Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,989
Mtuhumiwa Baraka Benedicto ambaye kabla ya kutiwa mbaroni alikuwa mlinzi katika Kanisa Katoliki la Sinza, Parokia ya Bikira Maria Mama Mwokozi-Sinza, amepandishwa kizimbani kwenye Mahakama ya Mwanzo Wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam na kusomewa shtaka moja la kumuingilia mtoto kinyume na maumbile.
Shtaka hilo limesomwa na Wakili wa Serikali mbele ya Hakimu Ramadhani Rugemarila ikielezwa kuwa mtuhumiwa anadaiwa kutenda tukio hilo Februari 3, 2024, mtuhumiwa amekana shtaka hilo.
Kufuatia hatua hiyo Mahakama imepanga kusikiliza tena shauri hilo Namba CC.5866, Jumatatu Machi 18, 2024 Saa tatu asubuhi ambapo mtuhumiwa amepelekwa rumande Segerea.
Baraka Benedicto anadaiwa kumuingilia mtoto wa kiume anayesoma Darasa la Tano katika moja ya Shule iliyopo Sinza, Dar, kinyume na maumbile "ulawiti" katika vyoo vya Parokia Bikira Maria Mama mwokozi - Sinza, ambapo awali ilidaiwa kuwa alikuwa nje kwa dhamana.
Hatua ya kufikishwa mahakamani kwa mtuhumiwa umefanyika siku moja baada JamiiForums kuripoti madai hayo ambayo yaliibuliwa na mdau kwenye jukwaa huru la maoni na mijadala.
Soma:
-Madai ya Mlinzi wa Kanisa Katoliki Sinza kumlawiti Mwanafunzi, mama wa Mtoto aomba Serikali imsaidie
- Tukio la Mlinzi wa Kanisa Katoliki Sinza kudaiwa kumlawiti Mwanafunzi, Padri asimulia kilichotokea
Shtaka hilo limesomwa na Wakili wa Serikali mbele ya Hakimu Ramadhani Rugemarila ikielezwa kuwa mtuhumiwa anadaiwa kutenda tukio hilo Februari 3, 2024, mtuhumiwa amekana shtaka hilo.
Kufuatia hatua hiyo Mahakama imepanga kusikiliza tena shauri hilo Namba CC.5866, Jumatatu Machi 18, 2024 Saa tatu asubuhi ambapo mtuhumiwa amepelekwa rumande Segerea.
Baraka Benedicto anadaiwa kumuingilia mtoto wa kiume anayesoma Darasa la Tano katika moja ya Shule iliyopo Sinza, Dar, kinyume na maumbile "ulawiti" katika vyoo vya Parokia Bikira Maria Mama mwokozi - Sinza, ambapo awali ilidaiwa kuwa alikuwa nje kwa dhamana.
Hatua ya kufikishwa mahakamani kwa mtuhumiwa umefanyika siku moja baada JamiiForums kuripoti madai hayo ambayo yaliibuliwa na mdau kwenye jukwaa huru la maoni na mijadala.
-Madai ya Mlinzi wa Kanisa Katoliki Sinza kumlawiti Mwanafunzi, mama wa Mtoto aomba Serikali imsaidie
- Tukio la Mlinzi wa Kanisa Katoliki Sinza kudaiwa kumlawiti Mwanafunzi, Padri asimulia kilichotokea