Tumain
JF-Expert Member
- Jun 28, 2009
- 3,154
- 70
MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahimu Lipumba, amemtaka Rais Jakaya Kikwete kukaa kando ili kumaliza migongano yao ndani ya CCM na kumpisha kiongozi atakayestahili kuwa rais katika uchaguzi mkuu mwakani.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam wakati akitoa maazimio ya kikao cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la chama hicho, Lipumba alisema kutokana na kuwepo kwa makundi ndani ya CCM ndiyo sababu kubwa ya nchi kuwa na ombwe katika uongozi.
Rais akiwa kama ni Mwenyekiti wa CCM ambayo ndiyo inaongoza nchi kwa sasa, anatakiwa kukaa kando ili kuweza kumaliza makundi yao ndani ya chama na kuwapisha viongozi wengine wanaofaa, kuweza kushughulikia masuala ya maendeleo na kukuza uchumi nchini, alisema Profesa Lipumba.
Alisema wanachama wa CCM ambao wengi wao ni viongozi wa ngazi za juu, wamekuwa wakijihusisha na makundi, ugomvi na hata kurushiana maneno badala ya kukaa na kujadili njaa inayowakabili Watanzania wengi kwa sasa.
Baraza Kuu limesikitishwa na kitendo cha CCM kuacha kuwatumikia wananchi iliyowaahidi kuwaletea maisha bora kwa kila Mtanzania na badala yake kugeuka jukwaa la malumbano, mapambano, matusi na kashfa kati ya makundi yanayopigania vita vya kulipizana visasi vinavyotokana na kugombea maslahi binafsi, alisema Lipumba.
Aidha, baraza hilo pia lilimtaka rais kuacha kuchezea akili za Watanzania kwa kuendesha kesi za kisanii za ufisadi na badala yake kutoa maelezo na kuchukua hatua kuhusiana na kashfa nzito za Meremeta, Mwananchi Gold, Tan Gold, Richmond, fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), Kagoda Agriculture Limited ambazo Watanzania wanasubiri kuona hatua zake.
Baraza hilo pia liliitaka serikali kutekeleza kwa ukamilifu maazimio yote 23 ya Bunge kuhusu kashfa ya Richmond na kuwasilisha bungeni katika kikao cha kwanza mwakani.
Aidha Profesa Lipumba alisema wamesikitishwa na uzembe uliofanywa na serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini, ambao umesababisha kukosa umeme wa uhakika, jambo ambalo linazorotesha maendeleo ya kiuchumi. Ni aibu kwa serikali kutangaza kutekeleza mpango wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania (MKUKUTA), huku ikiendelea kushindwa kuja na mipango madhubuti itakayohakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika katika nchi, alisema Lipumba.
Source: Tanzania Daima
My take: Kama hana uwezo si asubiri 2010 ashinde kilaini kwanini anatafuta kushindani na mtu mwingine mzuri au uwoga
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam wakati akitoa maazimio ya kikao cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la chama hicho, Lipumba alisema kutokana na kuwepo kwa makundi ndani ya CCM ndiyo sababu kubwa ya nchi kuwa na ombwe katika uongozi.
Rais akiwa kama ni Mwenyekiti wa CCM ambayo ndiyo inaongoza nchi kwa sasa, anatakiwa kukaa kando ili kuweza kumaliza makundi yao ndani ya chama na kuwapisha viongozi wengine wanaofaa, kuweza kushughulikia masuala ya maendeleo na kukuza uchumi nchini, alisema Profesa Lipumba.
Alisema wanachama wa CCM ambao wengi wao ni viongozi wa ngazi za juu, wamekuwa wakijihusisha na makundi, ugomvi na hata kurushiana maneno badala ya kukaa na kujadili njaa inayowakabili Watanzania wengi kwa sasa.
Baraza Kuu limesikitishwa na kitendo cha CCM kuacha kuwatumikia wananchi iliyowaahidi kuwaletea maisha bora kwa kila Mtanzania na badala yake kugeuka jukwaa la malumbano, mapambano, matusi na kashfa kati ya makundi yanayopigania vita vya kulipizana visasi vinavyotokana na kugombea maslahi binafsi, alisema Lipumba.
Aidha, baraza hilo pia lilimtaka rais kuacha kuchezea akili za Watanzania kwa kuendesha kesi za kisanii za ufisadi na badala yake kutoa maelezo na kuchukua hatua kuhusiana na kashfa nzito za Meremeta, Mwananchi Gold, Tan Gold, Richmond, fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), Kagoda Agriculture Limited ambazo Watanzania wanasubiri kuona hatua zake.
Baraza hilo pia liliitaka serikali kutekeleza kwa ukamilifu maazimio yote 23 ya Bunge kuhusu kashfa ya Richmond na kuwasilisha bungeni katika kikao cha kwanza mwakani.
Aidha Profesa Lipumba alisema wamesikitishwa na uzembe uliofanywa na serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini, ambao umesababisha kukosa umeme wa uhakika, jambo ambalo linazorotesha maendeleo ya kiuchumi. Ni aibu kwa serikali kutangaza kutekeleza mpango wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania (MKUKUTA), huku ikiendelea kushindwa kuja na mipango madhubuti itakayohakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika katika nchi, alisema Lipumba.
Source: Tanzania Daima
My take: Kama hana uwezo si asubiri 2010 ashinde kilaini kwanini anatafuta kushindani na mtu mwingine mzuri au uwoga