Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,789
- 218,420
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila leo Jumatatu Desemba 18, 2023 amesema kama kuna mkazi wa Dar es Salaam analalamika kuwapo kwa foleni katika jiji hilo, ahamie vijinini.
“Kwa yeyote anayeendelea kulalamika mkoa huu labda una mambo mengi ikiwemo foleni, kuna vijiji vingi sana bado havijajaa wanaweza kuhamia huko.
“Mkoa wa Dar es Salaam upo salama na hasa kwa wakati huu wakati wa kujiandaa na sherehe mbalimbali, kila mwaka wanaimarisha ulinzi lakini mwaka huu umeimarishwa zaidi,” amesema RC Chalamila.
Hayo ameyazungumza leo katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya ustawi wa jamii na miaka 50 ya Chuo cha Ustawi wa Jamii yaliyofanyika jijini hapo.