nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Na Dunstan Bahai
VYAMA vya Wananchi (CUF) na Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) vimesema vina historia ya kuuchukia ufisadi na kwamba havina sababu ya kutumiwa na mtu au kiongozi yoyote katika kufichua mafisadi wote.
Kauli hiyo ilikuwa ikijibu kauli iliyotolewa na Katibu wa Itikati na Uenezi wa CCM Bw. Nape Nnauye jana kwenye baadhi ya vyombo vya habari.
Bw. Nnaye alinukuliwa akisema kwamba vyama hivyo vinatumiwa na pia ni mawakala wamafisadi waliomo ndani ya CCM katika kumchafua na kumpaka matope Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete.
Akizungumza na Majira jana, Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba, alisema kuwa amestaajabishwa na kauli hiyo ya Bw. Nnauye kwani wao wamekuwa mstari wa mbele na wanayo historia ya kutangaza na kuwafichua mafisadi nchini.
Chama chetu kina historia ya kuchukia ufisadi, na tumekuwa mstari wa mbele katika kutangaza sera zetu zikiwemo za kuuchukia ufisadi kama ule wa manunuzi ya rada, ndege ya Rais, mikataba mibovu ya madini, EPA, IPTL na ufisadi wa ina yoyote hiyo na mstaajabu huyu kijana kama kweli ametoa hiyo kauli, alisema Profesa Lipumba.
Alisema kuwa hakuna kiongozi au mtu yoyote atakayewatumia wao kama chama, kama wa kuchafua watu wengine kwani chama chake kinajinadi kwa sera zake na hata masuala ya ufisadi nayo yamo kwenye sera za chama chao.
Akizungumza kwa niaba ya CHADEMA, Katibu Mtendaji wa chama hicho, Bw. Victor Kimesele alisema kwanza Bw. Nnauye siyo saizi yake na kwamba hiyo kauli ni ya mfa maji.
Huyu kwanza siyo saizi yangu, hizo kauli ni za kutapatapa tu kwani Chadema ilipowataja mafisadi haikutumwa wala kutumiwa na mtu na hata huyo Rais Kikwete alikuwemo kwenye orodha ya mafisadi tuliowataja," alisema Bw. Kimesera.
Huku akiangua kicheko cha kuashiria kuidharau kauli hiyo ya Bw. Nnauye, Bw. Kimesele alisema kuwa Nnauye anaona hodari kuzungumza sana kwenye vyombo vya habari lakini spidi aliyoanza nayo itakwisha.
Kwa mujibu wa Bw. Kimesele, CHADEMA itaendelea kuwataja mafisadi na itaendelea kuwaeleza wananchi jinsi wanavyoharibu uchumi wa nchi.
Alisema kwamba wao wenyewe kwa wenyewe wanajuana mafisadi ni wa kina nani na ndiyo hata kwenye vikao vyao wananyoosheana vidole.
Katibu Mtendaji huyo wa CHADEMA alisisitiza kwamba chama chake ndicho chenye historia ya kutamka hadharani mafisadi na kwamba hata kwenye orodha ya waliyo nayo wamo viongozi wa juu CCM.
Alisema pamoja na kauli ya Nnauye, lakini wataendelea kuwafichua mafisadi na kuwaomba wananchi kutoa ushirikiano katika kuwajua walipo na wanachokifanya katika kuuhujumu uchumi wa Tanzania.
VYAMA vya Wananchi (CUF) na Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) vimesema vina historia ya kuuchukia ufisadi na kwamba havina sababu ya kutumiwa na mtu au kiongozi yoyote katika kufichua mafisadi wote.
Kauli hiyo ilikuwa ikijibu kauli iliyotolewa na Katibu wa Itikati na Uenezi wa CCM Bw. Nape Nnauye jana kwenye baadhi ya vyombo vya habari.
Bw. Nnaye alinukuliwa akisema kwamba vyama hivyo vinatumiwa na pia ni mawakala wamafisadi waliomo ndani ya CCM katika kumchafua na kumpaka matope Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete.
Akizungumza na Majira jana, Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba, alisema kuwa amestaajabishwa na kauli hiyo ya Bw. Nnauye kwani wao wamekuwa mstari wa mbele na wanayo historia ya kutangaza na kuwafichua mafisadi nchini.
Chama chetu kina historia ya kuchukia ufisadi, na tumekuwa mstari wa mbele katika kutangaza sera zetu zikiwemo za kuuchukia ufisadi kama ule wa manunuzi ya rada, ndege ya Rais, mikataba mibovu ya madini, EPA, IPTL na ufisadi wa ina yoyote hiyo na mstaajabu huyu kijana kama kweli ametoa hiyo kauli, alisema Profesa Lipumba.
Alisema kuwa hakuna kiongozi au mtu yoyote atakayewatumia wao kama chama, kama wa kuchafua watu wengine kwani chama chake kinajinadi kwa sera zake na hata masuala ya ufisadi nayo yamo kwenye sera za chama chao.
Akizungumza kwa niaba ya CHADEMA, Katibu Mtendaji wa chama hicho, Bw. Victor Kimesele alisema kwanza Bw. Nnauye siyo saizi yake na kwamba hiyo kauli ni ya mfa maji.
Huyu kwanza siyo saizi yangu, hizo kauli ni za kutapatapa tu kwani Chadema ilipowataja mafisadi haikutumwa wala kutumiwa na mtu na hata huyo Rais Kikwete alikuwemo kwenye orodha ya mafisadi tuliowataja," alisema Bw. Kimesera.
Huku akiangua kicheko cha kuashiria kuidharau kauli hiyo ya Bw. Nnauye, Bw. Kimesele alisema kuwa Nnauye anaona hodari kuzungumza sana kwenye vyombo vya habari lakini spidi aliyoanza nayo itakwisha.
Kwa mujibu wa Bw. Kimesele, CHADEMA itaendelea kuwataja mafisadi na itaendelea kuwaeleza wananchi jinsi wanavyoharibu uchumi wa nchi.
Alisema kwamba wao wenyewe kwa wenyewe wanajuana mafisadi ni wa kina nani na ndiyo hata kwenye vikao vyao wananyoosheana vidole.
Katibu Mtendaji huyo wa CHADEMA alisisitiza kwamba chama chake ndicho chenye historia ya kutamka hadharani mafisadi na kwamba hata kwenye orodha ya waliyo nayo wamo viongozi wa juu CCM.
Alisema pamoja na kauli ya Nnauye, lakini wataendelea kuwafichua mafisadi na kuwaomba wananchi kutoa ushirikiano katika kuwajua walipo na wanachokifanya katika kuuhujumu uchumi wa Tanzania.