Lutala
JF-Expert Member
- Jun 17, 2010
- 848
- 103
Wana JF
Huyu ni mama wa 2 kids
Mtoto wa kwanza alimzaa na mwanaume mwingine miaka 6 iliyopita ,yalitokea matatizo hawakuweza kuwa an uhusiano na huyu baba wa mtoto na akawa ameoa,Ila katika kipindi chote hicho Baba wa mtoto hakuwahi kuwasiliana na huyu dada wala kutoa matumizi ya mtoto wala kukumbuka kama aliwahi kuzaa dada alisononeka mpaka akazoea
Mungu si Athuman huyu dada nae akapata mwenza na akafunga ndoa mwaka jana.wanaishi na mmewe kwa amani na upendo na mungu kamjalia mtoto mwingine ana 6 month sasa.
Tatizo limeanza baada ya huyu mzazi mwenzie kufukuzwa kazi ,pia biashara zake zimefirisika sasa hana kitu kabisa amerudi kwa mama mtoto wake huyu na anabembeleza asaidiwe angalau aanze tena maisha na ameanza kumlaumu eti ajaribu kukumbuka fadhira alizomfanyia kipindi walipokuwa B/F na G/F na anaomba asahau tofauti zao
Mbaya zaidi huyu Baba mtoto wake kaanza kupiga simu na kutuma msg za malalamiko mpaka usiku wa Manane
Huyu dada ana hofu kama mmewe akijua kinachoendelea ndoa yake iko matatani ,kamuelewesha huyo baba wa mtoto wake lakini inaelekea haelewi na amekuwa kinganganizi
Anajiuliza amwambie mmewe au afanyeje maana jamaa haachi usumbufu
Kila anapojisikia anapiga simu na kutuma msg .
Pls msaada wenu kimawazo kwa dada huyu
Hayo ndo matatizo ya stori za kutunga. Unajiua kutokuwa na mahusiano wa miaka 6 si mchezo. Haiwezekani kuwa huyo mume aliyefunga naye ndoa halijui suala hilo kwa kluwa mtoto wa jamaa si anamfahamu. Haiwezekani jamaa wa zamani afosi king namna hiyo kama hakuna kingine zaidi ya hivyo ulivyoandika hapo. Ushauri: Cha msingi huyo dada amshitaki huyo jamaa kwa kumbugudhi katika maisha yake