweza investment kubwa kama ile...wangejenga retail park nzuri na ardhi kubwa lakini wajanja na mafisadi kule serikalini wakaamua kuinyanganya serikali kiwanja na bila aibu viongozi wakuu serikalini washapalekwa pale kama kuendorse hiyo project

Haya tukubali ndio washaiba, mbona hawa jamaa hawamalizi huo ujenzi tujue moja? Maana bila kukuongopea wale wanaojenga/waliojenga kule milimani City naona walichukua ramani za shule na designs za correctional facilities za ulaya wakaenda kuzipeleka pale na lile jumba a cinema kila wakati umeme unakatika...bila kusahau Panya ambao nishawaona pale

who knows maybe Dar Village might bring vibe tofauti mjini lakini sijui waliotoa vibali kujenga pale kama walizingatia traffic kubwa itakayokwenda pale maana sisi pia ni ovyo kwenye hilo la traffic management


GT

Kuhusu designs za Mlimani City, umepata wapi habari kwamba "walichukua ramani za shule na designs za correctional facilities za ulaya.."? Tuambie mkuu.

Kuhusu jumba la sinema, si kweli kwamba kila mara umeme unakatika, na kwamba kuna panya pale. Nimeshakwenda kucheki movie pale, hata siku moja sijashuhudia umeme ukikatika pale... ukiingia ndani mule, A/C full Mufindi... kama hujavaa vizuri utajikunyata kwa baridi. Kama umetumwa kuwachafulia, sema....

Kuhusu Dar Village, bado natazama nione kitakachoendelea, lakini Serikali waliamua kuuza mali za Shirika la Posta na Simu (baadaye TTCL na TPC) wakati walipoamua kurekebisha mfumo wa mashirika yale. Nitalalamika iwapo taratibu za uuzaji wa mali hizo zilikiukwa, lakini kwa kuwa nimewafahamu baadhi ya wamiliki wa eneo hilo, sina budi kuwa na shaka jinsi walivyonunua sehemu hiyo. Hata hivyo, si lazima wapewe Pugu (sasa Nyerere) Road, kwani, eneo hilo si "commercial" park, ni "industrial" park. Usijichanganye mkuu! (LOL)

./Mwana wa Haki
 
Kwakweli wote hatujui kinachoendelea mule.

Mipango miji ZERRROOOOOOOOOOOOOOOO. Yaani hata hawakuwaza Traffic jam??!!!!
 
Mimi nimeenda jana pale Century Cinemax, Mlimani City na nimeona panya kibao! Nayo si mara ya kwanza kuwaona. Pia kule Shoprite ndani nimeshawaona mara mbili wanakatisha. Wakubwa kinoma. Umeme pia niliwahi kushuhudia ukikatika na haukurudi hadi ikabidi waturudishie hela yetu. Genereta lilikuwa halina mafuta na mtu aliyetumwa kununua baada ya umeme kukatika alichelewa.
 
Wewe GT nawe na sinema tuu....umesahau kuwa hata mlimani city ililala miaka mbili...hawa jamaa hawajengi kwa keshi....
 
Kwani nyie hamko TZ au ndo kusema ?mnajua fika TZ kuna mgao,pia acheni kujishaua eti jengo sijui ni kama sijui magereza ya ulaya ah jamani mnataka ma sky nini au ndo kasumba ya kubeba box imewajaa hata huko mamtoni kuna mijipanya
 
Haters wa maendeleo ya watanzania ni watanzania..sasa mlitaka hako ka-business kawe owened na mzungu..gosh! amejaribu tumpe moyo na tumpe alternative ya kujenga zaidi ala
 
Haters wa maendeleo ya watanzania ni watanzania..sasa mlitaka hako ka-business kawe owened na mzungu..gosh! amejaribu tumpe moyo na tumpe alternative ya kujenga zaidi ala

Labda wanataka mwekezaji mwarabu... u never know
 
Back
Top Bottom