'Cristiano Ronaldo Ametembea na Wanawake 80,000'

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,320
33,125
2383010.jpg

Cristiano Ronaldo Thursday, July 02, 2009 6:02 AM
Mpenzi wa zamani wa nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo ambaye alitoswa kwa njia ya ujumbe wa simu ameibuka na kutoa kali ya mwaka akidai kuwa mpenzi wake huyo wa zamani ametembea na wanawake 80,000. Nereida Gallardo mrembo wa Hispania alikuwa katika mapenzi na Cristiano Ronaldo kwa miezi minane kabla ya Ronaldo kuamua kumtosa kwa njia ya ujumbe wa simu.

Akiongea na gazeti la The Sun la Uingereza, Nereida alidai kwamba Paris Hilton ni mmoja wa wasichana 80,000 waliolala na Ronaldo tangia alipoachwa.

Nereida pia alimkandia Ronaldo kwa kusema kuwa hana chochote na hawezi kufananishwa na David Beckham.

Cristiano Ronaldo ndiye mchezaji anayelipwa pesa nyingi kuliko wote duniani hivi sasa baada ya kuvunja rekodi ya usajili kwa kuhamia Real Madrid kutoka Manchester kwa kitita cha dola milioni 173.

Nereida alisema kwamba alicheka sana wakati aliposikia Ronaldo yuko pamoja na Paris Hilton jijini Los Angeles, Marekani.

"Ni mmoja wa wanawake wengi waliolala kwenye kitanda cha Ronaldo" alisema Nereida.

"Kila wiki Ronaldo ana mwanamke tofauti" alisema Nereida na kuongeza " Tangia aliponiacha sijui ni wanawake wangapi ameshatembea nao, nakisia watakuwa 80,000".

Wakati huo huo Cristiano Ronaldo atatambulishwa mbele ya washabiki wa Real Madrid jumatatu baada ya juzi nyota wa Brazili, Kaka kutambulishwa mbele ya washabiki wengi sana wa Real Madrid walioujaza uwanja wa Santiago Bernabeu.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=2383010&&Cat=6
 
Anajua 80,000 ni nini?

Huyu dogo kazaliwa 1985, hivyo ana miaka 24, tuseme kaanza shughuli akiwa na miaka 10, hivyo ana miaka 14 ya shughuli, miaka 14 ina siku takriban 5000, ukigawanya 80,000 kwa 4749 ni karibu 20.

Kwa maana hiyo jamaa alikuwa analala na wanawake takribani 20 kila siku kuanzia alivyokuwa na miaka 10 mpaka leo, na mpira alicheza saa nagapi? alikuwa anakula nini?
 
Last edited:
Hell hath no fury than a woman scorned.. (tena kwa sms)..bua ha ha ha..!
 
Hahahaha its so funny....huyo mwanamama anadai 80,000 tangia alipoachwa yeye so it means ni zaidi ya hiyo namba kwa sababu sidhani kama ronaldo alianzia kwake mavituz..........halafu yeye mbona hasemi ameshalala vitanda vingapi vya wanaume tofauti tofauti?
 
Hii imekaa safi sana.

Inanikumbusha Babu mmoja aliyekuwa akijisifu kuwa shughuli ya mapenzi kwenye uwanja wa fundi seremala, huofanya kwa saa nzima. Vijana ilibidi washtuke na kumdadisi babu kuwa imekaa kaaje hiyo saa moja?
Babu akasema:-
"Maandilizi hadi kupanda kitandani ni dakika 10, shughuli kuanza hadi kumalizika ni dakika 5 na dakika 45 zinazofuata anakuwa kitandani anakoroma......
 
Back
Top Bottom