Chonde Chonde Ndugu zetu Wazanzibari, Msilete Fyoko Fyoko, Mtaumia bure!

Pasco lazima ukumbuke kitu kimoja shauri la Zanzibar mara hii lipo tofauti na miaka yote. Mara hii jumuia ya kimataifa haipo pamoja na ccm juu ya uamuzi wao wa kumlazimisha Jecha kufuta uchaguzi.
Mataifa yameweka macho yake kwa Magufuli...hatua yoyote atayo chukua kuzui mfano maandamano na watu wakapotea basi lawama zipo kwake hivyo ksiasa na kidiplomasia alitakiwa angalie ipepo lakini siasa za kuburuzana na kujidai kutumia nguvu kuna uwezekano akajiharibia.
Yeye alitakiwa alione hili kama majipu mengine alorithi kutoka tawala zilizo pita na moja katika mambo muhimu kuyamaliza kwa haki. Lakini kusema nitanyamaza , na kama watu wakidai haki yao hata kwa msuso basi atawashughulikia ...kuna walakini na sio busara wala sio uongozi ...sasa sio dunia ya kutumia nguvu..tumeona juzi Salva kiir akikubali pressure ya dunia...
Bado anao wajibu wa kuonesha uongozi ..kukimbia tatizo ni weakness kumwa saana
 
watachochewa wafanye vurugu watapambana na vyombo vya dola wengine wakipoteza maisha au kupata vilema vya maisha halafu viongozi wao watarudi mezani kutafuta mwafaka mwingine wajifunze katika vurugu zote zilizochochewa na wanasiasa ni kina nani walipata madhala au ni familia ya mwanasiasa gani iliathirika
Vitisho vya namna hii ndy vimetufikisha hapa ambapo hatuwezi kusimama kudai haki zetu km mtu mmoja mmoja au km Taifa.
Mnatuambia siasa ndy inaamua hatima yetu kimaendeleo, halafu wanaotakakudai siasa iwatendee haki mnawatisha.Wazanzibar hatuogopi kudai haki pale tutakapoonahaki yetu inaporwa.
 
Fyoko fyoko marufuku Zanzibar.
Kama hutaki kupiga kura baki chumbani March 20. Maalim alisema msimuone Kikwete anacheka cheka ni mbaya sana kwa Zanzibar sasa kaja kiboko ya Fyoko fyoko asiecheka Cheka! Vyombo vipo timamu kabisa barabbarra!
Hivi ugaidi maana yake ni nin?si matokeo ya mambo kama haya?
 
Wanabodi,

Baada ya lile tangazo la jana la Amiri Jeshi Mkuu wa nchi yetu, Dr. John Pombe Magufuli kumhusu yoyote atakayete fyoko fyoko popote alipo!.

Natoa wito kwa ndugu zetu Wanzibari, Chonde Chonde msilete fyoko fyoko!, upole, cheko cheko na bashasha za Jakaya Kikwete, zimetuponza Tanzania kama taifa, tukajiachia na kujisahau sana hadi kila siku kuleta fyoko fyoko na hakuna chochote ambacho kilifanyika!.

Magufuli sio Kikwete, jana katoa amri watu wasilete fyoko fyoko, ni kweli Watanzania katika umoja wetu tuitunze, tuienzi na kuithamini amani na utulivu uliopo, tusilete kabisa fyoko fyoko za aina yoyote!.

Naomba kukiri nimepandisha uzi huu kwa msipiration nilioipata kwenye mchango wa mwana jf huyu..

Magufuli atapeleka majeshi Zanzibar kwenda kusimamia amani na utulivu, ikitokea majeshi yakaua mtu, itakuwa mtu huyo ameleta fyoko fyoko!. Mtu akileta fyoko fyoko atashughulikiwa kikamilifu!. Ikitokea wengine wasi na hatia wakadhurika katika kututuliza hizo fyoko fyoko, then aliyesababisha madhara hayo ni muanzisha wa fyoko fyoko na sio mtulizaji au mdhibiti wa fyoko fyoko!.

Dawa ni moja tuu kwa Wanzanzibar, baada ya kumsikia Amiri Jeshi Mkuu akiwaonya msilete fyoko fyoko, hili sio ombi ni amri, hivyo msilete fyoko fyoko!.

