platozoom
JF-Expert Member
- Jan 24, 2012
- 9,366
- 11,156
Jamaa kampenda binti....Bila shaka kwenye macho ya wengi ilionekana wanapendana. Siku zikaenda na miezi kadhaa.
Sijui nini kilimpata binti, akaanza kupungunza mapenzi kwa Boyfriend wake. Boyfriend akawa anamlaumu kulikoni umekuwa hivyo siku hizi, binti akatia pamba.
Uhakika kama binti anamsaliti hana. Hatimaye binti akasema "yatosha" sitaki haya mahusiano tena kwa lugha ya kukera. Jamaa akalalamika lakini akakubali shingo upande hasira moyoni. Baada ya mwezi akamfuata mpenzi wake akiwa mpole na lake moyoni....Kweli baada ya kuzungushwa kama wiki 3 binti akakubali kurudiana naye.
Mapenzi yakaanza kunoga..Jamaa alipoona binti sasa kafika na ka-relax akamfanyia kitimbi fulani siku moja..binti akamsihi abadilike na kulalamika................Jamaa akamwasha kibao na kumwambia "Kuanzia leo mimi na wewe mwisho ondoka'.
Binti mpaka sasa mawazo tele na machozi kibao, lakini jamaa ana furaha kupita kiasi.........Kumbe kumbembeleza kote ilikuwa ni njama ya kulipa kisasi.
My take: Huu mchezo alioufanya jamaa si mzuri.
Sijui nini kilimpata binti, akaanza kupungunza mapenzi kwa Boyfriend wake. Boyfriend akawa anamlaumu kulikoni umekuwa hivyo siku hizi, binti akatia pamba.
Uhakika kama binti anamsaliti hana. Hatimaye binti akasema "yatosha" sitaki haya mahusiano tena kwa lugha ya kukera. Jamaa akalalamika lakini akakubali shingo upande hasira moyoni. Baada ya mwezi akamfuata mpenzi wake akiwa mpole na lake moyoni....Kweli baada ya kuzungushwa kama wiki 3 binti akakubali kurudiana naye.
Mapenzi yakaanza kunoga..Jamaa alipoona binti sasa kafika na ka-relax akamfanyia kitimbi fulani siku moja..binti akamsihi abadilike na kulalamika................Jamaa akamwasha kibao na kumwambia "Kuanzia leo mimi na wewe mwisho ondoka'.
Binti mpaka sasa mawazo tele na machozi kibao, lakini jamaa ana furaha kupita kiasi.........Kumbe kumbembeleza kote ilikuwa ni njama ya kulipa kisasi.
My take: Huu mchezo alioufanya jamaa si mzuri.