PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,203
- 8,725
Wanajamvi,
Kwa kipindi hiki cha mwaka, huwa ni mwanzo wa mvua kwa maeneo ya huku Arusha na Kanda nzima ya Kaskazini.
Kwa wanaofika Arusha, wataona bila kuambiwa kuwa eneo la Mlima Meru na maeneo ya jirani yake yako kwenye ukungu muda mwingi.
Na kwa bahati, mbaya, eneo hili ndipo mahali panapo husika na tukio la Uchaguzi, utakaotanguliwa na kampeni za kunadi sera!
Tumeshuhudia tokea miaka ya karibuni vyama kadha vimekuwa vikitumia Helikopta katika kampeni zao, kwa lengo la kuyafikia maeneo mengi katika muda mfupi unaopangwa kwaajili ya kampeni.
Kwa eneo hili la Arumeru, nawatahadharisha sana vyama vyote vitakavyohusika, Visithubutu kutumia helikopta, maana Arumeru yote ni eneo la mlima na vilima, ambavyo kwa majira ya sasa kumefunikwa na Ukungu.
Aidha natambua kuwa Helikopta inahitaji clearance kubwa ya Visibility na Obstacle -Free Zone ili rubani aweze kuona kwa usahihi horizon lines, ambapo kwa eneo la Arumeru kwa sasa hali hiyo ni negotiable.
Wagombea wetu wote tunawapenda sana, na hatutaki kampeni zigeuke kuwa msiba kwa jambo ambalo linaepukika.
Nawasilisha.
Kwa kipindi hiki cha mwaka, huwa ni mwanzo wa mvua kwa maeneo ya huku Arusha na Kanda nzima ya Kaskazini.
Kwa wanaofika Arusha, wataona bila kuambiwa kuwa eneo la Mlima Meru na maeneo ya jirani yake yako kwenye ukungu muda mwingi.
Na kwa bahati, mbaya, eneo hili ndipo mahali panapo husika na tukio la Uchaguzi, utakaotanguliwa na kampeni za kunadi sera!
Tumeshuhudia tokea miaka ya karibuni vyama kadha vimekuwa vikitumia Helikopta katika kampeni zao, kwa lengo la kuyafikia maeneo mengi katika muda mfupi unaopangwa kwaajili ya kampeni.
Kwa eneo hili la Arumeru, nawatahadharisha sana vyama vyote vitakavyohusika, Visithubutu kutumia helikopta, maana Arumeru yote ni eneo la mlima na vilima, ambavyo kwa majira ya sasa kumefunikwa na Ukungu.
Aidha natambua kuwa Helikopta inahitaji clearance kubwa ya Visibility na Obstacle -Free Zone ili rubani aweze kuona kwa usahihi horizon lines, ambapo kwa eneo la Arumeru kwa sasa hali hiyo ni negotiable.
Wagombea wetu wote tunawapenda sana, na hatutaki kampeni zigeuke kuwa msiba kwa jambo ambalo linaepukika.
Nawasilisha.