Mtumzima
Senior Member
- Sep 10, 2008
- 156
- 107
Ndugu zangu humu JF,
Salaam.
Nimetafakari mengi sana juu ya movie ya 'Uchaguzi Mkuu' wa Tanzania 2015.Nimeona kwa upande wangu na mimi walau nisaidiwe hoja hii tuweze kujua japo kidogo yasemwayo ndani ya jamii yetu.
Wengi tunakumbuka mambo ya uchaguzi mkuu mwaka 1995 yalivyokuwa.kwa wakati ule kwa upande wa CCM walijitokeza makada kadhaa kutaka kuwania kiti cha Urais wa Tanzania.Walikuwepo makada wawili waliotangaza nia kwa staili yao.Jakaya Kikwete na Edward Lowassa.
Inasemekana baada ya kujadiliwa ndani ya vikao ndani ya CCM na hatimkaye mchakato kufanyika,Lowassa hakuwa na sifa za kupata nafasi hiyo kwa mujibu wa taratibu ndani ya CCM.Mwalimu akiwa kama mmoja wa viongozi wakuu (ingawa hakuhusika na kupiga kura) alimshauri Kikwete kusubiri na ilihali Edward Lowassa akiambiwa wazi hafai.
Inasadikiwa kwamba bwana huyu alikubali na kwa staili yake ya kunyamaza kama ilivyokuwa kwa suala la Richmond.Alipania kuwa ni lazima aingie ikulu kwa namna yoyote ile.Kikwazo kilikuwa ni Julius Nyerere.
Mkapa alipoingia aliendelea na kazi yake huku Kikwete akiwa waziri wa mambo ya nchi za nje.
Likaja suala la kuugua na hatimaye kufariki kwa Julius Nyerere mwaka 1999.Suala hili lina utata mpaka leo.linafukiwa fukiwa kwa staili za ajabu.
Wakati mwalimu akiwa anaumwa pale st Thomas,kuna wakati alitumwa Mzee Kingunge Ngombale Mwiru kwa kilichoitwa "KUDHIBITI" habari za ugonjwa na matibabu ya Mwalimu.Swali linakuja je, Mzee kingunge alikuwa ni Waziri wa Afya,Daktari wa Mwalimu au msemaji wa serikali/familia ya Mwalimu??Je, alikuwa akidhibiti nini cha ajabu?Hatujui!.
Inasemekana Mwalimu alipokuwa huko Ughaibuni alitaka kumuona rafiki yake wa karibu Marehemu Mzee Rashid Kawawa.Kawawa alikwenda Uingereza.Aliporudi tulishuhudia magazeti yakiandika "KAWAWA ARUDI YA SIRI MOYONI".Hatukuambiwa ni siri gani mpaka leo.Hatimaye Mwalimu akatutoka na tukamzika kule Mwitongo.Wakati taifa halijathibitishiwa kuhusu kifo cha mwasisi yule,tayari heka heka zilianza kuonekana Dar es salaam kutayarisha mazingira ya kitu fulani...hasa msiba.
Ndugu yetu Kapteni John Komba alikuwa ametayarisha nyimbo kadhaa za maombolezo ya kifo cha Mwalimu!
Hapa najaribu kuandika kilichojiri wakati ule na baadhi ya matukio ya sasa ya kuutaka urais kwa namna yoyote ile kwa Edward Lowassa.
Alipoingia Kikwete tumeyaona na kuyasikia mengi.anakaribia kutoka.
Suala la kutangaza nia lilikuwepo miezi michache iliyopita na tumemshuhudia Mzee kingunge akilalamika hata kabla mchakato wa Dodoma kuanza,alianza kupiga kelele kwama kuna njama za kuwakata majina watu wengine.Sisi hatukujuwa anayezungumziwa ni nani ila tulijionea kwenye kutangaza nia kule Arusha Mzee Kingunge akiwa kifua mbele kumtetea huyu Lowassa.
Sasa swali linakuja je, kwa Kingunge kujitutumua kumpigania Lowassa ambaye alimuona Mwalimu kama kikwazo kwake kutimiza lengo lake,huku ni katika kutetea malipo ya kazi yake ya "UDHIBITI alioufanya mwaka 1999 kuhusu Mwalimu..kikwazo kikubwa cha Edward Lowassa na kundi lake kutawala???
Mwenye taarifa zaidi atupe ili tujue ukweli japo kidogo.
