Albert Msando
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 1,019
- 171
CUF ni wanafiki sana. sana.
Unafiki wao unajionyesha wazi kwa jinsi walivyowasahaulifu na wepesi kujitetea ili mradi waonekane wao ndio wao. Wanajiaminisha kwamba CHADEMA wanawachukia au wanawaonea wivu.
Wanasahau kwamba "Masikini hafilisiki" na "KICHAA HACHANGANYIKIWI"
CUF wameumia sana CDM wamekataa kuingia kwenye mtego wao na CCM. Inaendelea kuwauma na kutuliza roho zao wameamua kuwarushia makombora CDM.
Viongozi wa CUF wanajificha nyuma ya pazia jepesi la 'sauti ya wazanzibari'. Tunajua wazanzibari ni kina nani. Tunajua ni asilimia ngapi ya dini gani inaunda sauti ya wazanzibari. Hivyo kwa kujificha nyuma ya sauti hiyo CUF wanategemea CHADEMA wataumia kwa kuhukumiwa na baadhi ya watu wa dini fulani.
CUF wanasahau kwamba kura zilizopigwa Zanzibar kuhusu serikali ya 'umoja' wa kitaifa haikuwa kwa aina yoyote inayofanana na kura iliyopigwa sudan kusema kwamba asilimia 99 wamekubali. Kuna waliopinga na bado wanapinga. Kwani hao sio wazanzibari??
Kama kigezo ni vifo vya wanaCUF kuunda serikali wao na CCM peke yao na kusema kwamba vyama vingine havina wabunge je walivishirikisha hata kupata mawazo yao kuhusu umoja wao na CCM? waliwaeleza nii kwa nini kwao ni muhimu kuungana na CCM ilihali vyama vingine vitabaki nje ya serikali hiyo ya umoja wa kitaifa?
CUF kama wangekuwa wamefanya hivyo basi wangewalaumu CDM kwa kutokuwaelewa. Hawakuwahi kuwashirikisha wengine kuhusu Zanzibar. Vikao vyote vilikuwa kati ya Katibu Mkuu wao na CCM!! Mbona hawakutaka kushirikiana katika hilo?
Sasa wanaanza maneno, CDM wamelewa madaraka. Madaraka yapi? CDM ni wasaliti, wamemsaliti nani? Mbatia? Mrema? Lipumba?
Turudi kwenye ukweliushirikiano wa wapinzani bungeni ni nini? Wanashirikiana ili iweje?
Tukumbuke, CDM walitoka bungeni, hatuhitaji kujua ilikuwa ni sawa au si sawa lakini vyama vilivyobaki haraka haraka vilienda kukaa kwenye viti walivyotoka wabunge wa CDM. Baada ya hapo CCM wakashangilia.
Huo ni unafiki. Ni lini CUF na hivyo vyama vingine waliomba msamaha au walielezea sababu za kuwadhalilisha CHADEMA ili wananchi waelewe?
Hilo hawalioni badala yake wanataka ushirikiano kwenye bunge lile lile!! Ushirikiano kwa sababu wenye viti vyao wamerudi??
CHADEMA hakuna kushirikiana na CUF na wanaofuta mpaka pale wote watakapokuwa wamejifunza kwamba ushirikiano ni wa vitendo na si wa maneno tu. Haiwezekani utake uwaziri kamili, uone hautoshi ung'ang'anie uwaziri kivuri. Kwani kushirikiana mpaka upewe cheo?
Kwa nini basi kama ni muhimu kiasi hicho CUF na CDM wasiungane na kuwa chama kimoja?
CUF na vyama vingine lazima waonyeshe kwa vitendo kuipinga serikali ya CCM. Wao wanakuja na approach "if you cant fight them join them'
CHADEMA approach yake ni "if you cant fight them, fight them' sasa hiyo ni approach tofauti na ya CUF.
Mwisho, tunataka tuone matunda ya muungano wa CUF na CCM zanzibar baada ya miaka mitano. Kama hali ya maisha ya wazanzibari itakuwa imebadilika CDM wataomba msamaha na watajirudi kwa kukataa kujiunga na CUF. Na CUF watafanya hivyo hivyo endapo hali itakuwa haijabadilika.
Pia tutaona bunge linalokuja kwamba kutokuungana na CUF na vyama vingine kutakuwa na athari gani kwa taifa.
Kwa sasa hivi msimamo wa CDM ni kwamba CUF na vyama vingine rafiki kwa CCM waendelee na urafiki wao. CDM itabaki chama kinachoipinga CCM kwa vitendo na kitaendelea kuchukua maamuzi magumu na yasiyowafurahisha CUF lakini ukweli utasimama.
CDM haikuungana CCM Kigoma. CUF waache uongo na uzushi! CDM na CCM walikubaliana kuachiana madaraka baada ya kuwa wamefungana katika idadi ya wajumbe. Hiyo ilikuwa ni kwa faida ya watu wa kigoma. Sio kwamba CDM walishindwa basi wakapewa kipoozeo kama walivyofanyiwa CUF zanzibar.
