nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Muswada wa Katiba mpya
Waandishi Wetu
Viongozi wa CHADEMA kwenye maandamano
HALI ya kujaribu kupimana ubavu kati ya vyombo vya dola na baadhi ya wanasiasa, wakiwamo wabunge kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na baadhi ya wanaharakati, kupitia Jukwaa la Katiba, kwa sasa ni dhahiri, Raia Mwema, limejiridhisha.
Kusomwa kwa mara ya pili kwa Muswada wa Mabadiliko ya Katiba kulikofanywa na Serikali kupitia kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani, bungeni wiki hii, na uamuzi wa wabunge wa CHADEMA, kususia kushiriki mjadala wa muswada huo bungeni, ni matukio yanayobainisha mvutano huo wa dhahiri, wenye mwelekeo wa kupimana ubavu.
Lakini wakati hali hiyo ikijitokeza, Raia Mwema, imepewa taarifa kuwa wapo baadhi ya Watanzania wamejiandaa kufikisha suala hili katika Mahakama, kupinga muswada wa sasa wa mabadiliko ya Katiba kuendelea na hatua nyingine zinazofuatiwa ikiwa ni pamoja na kutiwa saini ili uwe rasmi sheria.
"Tunakwenda kupinga muswada huu katika Mahakama, ikibidi kuzuia kabisa mchakato huu hadi pale Serikali itakapokuwa tayari kuanza upya. Lengo letu ni kuweka mazingira ya usawa katika kufikia Katiba mpya," alisema mwanasiasa mmoja ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) mwenye msimamo mkali.
Tangu kuanza kwa vikao vya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, siku kadhaa kabla ya kuanza kwa mkutano wa sasa wa Bunge, mjini Dodoma, dalili za mvutano huu zilianza kujitokeza na msingi wa hoja ukiwa madaraka makubwa ya Rais, katika muswada huo.
Kati ya watu walioko kwenye orodha ya kutilia shaka madaraka hayo makubwa ya Rais katika muswada huo ni pamoja na wengine ambao si wanasiasa wala wanaharakati, bali ni wanataalamu wa sheria, wakiwamo wanasheria kutoka Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS).
Baadhi ya hao wamependekeza kuwa katika muswada huo, Rais asipewe jukumu la kupendekeza au kutunga hadidu za rejea na kwamba hadidu hizo ziwekwe moja kwa moja ndani ya muswada, ili kuondoa uwezekano wa kuzalishwa kwa Katiba yenye kukidhi utashi binafsi wa Rais ambao unaweza kupandikizwa kupitia fursa anayopewa ya kutunga hadidu za rejea.
Hata hivyo, kwa upande wake, Serikali imekuwa ikijieleza kuzingatia maoni hayo ya wadau mbalimbali na kutahadharisha kuwa si maoni yote yaliyozingatiwa. Baadhi ya wabunge pia wamependekeza hadidu hizo rejea asiachwe Rais kuzitunga.
Ni kutokana na mapendekezo hayo na mengine, shinikizo linajengwa kuwa ni lazima muswada huo usomwe kwa mara ya kwanza ili kuwapa nafasi zaidi Watanzania kuongezea maoni yao.
Lakini hali inazidi kuwa tete kwa sasa kutokana na Serikali kuendelea kuchukua msimamo wa kusoma kwa mara ya pili muswada huo, kinyume cha matakwa ya baadhi ya wanaharakati na wabunge wa CHADEMA, ambao wanataka usomwe kwa mara ya kwanza kwa sababu haukushirikisha wananchi kwa kiasi cha kutosha.
Kwa upande mwingine, taarifa zilizolifikia gazeti hili ambazo pia zimebainishwa na Mbunge wa Wawi (CUF), Hamad Rashid Mohamed, muswada huu unapopitishwa na Bunge, kuna maombo maalumu yaliyowasilishwa kwa Rais Kikwete, ili kwanza kabla ya kufikishwa kwake kwa ajili ya kutiwa saini, utapelekwa tena kwa Watanzania, ili kuoongezea nguvu.
Wanaharakati wanaoungana na wabunge wa CHADEMA kuwa na msimamo unaofanana ni pamoja na wanaoujumishwa katika Jukwaa la Katiba.
Jana Jumanne, wabunge wa CHADEMA walikutana kuweka msimamo wa pamoja, na kati ya malengo yao yatakayofuata ni kuungana na wanaharakati wengine kufanya maandamano yasiyo na kikomo nchi nzima, hali inayoviweka katika tahadhari vyombo vya dola nchini.
