CHADEMA wapinga muswada wa mchakato wa katiba mpya

Katiba si ya Kikwete, nimeusoma muswada umempa rais madaraka makubwa mno, yeye ndiye anateua na kuwathibitisha wajumbe wa tume, yeye anaanda hadidu za rejea anapokea mapendekezo ya tume na kuyakubali au kuyakataa.

Kwenye bunge la katiba ukiacha wabunge na wawakilishi ambao ni wajumbe yeye atayathibitisha majina mengine 116,
baadae yeye ndiye anaitisha bunge la katiba ambalo litawajibika kwake.

Walichoongeza kwenye huu mswada mpya ni kwamba kila wakati atashauriana na rais wa Zanzibar. Namwambia kwamba hii katiba ni ya watanzania si ya ukoo wa Mrisho muda wake ukiisha ataondoka na kuiacha, kwa hiyo atuache tuamue wenyewe.
 
kwa kuwa katiba ni dira ya nchi, na nchi ni mali ya wananchi, ccm haina haki ya kuhodhi utengenezaji wa dira ya nchi hata kwa kura, wakijaribu, huwa siwaungi mkono sasa nitajenga uadui nao!! hawataifaidi huruma yangu ikiwafika saa mfano wa gadafi, kwa kuwa wamenilenga kwa bunduki, mimi nawafyatulia kabla yao, wasijesema sikuwaonya kabla!!!
 
Naunga mkono hoja. Naona CCM na serikali yake hawajajifunza cho chote kutokana na mapinduzi yanazoendelea Africa ya kaskazini na Uarabuni kwa ujumla. Sikio la kufa alisikii dawa.

Tumechoka na mazingaombwe ya CCM, kilicho baki ni kuingia mitaani na kudai haki zetu, tumevumila kiasi cha kutosha sasa basi. Wananchi wote, majeshi yote, wanafunzi, wafanyakazi wote, machinga wote tuanze maadamano na migomo nchi nzima.

Mungu yuko upande wetu, tutashinda. Mungu ibariki Tanzania.
 
Kikwete na serikali yake haina haja ya kufanikisha uandishi wa katiba mpya na ndio maana inawajaribu wananchi ili damu imwagike! !Hata Gadaffi alijiamini hivyo hivyo mwishowe akaopolewa toka kwenye mfereji wa mavi!!
 
Hivi huu mchakato wa katiba mpya una timeline au ndiyo danadana hizi zitaendelea mpaka 2020?
 
Hizi habari za kujadili mambo mazito kama haya huku wengi wetu tukiwa tumejilaza vitandani tunadanganyana tukutane cjui mwembe chai wakati huo mi nipo mbeya kweli tutafika kwa stahili ya namna hii mbaya zaidi tunaongelea nyuma ya pazia mi naona kuwepo na njia mbadala mbali na hii lasi hivyo hz kelele zitahishia humu humu.
 
Hizi habari za kujadili mambo mazito kama haya huku wengi wetu tukiwa tumejilaza vitandani tunadanganyana tukutane cjui mwembe chai wakati huo mi nipo mbeya kweli tutafika kwa stahili ya namna hii mbaya zaidi tunaongelea nyuma ya pazia mi naona kuwepo na njia mbadala mbali na hii lasi hivyo hz kelele zitahishia humu humu.
Ushauri wangu tufanye kama nchi zingine zinavyofanya na kufanikisha, wanaharakati wajitokeze (ukweli hatuwezi wote kuwa wanaharakati wengine tunachangia tu kwa hali na mali) watafute ofisi tofauti na ofisi zao iwe spesho kwa kupokea mawazo na ushauri toka kwa wananchi, hiyo ofisi au sehemu itakuwa pahala pazuri pa kuanzia kukutana na kupeana mikakati.
 
hawa hawana tofauti na yule mfadhili wao aliye uwawa juzi na wananchi wake kama kibaka wa manzese.bado wanadhani wanaweza wakafanya chochote na watanzania wenye akili tukakaa kimya.bongo zao tayari zimejam.nyanja zote kuanzia uchumi,biashara,na sasa siasa imewashinda.
 
Muswada wa Katiba mpya: CHADEMA wacharuka
• Wasema serikali imepuuza wananchi

SIKU moja baada ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria ilipomtimua katika kikao Waziri wa Wizara ya Sheria na Katiba, Celina Kombani, kutokana na hatua yake ya kuwasilisha muswada mpya badala ya ule wenye marekebisho kama ilivyoagizwa na Bunge, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetangaza rasmi kutokuunga mkono muswada wa mchakato wa katiba mpya, kwa maelezo kuwa huu ulioletwa sasa una viepengele tata, na hauzingatii maoni ya wananchi walioukataa mara ya kwanza.

Chama hicho kimewataka wananchi nao kuukataa, na kujitokeza hadharani kuainisha upungufu watakaouona kwenye muswada huo, ili hatimaye katiba itakayopatikana itokane na nguvu ya wananchi, si mabavu na hila ya serikali.

Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, alitoa msimamo huo jana jijini Dar es Salaam, alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu muswada huo, unaotarajiwa kusomwa bungeni kwa mara ya pili na ya tatu, baada ya kuchapishwa kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza.
Dk. Slaa alisema katika muswada huo kuna vipengele ambavyo vinampa rais madaraka makubwa, badala ya kuyapunguza, kwani katiba inapaswa kuwa mali ya wananchi na si ya rais.

"Inaonekana rais ameongezewa madaraka katika muswada mpya. Hali hii ni hatari," alisema, na kuongeza kuwa moja ya mambo yalinayohojiwa katika katiba ya sasa ni madaraka makubwa ya rais, ambayo mara nyingi yamekuwa yakitumika vibaya.

Alisema muswada huu bado umeshindwa kuifanya Tume ya Taifa ya Uchaguzi iwe huru, kinyume cha matarajio ya wengi.
Aliongeza kuwa CHADEMA itaendelea kupinga muswada huo hadi utakaporekebishwa na kuunda tume hiyo kama chombo cha kitaifa ambacho si cha kiserikali, kitakachopewa uhuru, wataalamu na fedha za kutosha.

"Katika muswada huu tumeona kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi haiko huru, japo kipengele cha 10 kinaeleza kuwa tume itakuwa na mamlaka na uhuru kwa kadiri itakavyokuwa muhimu kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu. Ukweli ni kwamba kipengele hiki kinadanganya wahisani wa nje na hakipo kiuhalisia," alisema Dk. Slaa.

Badala yake CHADEMA kinataka mabaraza ya katiba yaundwe na wananchi na si tume. Alisema kifungu cha 18 kinaeleza kuwa baada ya tume kumaliza kazi yake, itawasilisha ripoti yake kwa rais wa Tanzania na wa Zanzibar. Katika hilo alieleza kuwa katiba haina uhusiano na sera, na kwamba serikali isiyo makini ndiyo inayofanya mambo yake namna hiyo kwa kuwagawa wananchi.

"Kwa kuwa ni mara ya pili kwa mchakato huu kuendelea, tutasubiri mpaka muswada upelekwe bungeni, vinginevyo tutakwenda kwa wananchi bila kumng'unya maneno.
"Tutakapokwenda kwa wananchi, tunaiomba serikali kuwa tulivu, iunde mchakato utakaokubalika, kwa kuurudisha kwenye kamati, maana kuendelea na huu uliopo ni sawa na ufisadi, na ni vema serikali nayo ikawa tayari kusikiliza maoni ya wananchi," alisema.
 
CCM kimekuwa chama cha ajabu sana. Wanadhani wanaweza kutumia ujinga wao kuwafanya wananchi wote wajinga, hawaelewi kwamba zama za ujinga zimeshapita. Nadhani wana hamu sana ya kuona damu inamwagika ili wafurahi.
 
Kwa nini serikali hii inatafuta kwa kwa makusudi kuweka historia ya machafuko yatayoishangaza dunia? Kwanini wanafanya mizaha na subira yetu? Tupo kwenye hali mbaya kiuchumi na bado wanachezea political stability!

Kwanini vyombo vya usalama havitoi tahadhari kwa serikali? Tunataka katiba mpya kabla ya 2013 na inawezekana.ilipofikia busara na subira ya Dr slaa ndio vinavyotuliza wananchi, sasa kama mnataka kuwajua watanzania,kuwajua kuwa walimchagua Dr slaa 2010 na ndiye mtu wanaye muamini kwasasa,wasiutoe huu muswada!!wapuuzi wachache wanaipeleka nchi shimoni,.

Haikubaliki!!!
 
Hii serikali ya JK inaliandalia taifa ili future ya namna gani?

Hivi mpaka leo bado wapo watu wanaamini katiba ni lazima iwapendelee wao wakiwa madarakani...! Mbona CCM nawaona kama vipofu kwasababu si muda mrefu wataondoka madarakani na wataingia wapinzani nao watatunyasa wananchi na katiba hiyo mbovu. Amkeni CCM na tambueni katiba si ya serikali bali ni ya watanzania.

Napinga mswaada utakaompa RAIS maamuzi makubwa kwa jinsi gani tutunge katiba; nitakubaliana na katiba mpya itakayoundwa kwa uhuru na hata kama itampa RAIS madaraka makubwa kuliko aliyonayo sasa!

Nilidhani Dowans inaweza kuwa chanzo cha hasira za umma kumbe hawa wajinga wanaleta na hili la katiba. Mungu tufikishe salama katika Tz yenye neema.
 
Katibu mkuu wa Chadema Dr Wilbrod Slaa amesema Chadema haitambui mswada wa mchakato wa katiba mpya kwani umechakachuliwa na bado umempa madaraka makubwa Rais kuingilia mchakato huo.Dr Slaa ameonya kama serikali haitasalimu amri na kubadilisha basi Chadema itawaongoza watanzania kuupinga kwa njia zote itakazoona zinafaa. SOURCE-ITV SAA 2 HABARI
Kwa hili la katiba Watanzania wote tushikamane maana ndio njia pekee itakayoweka msingi wa kuweza kujiletea mabadiliko ya kisiasa bila kumwaga damu. Damu iliyomwagika Igunga na Arusha na uporaji wa "kura" ni tunda la katiba tuliyonayo sasa.
 
Hizi habari za kujadili mambo mazito kama haya huku wengi wetu tukiwa tumejilaza vitandani tunadanganyana tukutane cjui mwembe chai wakati huo mi nipo mbeya kweli tutafika kwa stahili ya namna hii mbaya zaidi tunaongelea nyuma ya pazia mi naona kuwepo na njia mbadala mbali na hii lasi hivyo hz kelele zitahishia humu humu.
You have a valid point..I believe that it is time to stand out to be counted in support of things which MATTERS. What are you proposing that we Du?
 
Navyowajua Pro-CDM JF walivyokuwa pumba kwanye mambo ya kisheria hata mswada hawajaupitia lakini nao wanapinga tu kwa sababu a loser Dr Slaa kasema
 
Hivi hii nchi ni ya ccm au ya Watanzania?,mbona mbaziba macho na masikio yenu juu ya kile tunachokitaka Watanzania?Au mpaka tukong'otane ndio tutaheshimiana?Kwa nini mnataka tufanye mbaya?Katiba ni haki yetu,Tanzania ni mali yetu Watanzania pmj na vilivyomo ndani nnaomba nyie watawala mtuelewe hivyo.Tunarudia rudia na kupiga kelele kila siku kama sie ni"KASUKU"
 
Hivi hii nchi ni ya ccm au ya Watanzania?,mbona mbaziba macho na masikio yenu juu ya kile tunachokitaka Watanzania?Au mpaka tukong'otane ndio tutaheshimiana?Kwa nini mnataka tufanye mbaya?Katiba ni haki yetu,Tanzania ni mali yetu Watanzania pmj na vilivyomo ndani nnaomba nyie watawala mtuelewe hivyo.Tunarudia rudia na kupiga kelele kila siku kama sie ni"KASUKU"
Wewe utakuwa ni mhutu. Unadalili za mauaji mauaji.
 
Tuanze mapema kupinga kwa vitendo mpaka wakubali hii si nchi ya ccm ni yetu wananchi,alutaaa continua!
 
Back
Top Bottom