Narudia, masikini hawezi kufilisika, na kichaa hawezi kuchanganyikiwa!!:msela:
Unafiki wao unajionyesha wazi kwa jinsi walivyowasahaulifu na wepesi kujitetea ili mradi waonekane wao ndio wao. Wanajiaminisha kwamba CHADEMA wanawachukia au wanawaonea wivu.
Wanasahau kwamba "Masikini hafilisiki" na "KICHAA HACHANGANYIKIWI"
CUF wameumia sana CDM wamekataa kuingia kwenye mtego wao na CCM. Inaendelea kuwauma na kutuliza roho zao wameamua kuwarushia makombora CDM.
Viongozi wa CUF wanajificha nyuma ya pazia jepesi la 'sauti ya wazanzibari'. Tunajua wazanzibari ni kina nani. Tunajua ni asilimia ngapi ya dini gani inaunda sauti ya wazanzibari. Hivyo kwa kujificha nyuma ya sauti hiyo CUF wanategemea CHADEMA wataumia kwa kuhukumiwa na baadhi ya watu wa dini fulani.
CUF wanasahau kwamba kura zilizopigwa Zanzibar kuhusu serikali ya 'umoja' wa kitaifa haikuwa kwa aina yoyote inayofanana na kura iliyopigwa sudan kusema kwamba asilimia 99 wamekubali. Kuna waliopinga na bado wanapinga. Kwani hao sio wazanzibari??
Kama kigezo ni vifo vya wanaCUF kuunda serikali wao na CCM peke yao na kusema kwamba vyama vingine havina wabunge je walivishirikisha hata kupata mawazo yao kuhusu umoja wao na CCM? waliwaeleza nii kwa nini kwao ni muhimu kuungana na CCM ilihali vyama vingine vitabaki nje ya serikali hiyo ya umoja wa kitaifa?
CUF kama wangekuwa wamefanya hivyo basi wangewalaumu CDM kwa kutokuwaelewa. Hawakuwahi kuwashirikisha wengine kuhusu Zanzibar. Vikao vyote vilikuwa kati ya Katibu Mkuu wao na CCM!! Mbona hawakutaka kushirikiana katika hilo?
Sasa wanaanza maneno, CDM wamelewa madaraka. Madaraka yapi? CDM ni wasaliti, wamemsaliti nani? Mbatia? Mrema? Lipumba?
Turudi kwenye ukweliushirikiano wa wapinzani bungeni ni nini? Wanashirikiana ili iweje?
Tukumbuke, CDM walitoka bungeni, hatuhitaji kujua ilikuwa ni sawa au si sawa lakini vyama vilivyobaki haraka haraka vilienda kukaa kwenye viti walivyotoka wabunge wa CDM. Baada ya hapo CCM wakashangilia.
Huo ni unafiki. Ni lini CUF na hivyo vyama vingine waliomba msamaha au walielezea sababu za kuwadhalilisha CHADEMA ili wananchi waelewe?
Hilo hawalioni badala yake wanataka ushirikiano kwenye bunge lile lile!! Ushirikiano kwa sababu wenye viti vyao wamerudi??
CHADEMA hakuna kushirikiana na CUF na wanaofuta mpaka pale wote watakapokuwa wamejifunza kwamba ushirikiano ni wa vitendo na si wa maneno tu. Haiwezekani utake uwaziri kamili, uone hautoshi ung'ang'anie uwaziri kivuri. Kwani kushirikiana mpaka upewe cheo?
Kwa nini basi kama ni muhimu kiasi hicho CUF na CDM wasiungane na kuwa chama kimoja?
CUF na vyama vingine lazima waonyeshe kwa vitendo kuipinga serikali ya CCM. Wao wanakuja na approach "if you cant fight them join them'
CHADEMA approach yake ni "if you cant fight them, fight them' sasa hiyo ni approach tofauti na ya CUF.
Mwisho, tunataka tuone matunda ya muungano wa CUF na CCM zanzibar baada ya miaka mitano. Kama hali ya maisha ya wazanzibari itakuwa imebadilika CDM wataomba msamaha na watajirudi kwa kukataa kujiunga na CUF. Na CUF watafanya hivyo hivyo endapo hali itakuwa haijabadilika.
Pia tutaona bunge linalokuja kwamba kutokuungana na CUF na vyama vingine kutakuwa na athari gani kwa taifa.
Kwa sasa hivi msimamo wa CDM ni kwamba CUF na vyama vingine rafiki kwa CCM waendelee na urafiki wao. CDM itabaki chama kinachoipinga CCM kwa vitendo na kitaendelea kuchukua maamuzi magumu na yasiyowafurahisha CUF lakini ukweli utasimama.
CDM haikuungana CCM Kigoma. CUF waache uongo na uzushi! CDM na CCM walikubaliana kuachiana madaraka baada ya kuwa wamefungana katika idadi ya wajumbe. Hiyo ilikuwa ni kwa faida ya watu wa kigoma. Sio kwamba CDM walishindwa basi wakapewa kipoozeo kama walivyofanyiwa CUF zanzibar.
Narudia, masikini hawezi kufilisika, na kichaa hawezi kuchanganyikiwa!!:msela: