Changia Mawazo kuboresha mchango wangu bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu!

HK,
Naomba niyaamini mawazo yangu kuwa kuomba ushauri hapa JF unatutania,kwa sababu
ukweli ni kuwa yapo mambo muhimu ambayo unajua ni kero kwa watanzania, lakini
siamini kama una dhamira ya dhati kweli ya kuyasema,kwani nidhamu ya woga mliyonayo
wabunge wa CCM ni tatizo,mimi labda ushauri angeomba Mpina ningempa.kati ya wabunge
ambao watanzania at least walianza kuwa na matumaini nao wewe ni mmoja wao lakini tatizo
mmetanguliza maslahi yenu na ya Chama na kutusahau watanzania.so endeleeni na njia mliyoichagua
japo nina uhakika huko mbele itawagharimu.
 
Hoya kuu iwe ni mgomo wa madktari, madhara, sababu na solution. Kama dr. Na pia mbunge, angalia nyuma, waone madaktari wenzako wanavyoteseka, waone wananchi wavyoteseka na mgomo huu, angalia jimbon kwako wapiga kura wako wanavyoteseka na huduma mbaya na mboù za afya. Acha uchama kuwa mzalendo. Iga mfn wa akina filikunjombe, zambi, shelukindo, mwakyembe, etc. Wanavyotetea zaidi wananchi na sio chama. Usiwe kama lusinde, nchemba etc. 2015 sio mbali. Huo ni mtazamo wangu tu.
CPA(T) - Kutoka kamachumu, kagera kwetu.
 
HKigwangalla na Wana JF,
Kwanza nikupongeze kwa kufikiri kwako na kurudi kwetu (Raia aka Wananchi aka Watanzania) maana sisi ndio wenye Nchi. Najua wengi wenu mnalazimishwa na Mfumo wa Chama na Serikali wa kuunga Hoja hata kama hamtaki na kukubali Hoja.
Pili, ushauri wangu kwako, kama waliotangulia wachangiaji wengine, kwa kuwa wewe ni Dokta, jikite zaidi kwenye Fani yako ya Udaktari. Kwenye sekta hiyo ya Afya kuna matatizo mengi sana ya kuongelea.
Tatu, Matatizo ya Watanzania ni mengi sana kwenye Sekta zote, Sekta za Afya, Elimu, Miundo Mbinu, Kazi na Ajira, Kilimo, Nishati na Madini.
My Take: Ushauri wa bure, uje tena utuambie umewakilisha aka umechangia nini. Kila la Kheri
Nawakilisha
 
Mhe. Mbunge,

1.I am surprised kwamba huna habari na hitaji la ku-regulate renting business in Tanzania. January Makamba alipeleka hoja binafsi kuitaka Serikali ilete mswada bungeni on Rental Housing Act. Kama alivyosema Invisible, kwa sasa huyu bwana hana meno. Keshatulizwa. You can pick it up from where he left and I can tell you, uking'ang'ana nai hii hoja utakuwa umelifanyia taifa jambo kubwa sana pengine kuliko utakavyoweza kufanya maisha yako yote.

2. Tumesoma kwenye vyombo vya habari (The East African la wiki hii, front page) kwamba kuna watanzania wenzetu (wakiwemo "influential politicians") ambao wamehongwa na makampuni yanayotafuta mafuta na gesi hapa nchini kupitia akaunti zao kwenye mabenki ya Uswisi (Gazeti linanukuu taarifa ya Switzerland National Bank). Kwa ujumla, watu hawa wachache wana jumla ya $178 million kwenye akaunti hizo. Kwa vyovyote vile fedha hizo si halali. Hata kama ni halali, suala hili linapaswa kuchunguzwa kuthibitisha hilo. After all, sheria zetu zinakataza kuwa na akaunti nje ya nchi. Correct?

3. Mbio za mwenge hazina maana. Ni matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi.

Godspeed.
 
