hawa ni wazee wa kucopy na na kupaste wanasubiri wengine waanze.
Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
Kuna tetesi kesho CUF watatoa tamko kuhusu kukamatwa kwa shekh ponda, ktk mkutano wa Buguruni,.........na kutoa njia ya ufumbuzi wa tatizo.
NA hili lilikua nini?
Chama cha Wananchi CUF kinasikitishwa na matukio ambayo hayakutarajiwa kutokea hapa Zanzibar yaliyoanza kujitokeza jana tarehe 17/10/2012 ambayo yamesababisha vurugu kubwa katika Manispaa ya Zanzibar na vitongoji vyake.
Matukio hayo yamesababisha uharibifu mkubwa wa mali za Umma, wananchi mmoja mmoja na hata vyama vya siasa. Miongoni mwa vitendo hivyo ni kuvunjwa Maduka, vyombo vya usafiri, kukatwa miti ovyo na nguzo za umeme, pamoja na kuchomwa moto maskani za CCM. Matukio mengine ya kusikitisha na kuhuzunisha kufuatia vurugu hizo ni kuwepo taarifa za kuuwawa kwa Askari Polisi.
Kutokana na vitendo hivyo, Chama Cha wananchi CUF kinaalaani kwa nguvu zote matukio hayo ambayo yamepelekea uvunjifu wa mkubwa wa amani ya nchi, na kusababisha hofu kubwa kwa raia pamoja na wageni wanaotembelea Zanzibar.
Sambamba na vurugu hizo, Chama Cha Wananchi CUF kimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar iliyotolewa na Waziri wa Nchi Afisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mhe. Mohammed Aboud Mohammed iliyoeleza juu ya kutoweka kwa Sheikh Farid Hadi Ahmed katika mazingira ya kutatanisha.
Katika Taarifa hiyo, Serikali imethibitisha kuwa vyombo vyake vyote vya ulinzi havijamkamata Sheikh Farid, jambo ambalo limezidisha hofu na wasi wasi kwa wananchi juu ya mahali alipo na hali yake kiongozi huyo wa Jumuiya ya Maimamu Zanzibar.
Chama cha Wananchi CUF kinaiomba Serikali kuendeleza juhudi zote za kuhakikisha taarifa za ukweli na za uhakika zinapatikana juu ya kadhia ya kutoweka kwa Sheikh huyo kwani Sheikh Farid ni raia wa nchi hii, na Serikali hii ni kwajili ya wananchi wote, ili kuondoa hofu na wasi wasi ambao umesababisha baadhi ya wananchi kujengwa na dhana mbaya.
Aidha, Chama cha wananchi CUF kinawataka wanachama wake, wapenzi na wananchi wote kwa ujumla kutojiingiza na kutofanya vitendo vyovyote vinavyoweza kupelekea uvunjifu wa amani ya nchi yetu.
Sote kwa pamoja tukatae kabisa kujihusisha na vitendo vya kuleta vurugu kwa vitendo na kauli zitakazopelekea kuiondolea sifa njema nchi hii ya Zanzibar ambayo imejijengea duniani kote.
Haki sawa kwa Wote
..
Salim Biman
Kaimu Naibu katibu Mkuu Zanzibar
Cuf MNAWEZA KUSOMA HII NAYO KUWEKA MSIMAMO JUU YA BAKWATA NA KUMTAKA KIKWETE ALIVUNJEKuna tetesi kesho CUF watatoa tamko kuhusu kukamatwa kwa shekh ponda, ktk mkutano wa Buguruni,.........na kutoa njia ya ufumbuzi wa tatizo.
Cuf MNAWEZA KUSOMA HII NAYO KUWEKA MSIMAMO JUU YA BAKWATA NA KUMTAKA KIKWETE ALIVUNJE
NINI CHA KUFANYA ?
Napenda kutoa ushauri kwa Rais Kikwete kutumia busara na kulivunja BAKWATA mara moja.
Utaona bakwata wali rithishwa mali zote ya iliyokuwa jumuia ya waislam enzi hizo kazi yao kubwa ni kuziuza hizo mali na viwanja.
Livunje hili baraza na badala yake haraka uunde kamati ya muda ambayo itatoka kutoka madhebu yote ya waislam tanzania.Kumbuka Bakwata ndio baraza linalo tambuliwa na serikali kuhusu mambo yote ya waislamu.
.
kwa ufupi katiba ya bakwata ilifanyiwa mabadiliko chini ya mrema wakati ule akiwa ccm na kuondoa kabisa uwezekano wa kuondolewa kwa kiongozi ama mufti wa bakwata hata kama atafanya ufisadi aina gani.macos, uongozi wa bakwata ulipatikanaje? Nani aliwachagua, na kama wanafanya kinyume na maslahi mapana ya waislam wengi hakuna namna yoyote ya kuwaondoa bila ya chombo cha nje kuingilia kati i.e rais kama ulivyoshauri?
I am curious to know, kama kuna katiba inayoongoza taasisi hii ya waislam na kama ipo inasemaje kuhusu uongozi/miiko? Na pia viongozi wa bakwata wakishachaguliwa wanakaa kwa muda gani?
kwa ufupi katiba ya bakwata ilifanyiwa mabadiliko chini ya mrema wakati ule akiwa ccm na kuondoa kabisa uwezekano wa kuondolewa kwa kiongozi ama mufti wa bakwata hata kama atafanya ufisadi aina gani.
Ku kawaida katiba hizi za asasi za kiraia lazima zipetishwe na wizara ya mamb yandani.. Na mrema aliris=dhia hili
pili uongozi wa bakwata hauchaguliwi na waislam ama maimam ama taasisi nyengine bali huchaguliwa na wajumbe wa bakwata kutoka kila mkoa amabo nao huwa wanateuliwa na mufti !!
Sasa utaona hili baraza halina sura ya kitaifa ya waislam...ni kikundi cha wachache lakini kinatambuliwa kama wasemaji wa wasilam wote
sio haki lazima hali hii irekebishwe...na kwa vile serikali ndio ilio pitisha katiba yao yenye ukiritimba ni wao peke yao wanao weza kulivunja
hakuna mabadiliko yaliyofanywa..alipo fariki mufti hemed bin jumaa kuna waislam wasomi walijitokeza kutaka kugombeahii ndiyo classic example ya 'zidumu fikra za ...". Kama ni nimekuelewa vizuri, ni sawa na wakuu wa mikoa -ambao huteuliwa na rais wawe ndio wanachagua serikali kuu including rais! Mental!
Na kuhusu katiba, are you saying tangu wakati wa mwinyi (mrema alikuwa ccm wakati wa mwinyi) bakwata hawajafanyia marekebisho ya katiba yao licha ya kelele za waumini wanaowaongoza? Is that possible?
watoe tamko kama chama au kama serikali...wananichanganya na hawa watu