CHAI Day 5 Feb 2011 Dar: Kujadili fursa katika Kilimo na ufugaji

na sisi tunashukuru wote waliohudhuria..
kilichobaki ni kutekeleza tuliyokubaliana
 
Habari za Saa hizi

Nilikuwa naomba kuuliza sisi tunaoishi nje tunaruhusiwa kujiunga na hii fursa ya kuwa na shamba la pamoja.Kama tunaruhusiwa naomba mnipe taratibu za kujiunga.

Nimefurahishwa na jambo hili.

Shukran
 
Matepwende, Karibu sana...!!! Naamini inawezekana nawe kujiunga katika shamba la pamoja, kwa sasa linatafutwa shamba ambalo tutaweza kukubaliana aina ya mazao ya kuzalisha na kugawana shamba hilo. Unaweza kum-PM Kanyagio au Malila ili uweze kuingia katika hiyo list.
 
Jamani salama nataka kujoin kwenye hii kitu nipeni procedure

Kwa faida ya wengi ni kwamba,jamii farm inaweza kuwa faida sana kwa wengi wetu ambao tumeajiriwa. Nitatoa mifano hai ya kile tunachofanya. Tumetafuta na kupata maeneo makubwa mazuri,kisha tunagawana kila mtu kwa kadri ya nguvu zake. Tuna mashamba mkoani na mkuranga. Mkoani tunaotesha miti ya mbao, tuna block nyingi zenye watu kadhaa,tumeanzisha maeneo mawili ya ufugaji na kilimo Mkuranga, hapo tumeanza kupanda miembe kila mtu na kisehemu chake. Sasa kwa nini tunaita jamii, mtu mmoja miongoni mwetu anapokwenda shamba ( Mkuranga au mkoani) anatoa taarifa mapema kupitia mail yetu ya group. Akifika huko anakagua mashamba yote, na kama ni kupanda anahakikisha vijana wamepanda mashamba yote, anatoa taarifa. Hata mbegu tunanunua pamoja, usafirishaji pamoja na vijana wetu wanafanya kazi zao pamoja ktk mashamba yetu.

Baada ya kuona tumeweza, sasa tumeomba shamba kubwa zaidi kijiji fulani, na bado tunatafuta shamba/pori lenye mto ili tuanzishe mji kabisa hapo wa wawekezaji wazawa vijana. Lengo, ni kuwa na kampuni ya kilimo anuai ya kizawa, kwa taarifa tu, ni kwamba tunaendelea na ujenzi wa ofisi yetu pale Mkuranga. Tulinunua eneo la eka 8 ili iwe base yetu,kisha ndio tuanze mambo. Mungu akitujalia mwezi ujao tunaanza na mbuzi wa maziwa.

Namna ya kujiunga na kundi hili ( lote liko linked), hakuna masharti. Cha msingi au sifa muhimu ni team spirit kama unayo. Hakuna kiingilio. Tuma mail yako kwa pm ili nikupeleke kwa moderator wa kundi ili uwe linked up.
 
wanandugu nawashukuru wote walioweza kufika kwenye mkutano.. kwa kweli ulikuwa mkutano mzuri. naomba mniwie radhi kwa kuchelewa kuleta muhtasari ila naahidi kuuwakilishi si muda mrefu ujao.

Pamoja na hayo nawashukuru wote ambao walinipigia simu, PM au emai kuniambia kuwa hawatahudhuria. lakini nasikitika sana kuwa kuna watu wali-confirm kuja lakini hawakutoa taarifa kuwa hawaji.. sasa ndugu zangu naomba tujifunze kutoa taarifa tunapohairisha maanake isingekuwa uelewa wa wenye hoteli wangetu-charge hata wale ambao hawakufika (tulikuwa tumeweka order za watu 35 ila tukawa 23). Watu wa hotel walituelewa na wakawa flexible (baada ya kuwaomba) hivyo hawakutu-charge.

kutotoa taharifa kweli ni vibaya na mimi kama mmoja wapo naomba mnisamehe. Kuna mtu nilimwomba aniwakilishe na pesa nikamwachia pamoja na minutes za kikao nikasafiri, niliporudi akaniambia hakuja, na kwa kweli hakuwa na sababu iliyoniingia akilini. Nashukuru mlifanikisha vizuri na nawapa hongera naomba niwe nanyi msiniache tafadhali.
 
Ndg. Kanyagio au Malila,

Tafadhari tujulishe mara usomapo hapa lini tutakuwa na Chai Day ya kufungua mwaka 2012?