Bajeti Mama Unaipitisha tena kwa mbwembwe na kejeli kwa wapiganaji akina Mdee then HK unakuja hapa kutuchezea akili?Hamna ushauri hapa utakaopewa zaidi ya ule muhimu uliokataa wa KUTOIPITISHA ile bajeti ya Waziri Mgimwa iliyojaam mambo mengi ya KISHETANI!!!
 
Muombe waziri mkuu aliambie taifa ni lini watoto wetu wa shule za msingi wataacha kusomea chini ya miti. Serikali inalichukuliaje suala la watu kuficha hela nje ya nchi wakati madarasa hakuna.
 
Kwa nini ofisi ya Waziri Mkuu haitoi maelezo ya mauaji ya kisiasa ambayo tuliambiwa yanachunguzwa? Hapa namaanisha yote.
 
Ikiwa mwaka jana, (1) TRA ilikusanya zaidi ya malengo, (2) serikali ilikopa zaidi ya matarajio.
(i) Kwanini fedha za maendeleo hazikufika zilikopangiwa?
(ii) Hizo fedha zilikwenda wapi?
Siungi mkono hoja hadi nipate majibu yatakayoridhisha.
 
kama ulikuwepo kwenye kipindi cha maswali na majibu asubuhi ya last wk.. sikumbuki siku NB: rejea maswali ya wenje,,, (aliuliza kuhusu sheria za kulipa pango, alitaka kujua ni kwanini sheria ya zamani isirudishwe, govt kumonitor mikataba ya mpangaji/mwenyenyumba) etc waziri alijibu.. nadhani utakuwa umeshakumbuka mpk hapo
Narubongo, unapoteza muda wako bure kurespond kwa huyu jamaa. Bungeni kwenyewe ni mtoro ndo maana wala hakumbuki kama suala la pango lilijadiliwa.
Na sababu kubwa ya kutaka asaidiwe cha kuongea Bungeni ni kuwa hana jipya na wala hana concentration awapo mjengoni. Anasubiri kusema NDIYOOO!
 
ANZA na RAS Tabora: amekaa kimaslahi zaidi, hata sidhani that post fits her, hata cjui katokea wapi, I doubt her CV! haendani na kasi ya RC wake.
Afisa Elimu Mkoa: - is a bogaz person, yupo tu kwa ajili ya kula hela za kusimamia mitihani, while Tabora is always dropping down, and amekazania ukabila tu, amejaza wasukuma wenzake tu kwenye hio idara yake, advise ifanyike reshafle yake - amefanya tbr kuwa ya mwisho katika elimu.
Mauaji ya ajabu ajabu Tabora: hakuna security huko tunaogopa kwenda Tabora, and nothing been reported and polisi are just staying idol.
Child labour: msaidie Said Nkumba, na wabunge wengine wa urambo na Uyui, watoto wenu wa Tabora, have been so exploited, hawaendi shule wapo tu kwenye tumbaku mwisho wa kila kitu wanabaki hawana elimu, wananyonywa, masikini, halafu wanabaki kulaumu kuwa wakristo wanawanyonya.
RC: aachane na tume aliyounda ya kuchunguza kwa nini watoto (waislaam)wanafail shule, and kwa nini waislaam wanabaguliwa katika fursa mbalimbali huko TBR, RC aachane na siasa za maji Taka
wewe: vipi msimamo wako kuhusu wawekezaji wa madini? vip bado unaamini maandamano ndio suluhu ya wananchi wa Nzega kuwabana resolute Mine? ila nilitegemea usingeunga mkono hotuba ya bajeti coz ulionyesha (kuandamana) that haungi mkono kampuni za madini na system zao za kinyonyaji?
 
mlifanya mnachaahidi kwa wananchi hasa kusitisha mashangingi na kuuza yaliyopo kwa sasa nitawapa mawazo mazuri sana mwaka kesho maana huwezi kupunguza gharama za serikali kwa kubakia na magari yaliyopo kwa sasa fanyeni kama kenya..kazi kwa vitendo..mawazo yamchezo hatuna onesheni seriousness cc tutawaunga mkono kwa dhati kabisa
 
