Coming soon: New Kawe City (Uptown Kawe)

Wabongo wanapenda picha, so wape picha. Ndio maana wanafunga safari kwenda kupiga picha Mlimani City na Quality Centre kisha wanarudi kwao Buguruni Mnyamani, Tandale Mtogole au Manzese kwa Mfuga Mbwa na ku-chilll tu wala hawawi-inspired! Business as usual. Na serikali inalijua hilo vizuri sana.

Tunataka vitu halisi na sio mapicha picha tuuuu.

Na wanatuweza kweli na mapichapicha haya! wameshatujua udhaifu wetu

Mlimani city watu waliambiwa hivyo hivyo lakini hamna kinachoendelea pale
 
Ivi imekuwaje kila kitu mkiambiwa hamuamini yaani mumekosa imani na serikali yenu kiasi hicho
Ni mpango mzuri all the best for the planners and those in the project team to make it real
 
Huo ni ujanja wa watawala kujitwalia maeneo nyeti na muhimu zikiwemo fukwe za bahari kwa kigezo cha uwekezaji. Ni aibu na fedheha iliyoje kwa watawala kupanga mikakati ovu ya kuua viwanda ili waweze kujitwalia maeneo kwa faida zao binafsi. Kuna fununu kuwa eneo lote la iliyokuwa TANGANYIKA PACKERS limeshatwaliwa watawala waroho kwa mgongo/kivuli cha NHC
 
Ivi imekuwaje kila kitu mkiambiwa hamuamini yaani mumekosa imani na serikali yenu kiasi hicho
Ni mpango mzuri all the best for the planners and those in the project team to make it real
Ni kweli. Hatuna imani tena na serekali, full stop! Which is very very bad!
 
Tumuulize mbunge husika. Mchoro wenyewe unaonyesha utawameza wananchi wote waishio Kawe. Na ni kwa nini Dar tu? Dodoma makao makuu ya nchi haihitaji maendeleo kama haya?

Nashukuru kwa upande wa Tanga wamepeleka Pongwe Satellite City Project.

Dar walete miradi ya miundo mbinu zaidi kama ujenzi wa reli na meli kwa ajili ya usafirishaji wa abiria.
 
Nani wa kufadhili mradi huo? Kigamboni City imeishia kwenye internet, je hiyo Kawe City Mtaiweza?
Vinginevyo mtaambiwa kwanza muwe mashoga ndipo mfadhiliwe
 
Tanzania kwa mipango hatujambo!mambo yote huishia kwenye karatasi tukishachukua pesa
 
Nchi yetu imejaa wezi sana, naona sasa umezuka ufisadi wa aina mpya wa kutuchorea picha/city plans na kupiga hela za walipa kodi. Ukiuliza ni TZS ngap zimetumika katika kudevelop hiyo plan unaweza ukazimia. Kama kweli serikali imedhamiria kuendeleza nchi, kwanini isimalize plan ambayo tayari ipo???? Au kigamboni project imeshaisha???? Pia hiyo ni mbinu tu ya kutuibia lile eneo maana bila mapichapicha ya hivi pale hapaingiliki.

Kama nguvu ya kuendeleza eneo hilo ipo, pls tumalizieni kwanza Kigamboni project kisha tuamie Kawe. Hizi ni namna ya kutuibia hela kwa kujifanya wamelipa mabilioni kwa hao wanaodevelop hizo plan. Wiiiiizi mtupu. Hii serikali ilishajitoaga kwenye uwekezaji, kiherehere tena cha nn kwenye kugharamia maplan ya mabilion haya??? Wapelekeeni madawa na maendeleo bibi zangu vijijini.

Hakika unachosema!
Hii ni nchi ya kipuuzi tu! Mtindo mkubwa kabisa wa kipuuzi, kishenzi na kipumbavu ni huu wa kudhani kwamba Tanzania ni Daressalaam tu. Kila siku mijitu hii inayolia kule Bungeni inadhani Tanzania yote itahamia Dar.

Wanachota pesa ya serikali wanampa mtu ananunua UDA, wanachota pesa za serikali wanampa mtu anajenga vituo vya mafuta, sasa wanakuja na upuuzi huu wa kawe, tanzanite, kigamboni, n.k. Yote haya wanafikiria ni Dar tu.

Je wapuuzi hawa wanakumbuka kwamba tangu tupate uhuru hawajawahi kujenga Hospitali hata moja? wanafahamu kwamba watu milioni 5 walioko Dar sasa ni watu wanaohitaji hospitali kuliko shopping molls?

Naanza kutia mashaka juu ya uwezo wa mwafrika. Nadhani kweli sisi ni genetically weak.
 
Nchi hii imeendelea sana kwenye makaratasi,makablasha, mafaili na madokomenti tena ni zaidi ya u.s.a ila kwenye uhalisia ndo balaha.
 
JK alipoingia madarakani alisema ataifanya Kigoma kuwa kama Dubai na Mwanza kuwa kama Califonia. Atajenga Machinga Complex kila wilaya! Duuh, si shangai kutengeneza michoro mingi ya kila eneo la Dar ili kuwapa matumaini washinda vijiweni wasirect kwa kukosa ajira, kumbe upepo mtupu ataondoka 2015 hata 10% ya ahadi zake hajatekeleza!

Kiongozi huyu anajua kucheza na akili za wabongo!
 
Jamani, hapa si ndio pale Tanganyika parkers walipobomoa nyumba karibia mia mbili juzi, NHC wamebomoa nyumba za kizamani pale nahisi labda ndio wanataka waanze ujenzi wa mji huu mpya. kama ni hivyo itakuwa safi sana.
 
Back
Top Bottom