Chato: Rais Samia kuongoza kumbukizi mwaka mmoja kifo cha Magufuli

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,535
8,219
Rais Samia Suluhu kuongoza kumbukizi ya mwaka mmoja wa kifo cha hayati Magufuli itakayofanyika kwenye uwanja vya Magufuli uliopo Chato, March 17 mwaka huu.

Naona ndugu kmbwembwe sasa atashiriki mwaka mmoja wa Samia..

========

Geita. Rais Samia Suluhu Hassan atashiriki na viongozi mbalimbali pamoja na wananchi wa Mkoa wa Geita katika hafla ya kumbukumbu ya mwaka mmoja wa kifo cha Rais wa Awamu ya Tano, John Magufuli itakayofanyika Machi 17, 2022 katika Uwanja wa Magufuli uliopo mjini Chato.

Baadhi ya viongozi watakaoshiriki hafla hiyo ni makamu wa Rais, Dk Philip Mpango, Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma, Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi pamoja na viongozi mbalimbali wa nchi.

Hayo yameelezwa leo Jumapili Machi 13, 2022 na Mkuu wa Mkoa wa Geita, Rosemary Senyemule wakati akiwasalimia waumini wa Kanisa la KKKT Usharika wa Upendo mjini hapa na kuwataka wajitokeze kushiriki hafla hiyo.

Senyamule amesema Serikali kwa kushirikiana na familia ya hayati Magufuli wamekusudia kufanya kumbukumbu ya mwaka mmoja ikiwa ni njia ya kumkumbuka kiongozi huyo.

Rais Magufuli alifariki dunia Machi 17 mwaka 2021 katika Hospitali ya Mzena iliyopo jijini Dar es salaam baada ya kuugua maradhi ya moyo.

Mwananchi
 
Wanasiasa wanapeleka tu unafiki wao, hivi sasa wanafanya vice versa na JPM
 
Lupaso tupa kule!😁
Lupaso ilifanyika, ila hakukuwa na utitili wa wanafiki (wanasiasa)

Ilikuwa ni ya kiroho zaidi, ikihusisha familia na ndugu wa Ben, jamii yake, na viongozi wa imani yake Ben (Katoliki)
 
Hahahahaha

Taifa letu huenda linaongoza kwa Unafiki Duniani kwa sasa

Namsoma Lemutuz muda huu anamuasa Makonda kutulia kwa kuwa sasa hivi analipia gharama za udhalimu wake wakati enzi zile ilikuwa haipiti siku hajaandika Le commandant Field Mashal sijui kanyaga twende tumechelewa sana na fyoko fyoko zingine kibao…walio madarakani wana cha kujifunza
Siku hiyo anga litachafuka unafiki wa viongozi wetu. Jana walimsema na kumtukana sana ila utashangaa sifa zitakazo mwangwa siku hiyo huwezi amini.
 
Rais Samia Suluhu kuongoza kumbukizi ya mwaka mmoja wa kifo cha hayati Magufuli itakayofanyika kwenye uwanja vya Magufuli uliopo Chato, March 17 mwaka huu.

Naona ndugu kmbwembwe sasa atashiriki mwaka mmoja wa Samia..

========

Geita. Rais Samia Suluhu Hassan atashiriki na viongozi mbalimbali pamoja na wananchi wa Mkoa wa Geita katika hafla ya kumbukumbu ya mwaka mmoja wa kifo cha Rais wa Awamu ya Tano, John Magufuli itakayofanyika Machi 17, 2022 katika Uwanja wa Magufuli uliopo mjini Chato.

Baadhi ya viongozi watakaoshiriki hafla hiyo ni makamu wa Rais, Dk Philip Mpango, Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma, Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi pamoja na viongozi mbalimbali wa nchi.

Hayo yameelezwa leo Jumapili Machi 13, 2022 na Mkuu wa Mkoa wa Geita, Rosemary Senyemule wakati akiwasalimia waumini wa Kanisa la KKKT Usharika wa Upendo mjini hapa na kuwataka wajitokeze kushiriki hafla hiyo.

Senyamule amesema Serikali kwa kushirikiana na familia ya hayati Magufuli wamekusudia kufanya kumbukumbu ya mwaka mmoja ikiwa ni njia ya kumkumbuka kiongozi huyo.

Rais Magufuli alifariki dunia Machi 17 mwaka 2021 katika Hospitali ya Mzena iliyopo jijini Dar es salaam baada ya kuugua maradhi ya moyo.

Mwananchi

Mbona ya Mkapa haifanyiki, au sukuma gang wamekuwa na nongwa sana?
 
Back
Top Bottom