Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 40,000
Kipimo mwatupimia,
Mwajua twapungukia,
Lakini mwasubiria
Kuona tutapatia;
Sifa mnatutajia,
Za yule mwatamania,
Kila tukiangalia,
Vijana tumefulia,
Twabaki twatamania,
Kama sungura wa hadithia,
Ya ndizi alizochukia,
Kwa kukosa kufikia,
Nguo tunazovalia,
Kamwe hatujapatia,
Haraka mwatuambia,
Ni vipi tungevalia,
Nywele tulivyochania,
Manukato mwachukia,
Viatu mwaangalia,
Na tai mwaivutia,
Kama kisu mwakatia,
Mitima mwaivunjia,
Na hata mkipatia,
Hasira twajisikia,
Tunda twalitamania,
Na penzi twarajia,
Donge limetushikia,
Kisu twakiruhusia,
Wachache wanapatia,
Kwa upole watwambia,
Bila ya kukejelia,
Na dharau kumwagia
Ya'raabi katujalia,
Shukuru twashukuria,
Bila nyinyi twaumia,
Kizani twajikutia,
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Mwajua twapungukia,
Lakini mwasubiria
Kuona tutapatia;
Sifa mnatutajia,
Za yule mwatamania,
Kila tukiangalia,
Vijana tumefulia,
Twabaki twatamania,
Kama sungura wa hadithia,
Ya ndizi alizochukia,
Kwa kukosa kufikia,
Nguo tunazovalia,
Kamwe hatujapatia,
Haraka mwatuambia,
Ni vipi tungevalia,
Nywele tulivyochania,
Manukato mwachukia,
Viatu mwaangalia,
Na tai mwaivutia,
Kama kisu mwakatia,
Mitima mwaivunjia,
Na hata mkipatia,
Hasira twajisikia,
Tunda twalitamania,
Na penzi twarajia,
Donge limetushikia,
Kisu twakiruhusia,
Wachache wanapatia,
Kwa upole watwambia,
Bila ya kukejelia,
Na dharau kumwagia
Ya'raabi katujalia,
Shukuru twashukuria,
Bila nyinyi twaumia,
Kizani twajikutia,
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)