white wizard
JF-Expert Member
- May 18, 2011
- 8,316
- 13,282
juzi nilikuwa nakwenda morogoro,nimepanda basi la ABOOD,tumefika maeneo ya ruvu darajani,tairi moja la nyuma likapata pancha,tukatelemka ili wabadilishe tairi,wakaanza kazi ya kufungua tairi hilo,kaka nut zikawa ngumu sana kufunguka,huwa wanatumia bomba fulani[mtalimbo] wanaingiza spana kisha wanabembea,zile nut zilikuwa zimekazwa ile mbaya!hadi mabaunsa 3 wananing'inia hazifunguki jasho limewatoka.MUNGU sio mzee mkumba kama asemavyo Mbwiga,likatokea lori kubwa la mafuta likasimama,kwa mbele,akaja tingo akawaambia nenda ukanunue soda aina ya coca cola /Pepsi ulete hapa,kweli tingo wa bac akafanya hivyo,jamaa akaifungua ile soda aina ya coca cola na kuzimwagia zile nuts zote,kisha akawambia haya fungueni Ebwana zimekuwa laini kama unanawa vile!watu wote tuliona kama maajabu!!!!!!!Sasa kwa wataalam wa chemistry hii inakuwaje?au ndio maana wa2 wenye ulcers wanakatazwa kunya soda aina hizi??MIMI COCA/PEPSI BASI TENA KAMA KUTU INA LAINIKA VILE SEMBUSE TUMBO!!!!:yield: