Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,320
- 33,125
Cristiano Ronaldo Thursday, July 02, 2009 6:02 AM
Mpenzi wa zamani wa nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo ambaye alitoswa kwa njia ya ujumbe wa simu ameibuka na kutoa kali ya mwaka akidai kuwa mpenzi wake huyo wa zamani ametembea na wanawake 80,000. Nereida Gallardo mrembo wa Hispania alikuwa katika mapenzi na Cristiano Ronaldo kwa miezi minane kabla ya Ronaldo kuamua kumtosa kwa njia ya ujumbe wa simu.
Akiongea na gazeti la The Sun la Uingereza, Nereida alidai kwamba Paris Hilton ni mmoja wa wasichana 80,000 waliolala na Ronaldo tangia alipoachwa.
Nereida pia alimkandia Ronaldo kwa kusema kuwa hana chochote na hawezi kufananishwa na David Beckham.
Cristiano Ronaldo ndiye mchezaji anayelipwa pesa nyingi kuliko wote duniani hivi sasa baada ya kuvunja rekodi ya usajili kwa kuhamia Real Madrid kutoka Manchester kwa kitita cha dola milioni 173.
Nereida alisema kwamba alicheka sana wakati aliposikia Ronaldo yuko pamoja na Paris Hilton jijini Los Angeles, Marekani.
"Ni mmoja wa wanawake wengi waliolala kwenye kitanda cha Ronaldo" alisema Nereida.
"Kila wiki Ronaldo ana mwanamke tofauti" alisema Nereida na kuongeza " Tangia aliponiacha sijui ni wanawake wangapi ameshatembea nao, nakisia watakuwa 80,000".
Wakati huo huo Cristiano Ronaldo atatambulishwa mbele ya washabiki wa Real Madrid jumatatu baada ya juzi nyota wa Brazili, Kaka kutambulishwa mbele ya washabiki wengi sana wa Real Madrid walioujaza uwanja wa Santiago Bernabeu.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=2383010&&Cat=6