Boramaisha
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 820
- 18
Ndugu zangu wa JF,
Habari Leo limetoka na habari kuwa waziri wa utawala bora mathias chikawe amepingana na kulaumu kauli za mhe. Sitta na mhe. Dr. Mwakyembe za kutaka serikali isiilipe Dowans kwani ni kampuni ya kitapeli.
Anachosema kina mantiki kwamba wao kama mawaziri wana channels zao za kufikisha uamuzi wowote wanaoupinga ndani ya serikali badala ya kutumia vyombo vya habari.
Binafsi siwalaumu mzee sitta na dr. Mwakyembe kwani pamoja na uelewa wao wa taratibu zinazozungumzwa na chikawe lakini wameshindwa kuvumilia kukaa kimya kutokana na uzalendo kwa nchi yao. Wote wawili wanalifahamu vizuri suala la Dowans na wana uhakika kuwa ni utapeli tena mbaya zaidi unaofanywa na watanzania wenzetu. Suala la Dowans linatia uchungu tena mkubwa sana.
Kwa mtazamo wangu, ni bora viongozi wetu hao (sitta na mwakyembe) ili kulinda heshima yao kwa kujiondoa kwenye serikali inayotetea na kusimamia maamuzi ya kunyonga wananchi wao maskini.
Ndugu yangu, kwa haya tunayoyaona na kuyasikia unadhani Serikali ya Tanzania ya leo ina utaratibu wowote unaofuatwa? Kwa maoni yangu heshima ya Sitta na Mwakyembe itazidi kukua na kulindwa na wananchi endapo wataendelea kuwa kwenye vyeo walivyonavyo na kusaidia kuikosoa Serikali ipasavyo kwa mtindo huo huo wakiwamo ndani ya Serikali kuliko wakiwa nje!