HKigwangalla
JF-Expert Member
- Feb 6, 2008
- 717
- 971
Ndg zangu, nataraji kupata fursa ya kuhutubia bungeni kwenye bajeti ya ofisi ya waziri mkuu iliyowasilishwa leo, hapa tutapata fursa ya kusema lolote la kisera na hata la kijimbo, kama mlivyoshuhudia leo wachangiaji wa mwanzo walivyoanza.
Jina langu ni la 34 kwenye orodha ya wachangiaji hivyo nina matumaini makubwa ya kupata nafasi ya kuchangia endapo orodha hii itafuatwa kama ilivyo. Naomba mawazo ya nini unadhani ni nyeti sana na ungependa kisemewe na wabunge?
Nitatoa fursa kwa watu watakaonipa issue nyeti na zenye mantiki na hususan zilizokaa kitaifa zaidi. Kwa wale wa Nzega na hata Tabora kwa ujumla, mnakaribishwa kunipa issue za Kijimbo, kiwilaya ama hata kimkoa ili nizisemee bungeni.
wakatabahu,
HK.
Jina langu ni la 34 kwenye orodha ya wachangiaji hivyo nina matumaini makubwa ya kupata nafasi ya kuchangia endapo orodha hii itafuatwa kama ilivyo. Naomba mawazo ya nini unadhani ni nyeti sana na ungependa kisemewe na wabunge?
Nitatoa fursa kwa watu watakaonipa issue nyeti na zenye mantiki na hususan zilizokaa kitaifa zaidi. Kwa wale wa Nzega na hata Tabora kwa ujumla, mnakaribishwa kunipa issue za Kijimbo, kiwilaya ama hata kimkoa ili nizisemee bungeni.
wakatabahu,
HK.