Chukua tahadhari eneo la nyuma ya chuo cha Ustawi wa Jamii

Kim Jong Jr

JF-Expert Member
Mar 15, 2014
10,929
20,164
Habari wanajamvi...

Siku za hivi karibuni kumezuka kikundi cha vijana waharifu wanaotumia mapanga, visu, fimbo na malungu kufanya unyang'anyi kwa raia wa eneo tajwa au wapita njia wasioishi eneo hilo..

Mwezi uliopita Mwanafunzi wa chuo cha ustaw wa jamii alinusurika kifo baada ya kucharangwa mapanga na kuibiwa kila kitu alipokuwa akielekea chuoni kwenye tamasha la michezo ya chuo akitokea hostel za nje mida ya alfajiri.. Tukio hilo lilitokea karibu na ofisi za Kituo cha sheria na haki za binaadamu....

Wiki jana pia Mzee mmoja anaeishi eneo la nyuma ya chuo cha ustawi wa jamii alichomwa visu tumboni na vibaka hao muda wa saa kumi na moja asubuhi wakati akielekea kusali kanisa la ROMA Mwenge... Huyu mzee kwa sasa ana hali tete sana nasikia amelazwa muhimbili japo sina uhakika sana juu ya hilo..

Juzi usiku mbele ya ofisi za ofisi ya kituo cha sheria (LHRC) dereva wa bodaboda alitekwa na kuchomwa na bomba la kutolea moshi wa pikipiki kisha akaibiwa pikipiki na kujeruhiwa kwa mapanga..

Kikundi hiki kimekuwa kikitumia pikipiki au bajaji kufanya shughuli zao... Wakiwa kwenye shighuli zao endapo wakikukuta upo peke yako wanakushambulia kwa mapanga bila kuuliza na kukuchukulia kila kitu...

Jana nimenusurika kifo nilikuwa natokea makumbusho mida ya saa tano usiku nikielekea makongo juu. Niliamua kupitia shortcut ya barabara ya nyuma ya chuo cha ustaw wa jamii kwa kuingilia njia panda ya sayansi...
Nilipofika eneo karibu na Kituo cha sheria na haki za binaadamu ambapo barabara ina mashimo mengi sana. Niliona kikundi cha watu kama ishirini yaani 20 kikiwa kimeshika mapanga na visu na wengine wakinoa mapanga kwenye lami.. Nilichanganyikiwa saaaaaaaaana... Ile barabara ni nyembamba kwa ambao wanaifahamu si rahisi kugeuza haraka haraka... Wakati najiuliza namna ya kuguza nikimbie vijana wanne wakawa wamefika hatua chache karibu na gari wakinipa ishara ya kushuka... Nilichokifanya ni kukanyaga mafuta nikijiapiza lolote liwe mpaka nikaenda kutokea kona ya bar ya hongera....


Matukio ni mengi saaaaaaana kama ukipata muda wa kuongea na wenyeji...

Nilisikia kuwa mwaka jana pia kuna mwanafunzi wa cho cha ustawi alinisurika kifo alipotekwa na kunyang'anywa tiketi za ndege za wanafunzi waliokuwa wanaenda alfajiri hiyo kupanda ndege kwenda uganda kwenye ziara ya kimasomo...


TUNAOMBA ULINZI UIMARISHWE ENEO HILO KWANI NI HATARI KWA WAPITA NJIA NA WAKAZI WA ENEO HILO
 
Poleni wakazi wa hilo eneo...fanyeni mkakati muwawekee mtego,mkimpata hata mmoja ni kumchoma moto tu.
Mkisubiri polosi basi mtangoja sana
 
Du hatari ila mkuu kama ikitokea nimekuta vibaka wamesimama barabarani hawajapanga mawe wala magogo wakati niko na gari hata wanisimamishe kama walivyokufanyia ni lazima wataisoma namba nitapita nao
 
Kwani hakuna jipo lolote liliotumbuliwa polisi hadi sasa?...ila dawa ndio hiyo uwekwe mtego mnakamata hata wawili mnachoma kama ndafu basi watatulia walau mwaka..mnafanya ndafu tena basi maisha yanaendelea. Kwa maana hakuna namna sasa
 
Du hatari ila mkuu kama ikitokea nimekuta vibaka wamesimama barabarani hawajapanga mawe wala magogo wakati niko na gari hata wanisimamishe kama walivyokufanyia ni lazima wataisoma namba nitapita nao

yani sijui wangekuwa wamepanga mawe ingekuaje
 
Pole sana ndu. Wewe ni Muungwana sana umeweza kutuwekea TAARIFA ya usalama hapa !!!
Sasa jeshi la polisi na wahusika mujipange kuudhibiti mtaharuki huo wa kihalifu !!
Mungu ibariki Tanzania..
Daud1990 be blessed
 
pole sana mkuu, najaribu kuvuta picha ulivosimamia stelingi kama van dame.Ushauri tufunge ngao gari zetu na tuwe tunaangalia movie za action kwa wingi.
 