JF Marker anathibitisha kuhudhuria.
 
Ndg. Kanyagio au Malila,

Tafadhari tujulishe mara usomapo hapa lini tutakuwa na Chai Day ya kufungua mwaka 2012?

JF Marker anathibitisha kuhudhuria.

Asante mkuu kwa kuwa aware,

Mkutano utakuwepo january 14,2012, naamini ukumbi utakuwa pale pale Lunch time, mpaka sasa nimepata uthibitisho wa wadau wanne. Naamini wengi watahudhuria kutokea kwa group yetu. Kwa ye yote anayetaka kuja anakaribishwa, mchango ni gharama za ukumbi kama tutahitaji. Nitawasiliana na LTH nione gharama zitakuwaje.

Agenda/Mada za mkutano.

1; Mafanikio ya 2011
2; Changamoto za 2011
3; Miradi mipya tunayoweza kuifanya
4; Tulipofikia na nini kiongezwe ktk mipango yetu ili twende kisasa zaidi
5; Tutafanya nini 2012 and beyond that.
Hizo ndio mada kuu za siku hiyo.

Napendekeza muda uwe saa kumi juu ya alama.

Malila
 
malila upo sahihi, kikubwa ni watu kuanza ku-confirm. Itapendeza sana kama wale waliohudhuria last time waweze kuhudhuria!!
 
Karibu tujumuike pamoja, naamini utafurahia kukutana na wajasiriamali chipukizi.
malila, hongereni sana kwa hilo na ninampongeza aliyetoa chachu ya wazo hilo. Napenda kutoa taarifa kuwa na mimi nihitaji kujiunga. Nitatuma mchango wangu kushiriki.
 
malila, hongereni sana kwa hilo na ninampongeza aliyetoa chachu ya wazo hilo. Napenda kutoa taarifa kuwa na mimi nihitaji kujiunga. Nitatuma mchango wangu kushiriki.

Shadya unakaribishwa sana,
Ni tarehe 14january2012. Tahadhari, siku hiyo tunakunywa chai tu ili tuweze kujadiliana vizuri, maji ya mende huwa tunajizuia kwa masaa kadhaa. Mada zikiisha basi kila mtu ruksa kula kile roho inapenda.
 
Malila na ndugu wengine, inabidi kutoa mfumo bora wa watu kufanya confirmation ili kuzuia watu wanao-confirm mtandaoni then wanapotea kabisa hawaonekani na hawatoi udhuru.
So cha kufanya ni kufanya makisio ya gharama na kujua kila mtu atoe ngapi. na ukumbi utafutwe kulingana na idadi ya watu watakaokuja ili kuondoa hasara au waandaji kukabwa mashati na wenye hoteli.
so mtu akonfrm kwa kutoa participation fee.
nawasilisha!!
 
Malila na ndugu wengine, inabidi kutoa mfumo bora wa watu kufanya confirmation ili kuzuia watu wanao-confirm mtandaoni then wanapotea kabisa hawaonekani na hawatoi udhuru.
So cha kufanya ni kufanya makisio ya gharama na kujua kila mtu atoe ngapi. na ukumbi utafutwe kulingana na idadi ya watu watakaokuja ili kuondoa hasara au waandaji kukabwa mashati na wenye hoteli.
so mtu akonfrm kwa kutoa participation fee.
nawasilisha!!

Kikao kitakuwepo kama kilivyopangwa,wapo wanaona umuhimu wa kukutana, tukifika pale Lunch Time Hotel tutaendelea na agenda zetu. Muda ni saa kumi kamili jioni, jiandae na tsh 20,000/ kwa ajili ya mahitaji yako mwenyewe.
 
Mwakani 2013, tutakuwa na chai day tena kwa ajili ya mrejesho wa kilivhofanyika, mafanikio, changamoto na nini tunatakiwa kufanya. Kwa wasiojua nini kinafanyika huko, mnaweza kuuliza na kueleweshwa, kwa wadau wa chai day subirini tupange tarehe ya kukutana na ukumbi, kisha tutaweka hewani.

Kwa ufupi siku hii huwa tunakutana, tunakunywa chai huku tukiongea masuala ya uchumi. Vinywaji vikali havifai kwa sababu wengine wakishapitisha kamoja tu, basi frequency zinahama. Baada ya chai huwa tunaendelea na nyama choma kwa kadri yako mwenyewe.
 
Back
Top Bottom