Pasco
Pasco,
Katika miaka 24 ya vyama vingi CUF imeweza kujenga ''mtambo wa kupiga kura''
(election machinery) madhubuti na wa kuaminika.

Mtambo huu wa kupiga kura umeweza kushinda chaguzi zote nne bila matatizo
yoyote.

Chama kimejenga uhsiano mzuri na raia kiasi kwamba kimeweza kuchukua nafasi
ya CCM Zanzibar kwenye maeneo ambayo hawakupata kuwapo kabla.

CUF inajua faida ya kuwa na chama makini chenye akida kwani chama kama hicho
kinapendeza na kuvutia wananchi.

CUF haihitaji onyo la Rais Magufuli kuhusu amani kwani CUF imenufaika sana kwa
wanachama wake kuwa watulivi hata pale wanapopigwa na Mazombie na mali zao
kuvunjwa na kuchomwa moto.

Huu ni ukweli ambao sote tunautambua.
Msema pweke hushinda.

Rais Magufuli ana taarifa za Kijiintelijinsia nani ameunda jeshi la Mazombie.
Hii no moja ya kuwa mkuu wa nchi.

Rais Magufuli anajua kuwa CUF hawana ''thugs'' yaani wahuni wanaotembea majiani
na silaha za jadi na bunduki.

Ingekuwa Rais Magufuli si msema pweke mimi pale pale ningemuuliza,''Mheshimiwa
Rais kama kweli hutaki ''fyokofyko'' iweje hadi leo Ton Ton Macoute yaani Mazombie
wapo na silaha wanaranda mitaani na silaha na wanapiga raia na kuharibu mali zao
huko Zanzibar?''

Ningemaliza swali langu kwa kusema,'' Au Mtukufu Rais umekusudia ''fyokofyoko,''
kwa maana ya indhari kuwa CUF isithubutu kuwakabili hawa Mazombie waachiwe
wafanye watakavyo?''

CUF katika kipindi kizima cha uhai wake kimewekeza sana katika elimu ya wafuasi
wake.

Vijana wa CUF wamesoma historia na wanaijua saikoloji ya wakandamizaji kuwa
zipo namna nyingi za kuepusha shari na kumvuja nguvu dhalim nako ni kumzingira
adui na wananchi wapenda amani.

Huu ni mwamba usiweza kuvujwa kirahisi.

CCM Zanzibar haina pa kupumulia.

Ikifika mahali chama hakiwezi kushinda uchaguzi ila kwa kutegemea nguvu na vitisho
jua siku zake zinahesabika.
 
Nimeipenda!
Sasa liliobaki kuitangazia dunia kuwa sasa Zanzibar ni teka wa Tanganyika rasmi. Hatutaleta chochoko zaidi ya zile chokochoko zinazopata baraka ya watawala zinazoletwa na MAZOMBIE Kuleta chokochoko mbele ya watu wasiokuwa na huruma wala kustaarabika ni SUICIDE au wendawazimu. Tumekubali kwa shingo upande kuwa mateka wa Tanganyika, kunusuru maisha yetu. Ratio ya 49:1
BYE BYE UKOLONI KWAHERI UHURU KARIBU MAZOMBIE
 
Pasco,
Katika miaka 24 ya vyama vingi CUF imeweza kujenga ''mtambo wa kupiga kura''
(election machinery) madhubuti na wa kuaminika.

Mtambo huu wa kupiga kura umeweza kushinda chaguzi zote nne bila matatizo
yoyote.

Chama kimejenga uhsiano mzuri na raia kiasi kwamba kimeweza kuchukua nafasi
ya CCM Zanzibar kwenye maeneo ambayo hawakupata kuwapo kabla.

CUF inajua faida ya kuwa na chama makini chenye akida kwani chama kama hicho
kinapendeza na kuvutia wananchi.

CUF haihitaji onyo la Rais Magufuli kuhusu amani kwani CUF imenufaika sana kwa
wanachama wake kuwa watulivi hata pale wanapopigwa na Mazombie na mali zao
kuvunjwa na kuchomwa moto.

Huu ni ukweli ambao sote tunautambua.
Msema pweke hushinda.

Rais Magufuli ana taarifa za Kijiintelijinsia nani ameunda jeshi la Mazombie.
Hii no moja ya kuwa mkuu wa nchi.

Rais Magufuli anajua kuwa CUF hawana ''thugs'' yaani wahuni wanaotembea majiani
na silaha za jadi na bunduki.

Ingekuwa Rais Magufuli si msema pweke mimi pale pale ningemuuliza,''Mheshimiwa
Rais kama kweli hutaki ''fyokofyko'' iweje hadi leo Ton Ton Macoute yaani Mazombie
wapo na silaha wanaranda mitaani na silaha na wanapiga raia na kuharibu mali zao
huko Zanzibar?''

Ningemaliza swali langu kwa kusema,'' Au Mtukufu Rais umekusudia ''fyokofyoko,''
kwa maana ya indhari kuwa CUF isithubutu kuwakabili hawa Mazombie waachiwe
wafanye watakavyo?''

CUF katika kipindi kizima cha uhai wake kimewekeza sana katika elimu ya wafuasi
wake.

Vijana wa CUF wamesoma historia na wanaijua saikoloji ya wakandamizaji kuwa
zipo namna nyingi za kuepusha shari na kumvuja nguvu dhalim nako ni kumzingira
adui na wananchi wapenda amani.

Huu ni mwamba usiweza kuvujwa kirahisi.

CCM Zanzibar haina pa kupumulia.

Ikifika mahali chama hakiwezi kushinda uchaguzi ila kwa kutegemea nguvu na vitisho
jua siku zake zinahesabika.
Maalim karibu, ila ungenitembea hapa
BAKWATA Inamatatizo ya Uendeshaji, Jee Itaziweza Mahakama ya Kadhi?.
ungenisaidia zaidi, tukikutana kwenye siasa za Zanzibar, nawaogopa sana wale wafuasi wako, haswa akija yule muuza utumbo, mainzi yanayomfuata nyumba hayachelewi kuzonga na kuchafua hali ya hewa!.

Pasco
 
Chifu, 'kujitangaza' huko ndiko kunahalalisha ufutwaji wa matokeo na kurudia uchaguzi?
Sawa Maalim alikosea kufanya hivyo. Lakini sheria ya uchaguzi imetoa adhabu kwa kosa hilo: na adhabu hiyo siyo kufuta uchaguzi wote.
Jecha alisema kuna mambo hayakwenda sawia huko Pemba, lakini hadi sasa hakuna ushahidi kuthibitisha hilo.

Chifu, katika hili la Zanzibar, kutetea inachokifanya serikali ya CCM, ni kujitoa ufahamu.
Msikilize alivyowahi kusema Mkapa juu ya kurudiwa uchaguzi:

Halafu jiulize sasa hicho alichokisema ndicho CCM wanakisimamia sasa hivi.


Chifu, sishabikii kitendo cha CCM lakini pia nilikuwa nawaza inakuwaje kiongozi huyu wa CUF anajitangazia mwenyewe matokeo.
 
Kwa hili CCM ni ile ile-afadhali tuvunje sheria na haki za binadamu na tukose misaada-kuliko CUF kushika usukani Zenj. Wengine isomeni namba tu. Fyoko fyoko za Chaje sawa. Tume haingiliwi lakini nani asiyejua Makamu Mwenyekiti wa Tume ya ZEC alitolewa kwenye uhakiki matokeo na JESHI. Au nae alikuwa analeta fyoko fyoko?
 
Chifu, 'kujitangaza' huko ndiko kunahalalisha ufutwaji wa matokeo na kurudia uchaguzi?
Sawa Maalim alikosea kufanya hivyo. Lakini sheria ya uchaguzi imetoa adhabu kwa kosa hilo: na adhabu hiyo siyo kufuta uchaguzi wote.
Jecha alisema kuna mambo hayakwenda sawia huko Pemba, lakini hadi sasa hakuna ushahidi kuthibitisha hilo.

Chifu, katika hili la Zanzibar, kutetea inachokifanya serikali ya CCM, ni kujitoa ufahamu.
Msikilize alivyowahi kusema Mkapa juu ya kurudiwa uchaguzi:

Halafu jiulize sasa hicho alichokisema ndicho CCM wanakisimamia sasa hivi.