Lazima tuseme ukweli.
Makundi kama haya ambayo yanaweka kambi sehem muda mrefu,lazima polisi wanataarifa.
Na kukua kwa makundi haya ni kwakuwa wakianza wachache basi wenzao wanaingia kwakuona kwamba kuna pesa rahisi.
Mwisho wasiku inawezekana kukawa na makundi makubwa zaidi ya panya road ambapo serikali itabidi itumie nguvu kubwa sana na budget kubwa sana kuidhibiti hali hiyo.

Jeshi la polisi lisisubiri hadi hali iwe mbaya kama hivi,na kufanya watu kukosa imani nao,intelegensia ya polisi inafanyaklazi gani?Leo raia wa kawaida ana taarifa muhim za kugundua makundi haya na namna ya kuyatega kuliko hata Polisi,na kuienda kituo cha Polisi ukiwapa namna ya mikakati ya kuwatega hao wahalifu,wanakujibu Usitufundishe kazi tunajua cha kufanya.
Ila sio siri ,Dar inaelekea kuwa Jiji lisilo salama kwa kasi ya matukio ya kutisha
 
KWANZA NACHELEA KUAMINI MTOA MADA NI MKAZI WA MTAA HUU AMA NDIO WALE WANAO KUJA KUVIZIA WANAFUNZI...MAANA NI KWELI UHALIFU UMEZIDI SANA KWA HIZI SIKU ZA KARIBUNI..HIVYO SERIKALI YA MTAA KUSHIRIKIANA NA VIJANA WANAOISHI MTAANI HAPO WAKIWEMO WANAFUNZI WA USTAWIBWA KAMII KWA PAMOJA WALIAFIKIANA KUANZISHA ULINZI SHIRIKISHI (SUNGUSUNGU) NA NDIO VOJAN ULIOWAONA JANA WAKIZUNGUKA MTAANI ZAMU KWA ZAMU NA KWA MAFUNGU..SIJUI ILIKUAJE MTOA MADA WEWE MA GARI LAKO WAKAKUSIMAMISHA COZ MOJA YA TARGET KUBWA JANA ILIKUA VIJANA WA BODABODA ..MAANA NDIO TAARIFA TILIZONAZO NDIO WAHUSIKA WAKUU
 
KWANZA NACHELEA KUAMINI MTOA MADA NI MKAZI WA MTAA HUU AMA NDIO WALE WANAO KUJA KUVIZIA WANAFUNZI...MAANA NI KWELI UHALIFU UMEZIDI SANA KWA HIZI SIKU ZA KARIBUNI..HIVYO SERIKALI YA MTAA KUSHIRIKIANA NA VIJANA WANAOISHI MTAANI HAPO WAKIWEMO WANAFUNZI WA USTAWIBWA KAMII KWA PAMOJA WALIAFIKIANA KUANZISHA ULINZI SHIRIKISHI (SUNGUSUNGU) NA NDIO VOJAN ULIOWAONA JANA WAKIZUNGUKA MTAANI ZAMU KWA ZAMU NA KWA MAFUNGU..SIJUI ILIKUAJE MTOA MADA WEWE MA GARI LAKO WAKAKUSIMAMISHA COZ MOJA YA TARGET KUBWA JANA ILIKUA VIJANA WA BODABODA ..MAANA NDIO TAARIFA TILIZONAZO NDIO WAHUSIKA WAKUU
Mkuu kama ni kweli kuna hii sungu sungu ni jambo jema, ila na wao kama wanafanya vitendo vyao
Vinavyopelekea kutisha wananchi (kunoa mapanga barabaran kama mtoa mada alovyosema)itakuwa ni ngumu kitambua kama ni sungu sungu au ni vibaka wenyewe
 
Back
Top Bottom