Nawasilisha.....
Salaam.
Nimetafakari mengi sana juu ya movie ya 'Uchaguzi Mkuu' wa Tanzania 2015.Nimeona kwa upande wangu na mimi walau nisaidiwe hoja hii tuweze kujua japo kidogo yasemwayo ndani ya jamii yetu.
Wengi tunakumbuka mambo ya uchaguzi mkuu mwaka 1995 yalivyokuwa.kwa wakati ule kwa upande wa CCM walijitokeza makada kadhaa kutaka kuwania kiti cha Urais wa Tanzania.Walikuwepo makada wawili waliotangaza nia kwa staili yao.Jakaya Kikwete na Edward Lowassa.
Inasemekana baada ya kujadiliwa ndani ya vikao ndani ya CCM na hatimkaye mchakato kufanyika,Lowassa hakuwa na sifa za kupata nafasi hiyo kwa mujibu wa taratibu ndani ya CCM.Mwalimu akiwa kama mmoja wa viongozi wakuu (ingawa hakuhusika na kupiga kura) alimshauri Kikwete kusubiri na ilihali Edward Lowassa akiambiwa wazi hafai.
Inasadikiwa kwamba bwana huyu alikubali na kwa staili yake ya kunyamaza kama ilivyokuwa kwa suala la Richmond.Alipania kuwa ni lazima aingie ikulu kwa namna yoyote ile.Kikwazo kilikuwa ni Julius Nyerere.
Mkapa alipoingia aliendelea na kazi yake huku Kikwete akiwa waziri wa mambo ya nchi za nje.
Likaja suala la kuugua na hatimaye kufariki kwa Julius Nyerere mwaka 1999.Suala hili lina utata mpaka leo.linafukiwa fukiwa kwa staili za ajabu.
Wakati mwalimu akiwa anaumwa pale st Thomas,kuna wakati alitumwa Mzee Kingunge Ngombale Mwiru kwa kilichoitwa "KUDHIBITI" habari za ugonjwa na matibabu ya Mwalimu.Swali linakuja je, Mzee kingunge alikuwa ni Waziri wa Afya,Daktari wa Mwalimu au msemaji wa serikali/familia ya Mwalimu??Je, alikuwa akidhibiti nini cha ajabu?Hatujui!.
Inasemekana Mwalimu alipokuwa huko Ughaibuni alitaka kumuona rafiki yake wa karibu Marehemu Mzee Rashid Kawawa.Kawawa alikwenda Uingereza.Aliporudi tulishuhudia magazeti yakiandika "KAWAWA ARUDI YA SIRI MOYONI".Hatukuambiwa ni siri gani mpaka leo.Hatimaye Mwalimu akatutoka na tukamzika kule Mwitongo.Wakati taifa halijathibitishiwa kuhusu kifo cha mwasisi yule,tayari heka heka zilianza kuonekana Dar es salaam kutayarisha mazingira ya kitu fulani...hasa msiba.
Ndugu yetu Kapteni John Komba alikuwa ametayarisha nyimbo kadhaa za maombolezo ya kifo cha Mwalimu!
Hapa najaribu kuandika kilichojiri wakati ule na baadhi ya matukio ya sasa ya kuutaka urais kwa namna yoyote ile kwa Edward Lowassa.
Alipoingia Kikwete tumeyaona na kuyasikia mengi.anakaribia kutoka.
Suala la kutangaza nia lilikuwepo miezi michache iliyopita na tumemshuhudia Mzee kingunge akilalamika hata kabla mchakato wa Dodoma kuanza,alianza kupiga kelele kwama kuna njama za kuwakata majina watu wengine.Sisi hatukujuwa anayezungumziwa ni nani ila tulijionea kwenye kutangaza nia kule Arusha Mzee Kingunge akiwa kifua mbele kumtetea huyu Lowassa.
Sasa swali linakuja je, kwa Kingunge kujitutumua kumpigania Lowassa ambaye alimuona Mwalimu kama kikwazo kwake kutimiza lengo lake,huku ni katika kutetea malipo ya kazi yake ya "UDHIBITI alioufanya mwaka 1999 kuhusu Mwalimu..kikwazo kikubwa cha Edward Lowassa na kundi lake kutawala???
Mwenye taarifa zaidi atupe ili tujue ukweli japo kidogo.
Nawasilisha.....