Kamisheni inayosimamia ngumi za kulipwa Tanzania TPBRC, kupitia makamu wake imewapa adhabu za faini bondia Cosmas Cheka na mwenzie Isa Nampepeche.
Cosmas Cheka amepigwa faini ya Tshs laki nne (400,000/-) na Isa Nampepeche faini ya Tshs Laki Tatu (300,000/-).
Faini zote zilipwe ndani ya mwezi mmoja.
Aidha wamepewa onyo kali kwa sababu ni kosa lao la kwanza.
Bondia Cosmas Cheka alimpiga ngumi bondia mwenzie Isa Nampeche wakati wanafanyiwa mahojiano yaliyokuwa yanarushwa mubashara kwenye Runinga.
Mabondia hao walitarajiwa kupambana lakini ilishindikana baada ya Cosmas Cheka kuumia mkono jambo ambalo Isa Nampeche alipinga kama janja ya Cosmas kumkimbia.
Mara kadhaa mabondia hao mapambano yao yaliahirishwa kwa sababu kadhaa.
Licha ya kukubali msamaha wa Cosmas Cheka, bondia Isa Nampeche hakuridhishwa na faini aliyopigwa kwa sababu hakuna kosa alilofanya zaidi ya yeye ndio aliyopigwa ngumi.
Cosmas Cheka amepigwa faini ya Tshs laki nne (400,000/-) na Isa Nampepeche faini ya Tshs Laki Tatu (300,000/-).
Faini zote zilipwe ndani ya mwezi mmoja.
Aidha wamepewa onyo kali kwa sababu ni kosa lao la kwanza.
Bondia Cosmas Cheka alimpiga ngumi bondia mwenzie Isa Nampeche wakati wanafanyiwa mahojiano yaliyokuwa yanarushwa mubashara kwenye Runinga.
Mabondia hao walitarajiwa kupambana lakini ilishindikana baada ya Cosmas Cheka kuumia mkono jambo ambalo Isa Nampeche alipinga kama janja ya Cosmas kumkimbia.
Mara kadhaa mabondia hao mapambano yao yaliahirishwa kwa sababu kadhaa.
Licha ya kukubali msamaha wa Cosmas Cheka, bondia Isa Nampeche hakuridhishwa na faini aliyopigwa kwa sababu hakuna kosa alilofanya zaidi ya yeye ndio aliyopigwa ngumi.