Katika kile kinachotajwa kuwa ni hali ya mvutano na kutazamana kwa hadhari kubwa, kati ya wanasiasa na vyombo vya dola, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Saidi Mwema, ameweka bayana kuwa jeshi hilo halitavumilia hali yoyote ya uvunjifu wa amani.
"Moja ya jukumu la polisi popote duniani ni kuhakikisha usalama na amani pamoja na kulinda maisha ya raia na mali zao. Ili Jeshi la Polisi lifanikishe jukumu lake hili, ni muhimu sana kwa raia kuenzi amani na usalama uliopo nchini.
"Sababu ya msingi ya raia kuenzi amani, usalama na utulivu uliopo nchini ni rahisi kuona kwa sababu; amani ya nchi ikiharibika ni kama mfano wa chombo kinachozama baharini, hakuna anayepona, wote wanakwenda na maji. Ikiwepo bahati, ni wachache tu wanaonusurika.
"Itakuwa si hekima kwa nchi yetu kuona sheria inavunjwa na watu wachache, kwa kisingizio cha siasa, hasira kali ama jazba bila kuchukuliwa hatua. Shughuli za siasa ni kitu kimoja na fujo ama vurugu za jazba ni kitu kingine.
"Upo umuhimu wa kutenganisha mambo hayo mawili na hapana budi mamlaka za kisheria ziheshimiwe na watu wote bila kujali itikadi zao kisiasa au kijamii.
"Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, walipitisha sheria ya vyama vya siasa na sheria ya Jeshi la Polisi, sheria hizo zimeweka utaratibu na miongozo ya kufuata katika kuratibu mikusanyiko mbalimbali ikiwamo maandamano na mikutano ya hadhara.
"Haki, wajibu na utaratibu wa kufuatwa na vyama vya siasa pamoja na Jeshi la Polisi kupewa taarifa ya mikusanyiko imefafanuliwa pia katika sheria hizo. Kwa hali hiyo ifahamike wazi kwamba Jeshi la Polisi halina nia mbaya ya kuzuia mikusanyiko ama maandamano," awesema IGP Mwema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari.
Tayari baadhi ya maeneo ya miji mikuu na yenye ushawishi wa kisiasa yamekumbwa na vurugu kubwa zilizoisukuma Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani, kutoa tamko Bungeni kuelezea hali hiyo, ambayo inazidi kuashiria kuwapo kwa vuguvugu kali dhidi ya serikali.
Waandishi Wetu
Viongozi wa CHADEMA kwenye maandamano
HALI ya kujaribu kupimana ubavu kati ya vyombo vya dola na baadhi ya wanasiasa, wakiwamo wabunge kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na baadhi ya wanaharakati, kupitia Jukwaa la Katiba, kwa sasa ni dhahiri, Raia Mwema, limejiridhisha.
Kusomwa kwa mara ya pili kwa Muswada wa Mabadiliko ya Katiba kulikofanywa na Serikali kupitia kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani, bungeni wiki hii, na uamuzi wa wabunge wa CHADEMA, kususia kushiriki mjadala wa muswada huo bungeni, ni matukio yanayobainisha mvutano huo wa dhahiri, wenye mwelekeo wa kupimana ubavu.
Lakini wakati hali hiyo ikijitokeza, Raia Mwema, imepewa taarifa kuwa wapo baadhi ya Watanzania wamejiandaa kufikisha suala hili katika Mahakama, kupinga muswada wa sasa wa mabadiliko ya Katiba kuendelea na hatua nyingine zinazofuatiwa ikiwa ni pamoja na kutiwa saini ili uwe rasmi sheria.
"Tunakwenda kupinga muswada huu katika Mahakama, ikibidi kuzuia kabisa mchakato huu hadi pale Serikali itakapokuwa tayari kuanza upya. Lengo letu ni kuweka mazingira ya usawa katika kufikia Katiba mpya," alisema mwanasiasa mmoja ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) mwenye msimamo mkali.
Tangu kuanza kwa vikao vya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, siku kadhaa kabla ya kuanza kwa mkutano wa sasa wa Bunge, mjini Dodoma, dalili za mvutano huu zilianza kujitokeza na msingi wa hoja ukiwa madaraka makubwa ya Rais, katika muswada huo.
Kati ya watu walioko kwenye orodha ya kutilia shaka madaraka hayo makubwa ya Rais katika muswada huo ni pamoja na wengine ambao si wanasiasa wala wanaharakati, bali ni wanataalamu wa sheria, wakiwamo wanasheria kutoka Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS).
