Baada ya kusoma habari hii: NEC sasa kuengua CCM kwenye Gazeti la Raia Mwema nimepata mshituko kidogo. Kwa wale ambao ni wajuzi wa Sheria labda wanaweza kutusaidia kutuelewesha.
Kwenye habari hiyo Mzee Kinana anasema kwamba:
Kama deadline ya kuchukua na kurejesha fomu za kugombea kutoka ofisi za NEC imeishapita, hao wagombea wapya wa CCM wataingizwaje kwenye uchaguzi?
Ina maana vyama vya upinzani huwa havina uwezo wa kuteua wagombea wapya ili kujaza nafasi ya mgombea aliyeenguliwa?
Sheria ya Uchaguzi inasemaje iwapo mgombea akiwekewa pingamizi na likakubaliwa, je, chama chake kinaruhusiwa kuteua mgombea mwingine?
Kwenye habari hiyo Mzee Kinana anasema kwamba:
Mwenyekiti wa Kampeni za CCM, Abdulraham Kinana alisema uamuzi wowote wa NEC ni wa mwisho kisheria na kwamba kama hali itakuwa hivyo chama chake kitarejea kwenye taratibu zake ili kuteua wagombea wengine kuziba pengo la watakaoenguliwa.
Ni vizuri zaidi kusubiri matokeo ya Tume kuhusu pingamizi hizo, lakini taratibu zinafahamika kama katika maeneo ambayo wagombea wetu walitangazwa kupita bila kupingwa watarejeshewa wapinzani, maana yake watabaki kuwa wagombea wetu.
Lakini ikitokea wagombea wetu waliowekewa pingamizi wakaenguliwa Tume, tutumia vikao vyetu kwa mujibu wa taratibu za CCM kuteua mgombea mwingine kutoka kwenye orodha ya wagombea waliojitokeza kwenye kura za maoni, alisema Kinana.
Source: Raia Mwema - NEC sasa kuengua CCM
Kama deadline ya kuchukua na kurejesha fomu za kugombea kutoka ofisi za NEC imeishapita, hao wagombea wapya wa CCM wataingizwaje kwenye uchaguzi?
Ina maana vyama vya upinzani huwa havina uwezo wa kuteua wagombea wapya ili kujaza nafasi ya mgombea aliyeenguliwa?
Sheria ya Uchaguzi inasemaje iwapo mgombea akiwekewa pingamizi na likakubaliwa, je, chama chake kinaruhusiwa kuteua mgombea mwingine?