Stroke
JF-Expert Member
- Feb 17, 2012
- 34,669
- 40,917
Baada ya CHADEMA kuweka mkakati kwa mpango ambao tayari umeshafeli kabla ya utekelezaji wake walioupa jina la UKUTA, ningependa kuwasahihisha kidogo na kuwakumbusha kua neno sahihi linalofaa badala ya hilo wanalolitumia ni CHAKUTA.
CHAKUTA ni neno sahihi kwani mwenendo mzima wa CHADEMA umekuwa ni katika kupinga kila jambo linalofanyika sasa, ninaposema CHAKUTA namaanisha Chama cha Kupinga Kila kitu Tanzania, hilo linafaa sana kwa sasa.
Hivyo basi badala ya kupoteza muda kwenye UKUTA, ni vyema wakaelekeza nguvu na kili katika CHAKUTA maana huko kuna uwezekano wa kufanikiwa zaidi kuliko huko walipokuanza.
Vile vile nishauri kwamba UKUTA haitafanikiwa kwani siasa za nchi hii zimebadilika sana, na wananchi hawapo tayari tena kuona wakipata matatizo kwa ajili ya lengo lisilokuwa na faida kwao, CHADEMA kimewakwaza watu wengi hivyo imani imewatoka kabisa.
Ukiachana na hilo la kupoteza imani kwa wananchi, Serikali ya sasa inaonekana kufanya kazi yake kwa kugusa mambo nyeti yaliyokua yakipiganiwa na wengi kwa muda mrefu, hivyo movement hii kuonekana kama jitihada za makusudi za kukwamisha nia njema iliyopo kwa serikali ya sasa.
Wanachi wameamua kuachana na siasa za maandamano na kufanya kazi.
CHAKUTA ni neno sahihi kwani mwenendo mzima wa CHADEMA umekuwa ni katika kupinga kila jambo linalofanyika sasa, ninaposema CHAKUTA namaanisha Chama cha Kupinga Kila kitu Tanzania, hilo linafaa sana kwa sasa.
Hivyo basi badala ya kupoteza muda kwenye UKUTA, ni vyema wakaelekeza nguvu na kili katika CHAKUTA maana huko kuna uwezekano wa kufanikiwa zaidi kuliko huko walipokuanza.
Vile vile nishauri kwamba UKUTA haitafanikiwa kwani siasa za nchi hii zimebadilika sana, na wananchi hawapo tayari tena kuona wakipata matatizo kwa ajili ya lengo lisilokuwa na faida kwao, CHADEMA kimewakwaza watu wengi hivyo imani imewatoka kabisa.
Ukiachana na hilo la kupoteza imani kwa wananchi, Serikali ya sasa inaonekana kufanya kazi yake kwa kugusa mambo nyeti yaliyokua yakipiganiwa na wengi kwa muda mrefu, hivyo movement hii kuonekana kama jitihada za makusudi za kukwamisha nia njema iliyopo kwa serikali ya sasa.
Wanachi wameamua kuachana na siasa za maandamano na kufanya kazi.