Aisee Mkuu asante sana kwa video hii ,halafu cha ajabu huyu sasa hivi ndie mastermind wa kinachoendelea Zanzibar ,sijui tutegemee nini
 
Pasco sijajua nini sababu ya uzi huu wakati maudhui yake yanafanana na uzi mwingine ulio ufungua ,mbona umekomalia sana hizo fyoko fyoko ?? Ni kitu gani kinakufurahisha ?? Maana unaonekana kama unakomoa watu wa upande flani
 
Maalim karibu, ila ungenitembea hapa
BAKWATA Inamatatizo ya Uendeshaji, Jee Itaziweza Mahakama ya Kadhi?.
ungenisaidia zaidi, tukikutana kwenye siasa za Zanzibar, nawaogopa sana wale wafuasi wako, haswa akija yule muuza utumbo, mainzi yanayomfuata nyumba hayachelewi kuzonga na kuchafua hali ya hewa!.

Pasco
Pasco,
Sijawa maalim mimi bado mwanafunzi.

Kwangu mimi mjadala wa BAKWATA hauna tija yoyote huwa hata kusoma
nadra.

Mimi sina wafuasi hapa Majlis ni mchangiaji ikama wanavyochangia wengine.
 
Pasco,
Katika miaka 24 ya vyama vingi CUF imeweza kujenga ''mtambo wa kupiga kura''
(election machinery) madhubuti na wa kuaminika.

Mtambo huu wa kupiga kura umeweza kushinda chaguzi zote nne bila matatizo
yoyote.

Chama kimejenga uhsiano mzuri na raia kiasi kwamba kimeweza kuchukua nafasi
ya CCM Zanzibar kwenye maeneo ambayo hawakupata kuwapo kabla.

CUF inajua faida ya kuwa na chama makini chenye akida kwani chama kama hicho
kinapendeza na kuvutia wananchi.

CUF haihitaji onyo la Rais Magufuli kuhusu amani kwani CUF imenufaika sana kwa
wanachama wake kuwa watulivi hata pale wanapopigwa na Mazombie na mali zao
kuvunjwa na kuchomwa moto.

Huu ni ukweli ambao sote tunautambua.
Msema pweke hushinda.

Rais Magufuli ana taarifa za Kijiintelijinsia nani ameunda jeshi la Mazombie.
Hii no moja ya kuwa mkuu wa nchi.

Rais Magufuli anajua kuwa CUF hawana ''thugs'' yaani wahuni wanaotembea majiani
na silaha za jadi na bunduki.

Ingekuwa Rais Magufuli si msema pweke mimi pale pale ningemuuliza,''Mheshimiwa
Rais kama kweli hutaki ''fyokofyko'' iweje hadi leo Ton Ton Macoute yaani Mazombie
wapo na silaha wanaranda mitaani na silaha na wanapiga raia na kuharibu mali zao
huko Zanzibar?''

Ningemaliza swali langu kwa kusema,'' Au Mtukufu Rais umekusudia ''fyokofyoko,''
kwa maana ya indhari kuwa CUF isithubutu kuwakabili hawa Mazombie waachiwe
wafanye watakavyo?''

CUF katika kipindi kizima cha uhai wake kimewekeza sana katika elimu ya wafuasi
wake.

Vijana wa CUF wamesoma historia na wanaijua saikoloji ya wakandamizaji kuwa
zipo namna nyingi za kuepusha shari na kumvuja nguvu dhalim nako ni kumzingira
adui na wananchi wapenda amani.

Huu ni mwamba usiweza kuvujwa kirahisi.

CCM Zanzibar haina pa kupumulia.

Ikifika mahali chama hakiwezi kushinda uchaguzi ila kwa kutegemea nguvu na vitisho
jua siku zake zinahesabika.[/QUOTEwanchi wa pemba wala hawahitaji vifaru ni wastaarabu sana


Wao ukisema unataka demokrasia ya vyama vingi wapo tayari kwenda kupiga kura .hili la fyoko fyoko si la wapemba wala wazanzibari wala cuf .

Wao ni wastarabu zaidi ya waswiss au wascandinavia

Ila mwishobwa siku nyinyi watawala ndio mnawapelekea hiyo fyoko fyoio yenu .

Mnadhilumu hakafu alizulumiwa anaambia akatwe mapanfa na zombii .mungu atawalinda wale waliodhulumiwa .asiye na dula ana mungu .
 
Back
Top Bottom