Afya ni kila kitu. Huna afya njema huwezi kusoma,kufanyakazi na kuleta maendeleo. Hiyo ndio hoja mama najua wewe ni mtaalamu wa afya chukua hili lipambanue na lieleze kwa kina
 
Mh. mpe salamu waziri mkuu kunyanyaswa kwa wanasiasa na polisi sio jambo zuri ni lini litaisha?

ushauri: CCM sio mbaya bali watu wake wa sasa ndio wabaya hivyo nakushauri achana nao sema ukweli kama mpina CCM mwenzako aliyepinga bajeti bila uoga sababu CCM haikuingia kwenye kichwa chako ukapata degree bali ni akili zako wewe mwenyewe. ukweli utakurudisha bungeni 2015 hata kupitia mgombea binafsi. Hamis go go go......
 
Mimi nimemuunganisha huyu HK wa sasa kwenye kundi la kina Deo Filikunjombe, la kusimama na kuhesabiwa!. Kwa msimamo wake wa sasa, mbele ya HK wa sasa, Bashe is nothing!. CCM ni chama kongwe na rushwa is the order of the day ndani ya CCM, msomali ameishaitandaza kisawasawa, hivyo CCM sasa ndio wanamhujumu HK ili 2015 wapate ground na justification ya kumtema na kumpitisha kipenzi chao Bashe!. HK ameshaona mbali, and he banks with the people who matter most, and by that time, kusimama kuwatumikia wananchi, sio lazima kudhaminiwa na chama cha siasa, hivyo HK akishikilia msimamo wake wa kusimama na wananchi, wana Nzega, watasimama nae, Bashe na CCM yake, down the drain, watakwenda nayo!.
Pasco wa JF unachoongea ni kweli tupu, nilishamuweka huyu ndugu HK kwenye vitabu vyangu vya kumbukumbu, lakini alinichefuwa nyongo pale alipokataa kusaini Paper ya Zitto Kabwe, lakini tatizo kwangu si yeye kukataa kusaini bali sababu dhaifu alizokuja nazo hapa JF na kuanzisha thread ni kwa nini hakusaini ile paper ya Zitto Kabwe.

Utetezi wa HK ulijaa udhaifu mwingi na kibaya zaidi akajiingiza tena kwenye mtego uleule wa chama changu!! kwa kweli alinisikitisha sana, na ndio maana kwenye mgomo wa kwanza wa madaktari aliwaunga mkono vizuri madaktari wenzake, lakini mwishoni akajidhihirisha kwamba yeye ni nothing but a Coward. anyway bado nampa muda atleast nyakati nazo zitaamuwa zenyewe, still bado ana nafasi ya kutuonesha kama yuko upande wa wananchi au upande wa wakolono weusi.
 
Last edited by a moderator:
Sababu na wewe upo kwenye industry ya pamba na juzi ulikua kwenye vikao vyenu vya Stake holders pamoja na Shibuda ningekuomba uongee matatizo yanalolikumba soko la pmaba na kuwaweka katika maisha magumu wakulima ambao ndio wamewapa dhamana

Naomba utoa maoni yako na hii ishu ya Contract farming kama ina manufaa kwa Taifa au Haina. Lakini tunaona wenzetu Zambia,Malawi na Zimbabwe wanamake headline kwenye high yield ya zao la pamba sababu siasa kwao si kubwa kama Tanzania

Wakulima wana malimbikizo zaidi ya miaka mitatu hawajawahi kupata pesa zao za incentives.

Ni hayo tu
 
mpaka sasa hivi hajachangia au??maana hapa Nzega kuna maandamano ya kukupinga HK kama vipi omba Bunge la CCM litoe mwongozo
 
tuna upungufu wa madaktari wewe ukakimbilia ubunge kupata hizo milioni kumi...filikunjombe ataendelea kuwafunika wabunge vilaza wa ccm kama wewe.,misimamo ya deo inafahamika lakini wewe ni kama kinyonga yani umewasaliti hata madokta wenzio..by the way ulishawahi hata kumwandikia dawa hata mgonjwanasikia tu wewe ni dokta
 
Back
Top Bottom