LD
JF-Expert Member
- Aug 19, 2010
- 3,014
- 578
Niko kwenye daladala natokea kwenye pilikapilika za kutafuta mkate wa kila siku.
Pembeni yangu kakaa mama mmoja anayeonekana katoka kutafuta mkate na yeye. Mama huyu amechoka, anaonekana pia hana furaha ya kutosha. Mara amefungua mfuko wake katoa mboga za majani anaanza kuchambua. Dah nkimwambia mama umeona urahisishe mambo eeh! Akanijibu kwa upole acha tu dada angu, maisha haya. Tunavyohangaika hata muda hautoshi.
Mama huyo hapo ukute watoto wamekaa mlangoni wanasubiri mama arudi.
Pembeni yangu kakaa mama mmoja anayeonekana katoka kutafuta mkate na yeye. Mama huyu amechoka, anaonekana pia hana furaha ya kutosha. Mara amefungua mfuko wake katoa mboga za majani anaanza kuchambua. Dah nkimwambia mama umeona urahisishe mambo eeh! Akanijibu kwa upole acha tu dada angu, maisha haya. Tunavyohangaika hata muda hautoshi.
Mama huyo hapo ukute watoto wamekaa mlangoni wanasubiri mama arudi.