Baadhi ya hao wamependekeza kuwa katika muswada huo, Rais asipewe jukumu la kupendekeza au kutunga hadidu za rejea na kwamba hadidu hizo ziwekwe moja kwa moja ndani ya muswada, ili kuondoa uwezekano wa kuzalishwa kwa Katiba yenye kukidhi utashi binafsi wa Rais ambao unaweza kupandikizwa kupitia fursa anayopewa ya kutunga hadidu za rejea.
Hata hivyo, kwa upande wake, Serikali imekuwa ikijieleza kuzingatia maoni hayo ya wadau mbalimbali na kutahadharisha kuwa si maoni yote yaliyozingatiwa. Baadhi ya wabunge pia wamependekeza hadidu hizo rejea asiachwe Rais kuzitunga.
Ni kutokana na mapendekezo hayo na mengine, shinikizo linajengwa kuwa ni lazima muswada huo usomwe kwa mara ya kwanza ili kuwapa nafasi zaidi Watanzania kuongezea maoni yao.
Lakini hali inazidi kuwa tete kwa sasa kutokana na Serikali kuendelea kuchukua msimamo wa kusoma kwa mara ya pili muswada huo, kinyume cha matakwa ya baadhi ya wanaharakati na wabunge wa CHADEMA, ambao wanataka usomwe kwa mara ya kwanza kwa sababu haukushirikisha wananchi kwa kiasi cha kutosha.
Kwa upande mwingine, taarifa zilizolifikia gazeti hili ambazo pia zimebainishwa na Mbunge wa Wawi (CUF), Hamad Rashid Mohamed, muswada huu unapopitishwa na Bunge, kuna maombo maalumu yaliyowasilishwa kwa Rais Kikwete, ili kwanza kabla ya kufikishwa kwake kwa ajili ya kutiwa saini, utapelekwa tena kwa Watanzania, ili kuoongezea nguvu.
Wanaharakati wanaoungana na wabunge wa CHADEMA kuwa na msimamo unaofanana ni pamoja na wanaoujumishwa katika Jukwaa la Katiba.
Jana Jumanne, wabunge wa CHADEMA walikutana kuweka msimamo wa pamoja, na kati ya malengo yao yatakayofuata ni kuungana na wanaharakati wengine kufanya maandamano yasiyo na kikomo nchi nzima, hali inayoviweka katika tahadhari vyombo vya dola nchini.
Katika kile kinachotajwa kuwa ni hali ya mvutano na kutazamana kwa hadhari kubwa, kati ya wanasiasa na vyombo vya dola, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Saidi Mwema, ameweka bayana kuwa jeshi hilo halitavumilia hali yoyote ya uvunjifu wa amani.
"Moja ya jukumu la polisi popote duniani ni kuhakikisha usalama na amani pamoja na kulinda maisha ya raia na mali zao. Ili Jeshi la Polisi lifanikishe jukumu lake hili, ni muhimu sana kwa raia kuenzi amani na usalama uliopo nchini.
"Sababu ya msingi ya raia kuenzi amani, usalama na utulivu uliopo nchini ni rahisi kuona kwa sababu; amani ya nchi ikiharibika ni kama mfano wa chombo kinachozama baharini, hakuna anayepona, wote wanakwenda na maji. Ikiwepo bahati, ni wachache tu wanaonusurika.
"Itakuwa si hekima kwa nchi yetu kuona sheria inavunjwa na watu wachache, kwa kisingizio cha siasa, hasira kali ama jazba bila kuchukuliwa hatua. Shughuli za siasa ni kitu kimoja na fujo ama vurugu za jazba ni kitu kingine.
"Upo umuhimu wa kutenganisha mambo hayo mawili na hapana budi mamlaka za kisheria ziheshimiwe na watu wote bila kujali itikadi zao kisiasa au kijamii.
"Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, walipitisha sheria ya vyama vya siasa na sheria ya Jeshi la Polisi, sheria hizo zimeweka utaratibu na miongozo ya kufuata katika kuratibu mikusanyiko mbalimbali ikiwamo maandamano na mikutano ya hadhara.
"Haki, wajibu na utaratibu wa kufuatwa na vyama vya siasa pamoja na Jeshi la Polisi kupewa taarifa ya mikusanyiko imefafanuliwa pia katika sheria hizo. Kwa hali hiyo ifahamike wazi kwamba Jeshi la Polisi halina nia mbaya ya kuzuia mikusanyiko ama maandamano," awesema IGP Mwema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari.
Tayari baadhi ya maeneo ya miji mikuu na yenye ushawishi wa kisiasa yamekumbwa na vurugu kubwa zilizoisukuma Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani, kutoa tamko Bungeni kuelezea hali hiyo, ambayo inazidi kuashiria kuwapo kwa vuguvugu kali dhidi ya serikali.